Huu ni uthibitisho mwingine kuwa Jeshi letu la Polisi limekosa weledi

ibesa mau

JF-Expert Member
Sep 17, 2015
2,109
1,692
Hii tabia ya kuzoa zoa tu vijana mtaani na kuwapeleka depo miezi 6 halafu unamwajiri ni uthibitisho tosha kwamba ipo haja ya kuongeza muda wa mafunzo toka miezi sita hadi miaka 3 hadi 5. Askali wetu wamekosa weledi wa kupambana na matukio .

Askali anakwenda kwenye kupambana na maandamano ya watu wasio na silaha halafu ameambiwa achukue risasi za rubber yeye anachukua risasi za moto,michezo kama hii tukiiachia italeta madhara kwa viongozi wetu wa juu.

Wahenga wanasema mchelea mwana kulia, hulia yeye, ipo siku inaweza ikatokea kiongozi wa juu akakagua gwaride kama mchezo wao watabeba risasi za moto baadala ya rubber halafu akatokea kichaa mmoja akamuwasha risasi ya moto sijui hapo tutasemaje.

Nashauri muda wa mafunzo uongezwe lakini pia vijana wanaochukuliwa waangaliwe. vijana wamekaa kijiweni , wamevuta bangi uraiani halafu unamchukua unampa mafunzo miezi sita anakuwa askali hii tabia iachwe waangaliwe vijana wa kuwachukua wachukuliwe hata division one na two.

Kuna kipindi cha miaka ya katikati vijana hadi wenye ziro waliingizwa jeshini hao ndio wanao tuulia watoto wetu wa vyuo wasio na hatia.
Askali wetu wanatumia nguvu nyingi kuliko akili.

Tubadilishe mitaala yao muda wa mafunzo uongezwe kijana akae hata miaka 5 ajifunze na sheria za nchi hii itasaidia kuwa na jeshi lenye weledi mkubwa kama nchi za wenzetu kenya na nyinginezo.
 
Kaka/dada, mambo mengine tuwaachie wanaofahamu. Polisi hawajichagulii silaha ya kuondoka nayo kituoni kama wananchi wanaochagua zana za kwenda nazo kwenye harambee.

Kama ukiwaona na virungu basi ndio maelekezo na ukiona wameambatana na deraya pia ni maelekezo.
 
Badhani hapa mbaka ieajibikaji utokee ndio kutkuwa na mabadiliko.

Kwenye mpira timu ikifanya vibaya kocha ndio anafukuzwa, hapo shida ipokwa kocha.

Kocha ajipime.
 
Kaka/dada, mambo mengine tuwaachie wanaofahamu. Polisi hawajichagulii silaha ya kuondoka nayo kituoni kama wananchi wanaochagua zana za kwenda nazo kwenye harambee.

Kama ukiwaona na virungu basi ndio maelekezo na ukiona wameambatana na deraya pia ni maelekezo.

Hata kufyatua risasi lazima itoke order "haya sasa piga" ama kwa kuuwa au kujaruhi toka kwa boss wake.
 
Nikakumbuka yule Waziri wa UK aliyejiuzulu kwa kuchelewa kidogo bungeni, kutokana na uungwana wake bunge zima hadi upinzani walishout no asijiuzulu, huku kwetu historia ya mwisho ni mzee Mwinyi.
 
Tuanzie hapo.
Is it lack of training?
Is it lack of supervision?

Au jamaa(polisi) wamekuwa instructed , shoot to kill!

Eitherway, Tanzania Police Force and proffessionalism vina jionyesha sasa kuwa mafahali wawili wasiokaa nyumba moja.
 
Master remote controller at work ndio sababu akawekwa Kamanda Zerro easily manipulated
 
Tatizo ni Chama Cha Majambazi (CCM) kinatumia ugaidi kutawala. Polisi ni moja ya zana zao.
 
Tuanzie hapo.
Is it lack of training?
Is it lack of supervision?

Au jamaa(polisi) wamekuwa instructed , shoot to kill!

Eitherway, Tanzania Police Force and proffessionalism vina jionyesha sasa kuwa mafahali wawili wasiokaa nyumba moja.
Kama kweli unao weledi, ukiwa instructed to shoot to death an innocent people what u do is u turn around and shoot the commander!!!
 
Polisi hawana tatizo tatizo ni mfumo mbovu na katiba inayowafanya viongozi kuwa wakuu kuliko Mungu muumba wa mbingu na ardhi.
Huyu askari wa ngazi za chini yeye anaubavu gani wa kupingana na amri na matamshi ya kuwaita waasi wale wote wanaopinga CCM na serikali yake.

Katiba ya Warioba ndilo jibu la haya matatizo.
Mtu mmoja ana mamlaka makubwa saba humu duniani.
Mungu yuko chini ya watawala wa hizi nchi maskini.
Matokeo yale zimekua ni nchi zilizojaa laana ,unyonge,hofu,vitisho, vifo, ubabe, uonevu, roho mbaya, unyama, unyanyasaji, viburi, na kila aina ya majivuno kwa watawala huku wananchi wakibaki kama foot step za watawala.

Dawa ya yote ni kuwa na katiba inayomnyima mtu mmoja kupanga mpaka riziki za wanadamu.
Ni mifumo ya namba 666 yaani utawala wa binadamu kujikweza kama mungu na kupanga kila kitu . Nani auze na nani asiuze.Nani kesho akiamka ni mkuu wa idara na nani analala njaa gerezani au hata kuuawa.

Tumewatengeneza wakina Nebkadreza wenyewe kupitia katiba yetu. Bara la Afrika Tumeamua kurudi enzi za wafalme waliojikweza na kuwa miungu kama akina Firauni.
Leo hii tunasikia wakuu wa mikoa wakijikweza kuwa na kuona Mungu si chochote juu ya amri zao.

Jeshi la Polisi liko vizuri sana kiurendaji lakini miungu iliyoko juu ya maisha yao, vyeo vyao,riziki zao na hatima yao ndani na nje ya kazi zao.
Kila mmoja anahofia ugali wake. Leo hii hata wafanyakazi wa idara nyingine wameufyata kwa hofu kuu. Hawaogopi chochote bali ugali wao kuondolewa na wale waliokwezwa na katiba na wao wakajiinua juu ya kila kiumbe na hata kujiona kuwa wamekuja kudumu humu duniani milele.
Kama sanduku la kura linabebwa mbele ya polisi bila hofu kwa nini mtu asiuawe mbele ya polisi bila woga.

Ndani ya CCM kwa sasa kuna watu wenye uwezo wa kufanya chochote kwa kuwa wao wamejiona kuwa ni miungu watu hakuna hukumu wala adhabu juu yao. Wanaweza wakafanya wanachotaka kwa manufaa ya ushindi wao naadaraka yao yanayowapa ugali.

Kama mtu wa CCM anamkata mtu wa chadema au CUF mapanga bila kukamatwa kwa nini tusiwaze kuwa hata risasi inaweza ikarushwa na hao magreen guard wasioopoa chochote mana wametoka mbinguni na kamwe hakuna wa kuwagusa?

Tukiwalaumu polisi tuangalie na upande wa pili wa shilingi.
Kama Mkurugenzi anavunja sheria wazi ili tu abakie madarakani itakuaje kwa polisi. Yani Mkurugenzi akifanya kazi yake kwa weledi na CCM ikashindwa kihalali chini ya mfalme polepole inakua ndio mwisho wa ukurugenzi wake basi hali hiyo itakua iko mpaka kwa polisi.
Nakumbuka Spika Ndugai aliwahi kutoa amri askari waliokiwa wamefanya kazi yao kwa weleni wa kumtoa Sugu nje kistarabu kama Mbunge mwenye haki zake. Ndugai alisema hataki askari anayemtoa mheshimiwa kistarabu bali anatakiwaa amtoe harakaharaka na kwa nguvu bila kuwa nyoronyoro.
Hapa tuwe na kumbukumbu kwa maelekezo ya ndugai kwa askari wa bunge dhidi ya wapinzani.
Walielekezwa kuondoa huruma wakati wa kudili nao.
Hakuna aliyejali.
 
Police sioni hatia yao wao wanatekeleza oder zinazotoka huko majuu hawezi kuondoka na silaha ambayo hajaruhusiwa pia hawez kushoot bila kuruhusiwa me binafsi sioni hatia yao ila hao wakubwa ndo wanatuua kila kukicha
 
Tubadilishe mitaala yao muda wa mafunzo uongezwe kijana akae hata miaka 5 ajifunze na sheria za nchi hii itasaidia kuwa na polisi wenye weledi mkubwa kama nchi za wenzetu kenya na nyinginezo.

Mengi uliyoongea nilitikisa kichwa, maana ulikuwa unaelekea, lakini hapa umechemka. Kwa maana hao uliowatolea mfano juzikati tu ndio nao walikuwa wanafanya vitendo hivyo hivyo.
Na hapo kwenye nchi nyinginezo ni bora ungesema ni nchi za nje lakini sio afrika hii.
 
Back
Top Bottom