Huu ni ujasiliamali halali au haramu wanaofanya wauza magazeti?

TUJITEGEMEE

JF-Expert Member
Nov 6, 2010
23,914
23,075
WanaJF, jana nilikwenda kwa wauza magazeti kununua gazeti fulani. Kufika pale nikakuta gazeti nililolihitaji halipo. Kwa kuwa nilikuwa nalihitaji sana gazeti hilo nikalazimika kumuuliza muuzaji wa magazeti mahali ambapo niweza kupata gazeti hilo. Alinijibu kuwa nipitie baada ya masaa matatu atakuwa amelipata.Baadaye nilikuja kugundua kuwa wauza magazeti hao ukodisha magazeti kwa watu kwa malipo kati ya Tsh.100 mpaka 300 kulingana na muda atakoutumia (aliyelikodi) kulisoma,aina na bei ya gazeti hilo. Malipo hayo huchukuliwa na wauzaji wa magazeti hayo.Magazeti hayo yaliyokodiwa wakati mwingine ukosa wateja wa kuyanunua hivyo urudishwa kwa wakala wa magazeti hayo. WanaJF kitendo hiki cha wauza magazeti ni ujasiriamali au uharamu (hujuma ya kifedha kwa wamiliki wa magazeti)?
 
WanaJF, jana nilikwenda kwa wauza magazeti kununua gazeti fulani. Kufika pale nikakuta gazeti nililolihitaji halipo. Kwa kuwa nilikuwa nalihitaji sana gazeti hilo nikalazimika kumuuliza muuzaji wa magazeti mahali ambapo niweza kupata gazeti hilo. Alinijibu kuwa nipitie baada ya masaa matatu atakuwa amelipata.Baadaye nilikuja kugundua kuwa wauza magazeti hao ukodisha magazeti kwa watu kwa malipo kati ya Tsh.100 mpaka 300 kulingana na muda atakoutumia (aliyelikodi) kulisoma,aina na bei ya gazeti hilo. Malipo hayo huchukuliwa na wauzaji wa magazeti hayo.Magazeti hayo yaliyokodiwa wakati mwingine ukosa wateja wa kuyanunua hivyo urudishwa kwa wakala wa magazeti hayo. WanaJF kitendo hiki cha wauza magazeti ni ujasiriamali au uharamu (hujuma ya kifedha kwa wamiliki wa magazeti)?

Tanzania kwa sasa kila mtu anatafuta mrija wake wa kufanyia ufisadi kulingana na nafasi yake. Wanasena

kila mbuzi anakuala kwa urefu wa kamba yake, au kwa kuazima maneno ya Generali ulimwengu, "Kila

mtanzania sasa anajaribu kutengeneza EPA yake, wengine EPA zao maalbino, traffic police EPA zao rushwa

za barabarani, wengine Richmond, wengine Meremeta, etc". Kwa hiyo tusishngae kuona wauza magazeti

nao wamegundua "EPA" yao ya kufanya kaufisadi mdogo mdogo. Kwa ufupi, Taifa hili limepoteza maadili

kuanzia kwenye ngazi ya familia mpaka Taifa. Limekuwa Taifa la watu wanaoishi kwa ujanja ujanja, kila mtu

anataka kula kwa ulaini. Haya yanayofanywa na wauza magazeti ni sehemu ndogo sana ya mfumo hatari

na kansa ya udhalimu inayoendelea kuitafuna nchi yetu. Kwa mtindo huu hatuwezi kufika mbali. Tukemee

maovu, tuache maovu!
 
saloon za kiume (babashopu) karibia zote mijini hukodisha magazeni. wakibisha waende mahakamani kwa kuwachafulia nitaleta ushahidi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom