Huu ni Ukweli wa Dr Slaa??

John Mnyika

JF-Expert Member
Jun 16, 2006
712
1,240
Kumetolewa tuhuma kadhaa kuhusu ubadhirifu wa fedha za wakatoliki zikimlenga Dr Slaa; kwa bahati mbaya hoja hizi zimeanza kujitokeza sasa wakati ambapo Dr Slaa yuko katika heka heka za kuibua ubadhififu BOT, Richmond, Meremeta nk. Kwa vyovyote vile kuchanganya mjadala wa Balali na BOT na Dr Slaa kutapoteza mwelekeo wa mjadala mmoja wapo. Hivyo nimefungua thread hii ili yule anayetaka kumjadili Dr Slaa amjadili hapa. Kule kwa BOT mjadala wa BOT na Balali uendelee kujadiliwa bila kuingiliwa.

Kwa wale walioanzisha hoja kuwa Slaa alifanya ubadhirifu wa mali za kanisa katoliki; huu ndio wasaa wenu sasa wa kutoa facts.

Mimi nimeshaweka maoni yangu bayana kuwa namfahamu Slaa kwake Karatu na Sinza DSM pia ni jirani yangu. Ni mtu wa kawaida sana.

Na pia najua ni kwa nini alitoka upadri kanisa katoliki(ingawa sakramenti ya upadri haifutiki).

Wenye taarifa tofauti waziweke hapa basi zijadiliwe. Kule tuendelee kujadili BALALI, BOT na UFISADI katika taifa letu.

JJ
 
Nd. Mnyika!
Nitashukuru kama utatufahamisha ni kwanini Ng. Slaa aliacha kuwa Padre( Ingawa Sakramenti ya Upadre haifutki).
What happened?
 
Nd. Mnyika!
Nitashukuru kama utatufahamisha ni kwanini Ng. Slaa aliacha kuwa Padre( Ingawa Sakramenti ya Upadre haifutki).
What happened?

Kaka Brutus,

Naomba nisijibu chochote kwa sasa; nawasubiri kwanza hao walioanzisha hili suala waweke their versions of the storty.

1. Watueleze ni ubadhirifu gani huo wa mali wakatoliki alioufanya kamba ambavyo wameelekeza shutuma kwake?

2. Ni sababu zipi zilizomfanya atoke katika upadri?

Lengo langu kuanzisha hii thread ni ili kuulinda ule mjadala wa BOT na Balali usipotezwe mwelekeo.

JJ
 
Lowasa Alipokwenda Canada Wakatoliki Walimpa Bilioni 1 Mbona Watu Hawaulizi Hizo Pesa Zilipelekwa Wapi?
 
Nilifiriki wanataka kumzungumzia Dr. Slaa... Lowassa watu wanaweza kumuuliza nadhani, hasa wakijisikia kuanzisha mada ya kuulizia hizo hela bilioni moja alizopewa na "wakatoliki".
 
Bob,

Hebu naomba nielimishe hapa........Legacy ya Dr.Slaa relatively to commitment na nidhamu katika uongozi........najiuliza hivi kutokana na maelezo ya kinyau hapo juu kama ni kweli
 
Mi nadhani issue ya wakatoliki waachieni Wakatoliki! Kama aliwaibia watampeleka wanakojua wao au walishampa adhabu-mi sijui.... hii ya Balali waachieni WANANCHI wa TANZANIA ambao ni mimi na wewe-kama ametuibia tujue pa kumpeleka! kwa sababu issue ya Balali ni ya watanzania wote..wenye dini na wasio na dini. Personally, Iam more interested katika issue ya Balali kwa sababu ni kodi zetu, in otherwords Watanzania wote tuna hisa pale BOT! and everything is done in the name of wananchi ambao ndo sisi na sio wakatoliki au waislamu!

If Iam not a catholic, why should I be bothered in whats happening in Rome or msimbazi kwa Pengo for that matter?-as long as it doesnt affect me (ndo human rights zenyewe tunazozipigia kelele kila siku ati!-uhuru wa kujiamlia mambo!)Sioni sababu ya kumuandama Slaa in what transpired in Church/with his former employer, kama kuna anayetaka kujua zaidi..akamuulize cardinally Pengo! But for Balali lazima tuwe naye sambamba..kwa sababu what is at stake is the survival of our nation. Kama Slaa aliiba hela za umma za wananchi wa Karatu..or anything touching maslahi ya WATANZANIA (in our country, Catholics are Tanzanians but Tanzanians are not catholics)..then, we should argue on that line.....Au mwenye data ambazo anaamini zina compromise intergrity za huyu bwana kuweza kuwa kiongozi azitoe kusudi wananchi tupime tujue.....

Perhaps wengine watasema kwamba namtetea Slaa..wala hasha (infact simfahamu vyema..)....objectively ni kuacha unafiki. (mserengeti ameelezea vyema hili)....tulipo mpigia kura JK tulimuuliza na watoto wangapi? ana magirlfriend wangapi? amelala na wanawake wangapi? EL vile vile..tukiamua kuchimba huko kuangalia morality za watu..Hakuna msafi- mimi na wewe, ndo maana hatukuweka morality kama kigezo wakati tunachagua hawa viongozi..Bali tulitaka viongozi wasafi AMBAO SI WALA RUSHWA, wanaoweka maslahi ya WATANZANIA mbele! Kama Slaa ni mla rushwa..mtuambie ila sio hadithi za kanisani na sadaka....Infact kama aliibia kanisa..wakatoliki ndo inabidi wamshikie bango...Ni kama ukute Mikuki namlaumu Sheikh Simba kwa kula swadaka ya waislamu..wapi na wapi?

