peter daudi
Senior Member
- Sep 16, 2012
- 112
- 30
Jamaa mmoja alikuwa na mawasiliano na dada mmoja(wakiitana mme/mke).jamaa alikuwa masomoni Dar na dada alikuwa nyumbani .Sasa muda wa mazoezi ukafika, jamaa akaenda mazoezini(kufundisha) karibu kabisa na yule dada(ndani ya wilaya).Basi wakakubalian kukutana kwa maana ya dada kwenda kwa jamaa.Dada aKasafiri salama na kufika kwa jamaa.Usiku mzima ukapita jamaa "NO ACTION" .Dada kakosa raha kabisa kiasi kwamba hata chai ikawa ni ngumu kunywa.Mchana ukapita,usiku mwingine tena "NO ACTION". Kesho yake dada akakosa amani zaidi na kusababisha kuwa mtu mwenye huzuni mda wote.Basi mwalimu wakike(naye alikuwa mazoezini) akapewa jukumu la kumdadis yule dada na akapata kufunguku kuwa jamaa hataki "KUDO".Kwanza analala na nguo na nikimsogelea anashuka kitandani na kutandika shuka chini na kulala.Jamaa alipo ulizwa akasema ni dhambi.Dada(mwalimu) akamwelekeza juu ya huzuni aliyokuwa nayo rafiki yake na sababu yake, jamaa akajibu kwamba atalekebisha ile hali.Usiku tena "NO ACTION".Asubuhi dada(mwalimu) anakuta bado yule dada yuko na huzuni kiasi cha macho kuwa mekundu.Basi yule dada akashauriwa kurudi nyumbani(SIKU YA NNE) kwao kama alivyokuja. Sasa Je! Huu ni ugonjwa au ndo kumwogopa mungu?.