Gluk
JF-Expert Member
- Mar 23, 2017
- 1,855
- 2,953
Habari wanaJF;
Leo nataka niongelee UTAPELI uliohalalishwa, nao ni hizi kampuni zinazofanya biashara ya mtandao
(Network Marketing) Nimeshudia vijana wengi wakilizwa na hizi biashara hususani mawanawake na wanafunzi wa chuo.
Hawa jamaa wanakushawishi kwa ahadi kuwa ukitoa kiasi fulani utaingiza watu kadhaa na wewe utajipatia mamilioni ya pesa kwa lugha yao huita pea ( pair).
Ukijiroga ukaingia unabaki na kazi ya kuanza kuvaa shati nyeupe na suruali nyeusi na kuaminisha kuwa wewe ni bilionea mtarajiwa kumbe moyoni unaugulia maumivu..
Siku moja niliwahi kuhudhuria semina zao uli kufanya utafiti wangu mmoja kasimama mbele na kujinasibu kuwa kafanikiwa sana na anaingiza mamilioni ya pesa kwa wiki na anabadili magari apendavyo, jioni tulivyotoka nikamkuta standi ya daladala na tugagombania DCM za Mbagara pamoja.
NB: Ukiitwa kwenye fursa tambua kuwa wewe ndiyo fursa yenyewe.
Leo nataka niongelee UTAPELI uliohalalishwa, nao ni hizi kampuni zinazofanya biashara ya mtandao
(Network Marketing) Nimeshudia vijana wengi wakilizwa na hizi biashara hususani mawanawake na wanafunzi wa chuo.
Hawa jamaa wanakushawishi kwa ahadi kuwa ukitoa kiasi fulani utaingiza watu kadhaa na wewe utajipatia mamilioni ya pesa kwa lugha yao huita pea ( pair).
Ukijiroga ukaingia unabaki na kazi ya kuanza kuvaa shati nyeupe na suruali nyeusi na kuaminisha kuwa wewe ni bilionea mtarajiwa kumbe moyoni unaugulia maumivu..
Siku moja niliwahi kuhudhuria semina zao uli kufanya utafiti wangu mmoja kasimama mbele na kujinasibu kuwa kafanikiwa sana na anaingiza mamilioni ya pesa kwa wiki na anabadili magari apendavyo, jioni tulivyotoka nikamkuta standi ya daladala na tugagombania DCM za Mbagara pamoja.
NB: Ukiitwa kwenye fursa tambua kuwa wewe ndiyo fursa yenyewe.