What I see kuna watu humu wanajua ukweli wa hii issue ya BOT na wanajaribu ku-question intergrity ya bwana Slaa, kusudi watupoteze waendelee kula na Balali and co..their ill-gotten wealth of poor Tanzanians-though unfortunately wanashindwa kujenga hoja zenye mashiko. Balali akapumzike..awe cleared na tuhuma..then arudi kazini..kama hakuiba! Period.
 
i_will_use_google_before_asking_dum.jpg

Google is your friend
 
Sina uhakika na kitu kilocho anza kujadiliwa hapa, ila maoni yangu ni kuwa; (tukichukulia kama yaliyosemwa yote ni ya kweli), cha kujiuliza hapa ni kuwa: Je, alitubu? Je, alizilipa hizo pesa? Je,hajarudia kosa kama hilo tena? Je, sasa hivi anasaidia vipi jamii? n.k.

Nimeuliza maswali hayo kwani mimi naona ndiyo msingi mzuri wa maendeleo, kama mtu kafanya kosa ambalo tunaweza kusema ni la kiwango cha kawaida katika jamii (kwani makosa yapo tu nyakati zote), yanini kuendelea kumshutumu mtu huyo kama atakuwa amejirekebisha na ametubu makosa yake..

Kuna mifano mingi inaweza kutolewa hapa, lakini nitakao toa ni ule wa David Cameron, Kiongozi wa upinzani Uingereza. Huyu alishutumiwa kuwa alivuta bangi akiwa chuoni, walipo muhoji wakati wa kuchaguliwa kwake hakujibu swali hata kidogo kama kweli alifanya hivyo.

Muhimu sasa, huyo Cameron alichaguliwa kuwa kiongozi bila kujali yaliyo pita au yanayosadikiwa kuwa ni makosa ya kawaida katika jamii hata kama mtu huyo hakukiri au kutubu makosa yake ya awali, kwani uwezo wake wa kuwa kiongozi kwa wakati huu ndiyo uliotiliwa maanani zaidi.

Nakubali kuwa kuna makosa fulani fulani ambayo mtu ukitenda katika jamii haya sahuliki na pengine hayasameheki kabisa. Ndiyo maana nimesema kuwa msingi wa maendeleo kama wananchi watautambua ni hayo maswali, kwani yakijibiwa, swali la mwisho likawa kuwa huyo Dr. Slaa anaendeleza demokrasia na kusukuma gurudumu la maendeleo kwa kuhoji wabadilifu katika jamii, basi makosa yake yanaweza kusahaulika na kusameheka kama hayo maswali mengine hapo juu atakuwa ameyatekeleza ipasavyo.

SteveD.
 
Nyinyi wapenda udini mnaboa kweli kweli...halafu mko-sensitive sana. Sometime I wish everybody was like me....daaaamn it!!
 
i_will_use_google_before_asking_dum.jpg

Google is your friend

Sidhani kama kwenye Google unaweza kupata kila kitu and by the way mtu makini hawezi kurusha majibu kama wewe unavyofanya, mtu makini anapotoa shutma anatakiwa atoe ushahidi wa data au kutoa link ya kuweza kupatikana data hizo, sio kurusha maneno tu? nenda kwenye Google and the like.

kuwa mwerevu
 
Huyu jamaa kwanza namsihi aache kujipachika title ya "doctor" kwani nyanja aliyosomea (Canon Law au sheria ya Kanisa Katoliki) haina faida yoyote kwake yeye mwenyewe achia mbali wapiga kura wake (Wakristo kwa Waislamu) na Watanzania wote kwa ujumla haswa baada ya kuamua kuondoka upadri.

Ni kweli Wilbrod Slaa alitumia cheo chake akiwa kama padri na katibu mkuu wa TEC (Baraa la Maaskofu Tanzania) kujilimbikizia mali moja wapo ikiwa ni kujijengea nyumba Sinza kutumia mkandarasi wa Kanisa Katoliki wakati bado akiwa kama padri na Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC). Habari hii wala siyo siri kwani iliandikwa hata na gazeti la "Kiongozi" enzi hizo mwishoni mwa miaka ya 80.

Pia huyu bwana anaeleweka kuwa aliachiwa nyumba/estate Ujerumani kwenye mirathi na mama mmoja wa Kijerumani, hii pia akiwa kama padri.

Kuhusu tuhuma za uzinzi akiwa kama padri, nadhani hapa wala hakuna sababu ya ushahidi kwani ni wazi kuwa suala hili ndilo lilichangia kwa kiasi kikubwa uamuzi wake wa kuachana na upadri na kuamua kumuoa hawara yake wa siku nyingi. Huyu mama alikuwa ni changudoa tu mmoja pale Arusha ambaye special clientele yake ilikuwa ni mapadri tu. Mara baada ya kumnasa Wilbrod Slaa na hatimaye kufunga naye ndoa, huyu mama akaonekana Dar akitanua na magari ya kifahari. Sasa jiulize utajiri huu wa haraka haraka ulitokea wapi kama siyo Wilbrod Slaa kutumia visivyo vyeo vya upadri na ukatibu mkuu wa baraza la Maaskofu Tanzania kujilimbikizia mali na kuiba pesa za kanisa?
 
Yote hayo hayaondoi ukweli wa huo unyang'au anaokemea wakati wale mnaowaona wasafi wakiwa wanakenua meno na kujikuna vichwa...
 
Swali: Hivi Toka Lini Padri Akaacha Upadri Na Kuoa? Huyu Slaa Aliacha Upadri Kisha Akamwoa Huyo Mwanamke Aliyempa Mimba
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom