Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 92,211
- 113,520
Nilidhani huyu mama yenu atakuwa tofauti na waliomtangulia.
Kwamba hatoendeleza huu ushamba wa viongozi mbalimbali wa serikali na idara kwenda uwanja wa ndege kumsindikiza aendapo safari na pale arudipo toka safarini.
Yaani majitu yote hayo, kuanzia makamu wa Rais, mawaziri, sijui mkuu wa mkoa, mkuu wa jeshi la polisi, mkuu wa jeshi la wananchi, viongozi wengine waandamizi wa kijeshi na kiaskari [nadhani nimemuona na wa magereza hapo], na chawa wengine.
Si ajabu hata yale Maharage ya Tanesco yalikuwepo hapo.
Huu ushamba ni matumizi mabaya ya muda wa uzalishaji.
Badala ya kuwa maofisini huko na sehemu zingine za kazi, majitu yote hayo yanaenda kurundikana na kupanga mstari kumsindikiza Rais akienda Ulaya.
Ushamba na ujuha wa kiwango cha juu kabisa.
Na Rais naye hana busara ya kuwaambia hakuna haja ya kunisindikiza wala kunipokea uwanja wa ndege, na badala yake endeleeni kupiga kazi.
Sisi bado sana aisee!