Lunyungu
JF-Expert Member
- Aug 7, 2006
- 8,873
- 1,906
Na Rehema Mohamed
KUNDI maarufu la sanaa za maigizo The Comedy limemaliza mkataba wake na kituo cha televisheni cha East Afrika (EATV) kinachorushwa kila siku ya Alhamis.
Kutokana na kumalizika mkataba huo kipindi hicho maarufu hakitarushwa kuanzia Alhamis ijayo. Kundi hilo liliingia mkataba wa mwaka mmoja na miezi nane kufanya kazi na EATV uliofikia ukingoni juzi.
Ukiondoa Ze Comedy, naye Mratibu wa kundi hilo Sekioni David amesitisha mkataba na kituo hicho na sasa anaelekeza nguvu zake ndani ya kundi hilo.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mkurugenzi Mtendaji wa Kundi hilo, Isaya Mwakilasa (Wakuvanga) alisema wameamua uamuzi huo ili kupata mapumziko kwa muda kabla ya kuendelea na sanaa hiyo.
Mwakilasa alisema wanasikitika kumaliza mkataba na EATV na hivyo wameamua kurudi nyumbani kujipanga upya lakini pia wanaweza kuingia mkataba mpya endapo watakubaliana.
"Mkataba wetu na EATV umeisha nasi tumeamua kurudi nyumbani kupumzika kwa nia njema, hasa kwa maslahi ya wengi zaidi na tulikuwa tukifanya kazi nao vizuri na huu si mwisho wetu," alisema Mwakilasa.
Mwakilasa alikanusha taarifa kuwa Ze Comedy lina mpango wa kuingia mkataba mpya na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC 1) na kuongeza kuwa sanaa ni ajira yao hivyo kama watahitajika hawasita kuingia mkataba na kituo hicho.
Kundi hilo limejipatia umaarufu mkubwa ndani na nje ya Tanzania kutokana na ubunifu wao ikiwa ni pamoja na kuwakosoa baadhi ya viongozi wa Serikali wanaokwenda kinyume na maadili ya kazi.
Kundi la The Comedy linaundwa na wasanii sita ambao ni Joseph Shamba 'Vengu', Alex Chalamila 'McRegan', Mjuni Syliveri 'Mpoki', Emmanuel Mgaya 'Masanja', Lucas Mahuvile 'Joti na Mwakilasa.
KUNDI maarufu la sanaa za maigizo The Comedy limemaliza mkataba wake na kituo cha televisheni cha East Afrika (EATV) kinachorushwa kila siku ya Alhamis.
Kutokana na kumalizika mkataba huo kipindi hicho maarufu hakitarushwa kuanzia Alhamis ijayo. Kundi hilo liliingia mkataba wa mwaka mmoja na miezi nane kufanya kazi na EATV uliofikia ukingoni juzi.
Ukiondoa Ze Comedy, naye Mratibu wa kundi hilo Sekioni David amesitisha mkataba na kituo hicho na sasa anaelekeza nguvu zake ndani ya kundi hilo.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mkurugenzi Mtendaji wa Kundi hilo, Isaya Mwakilasa (Wakuvanga) alisema wameamua uamuzi huo ili kupata mapumziko kwa muda kabla ya kuendelea na sanaa hiyo.
Mwakilasa alisema wanasikitika kumaliza mkataba na EATV na hivyo wameamua kurudi nyumbani kujipanga upya lakini pia wanaweza kuingia mkataba mpya endapo watakubaliana.
"Mkataba wetu na EATV umeisha nasi tumeamua kurudi nyumbani kupumzika kwa nia njema, hasa kwa maslahi ya wengi zaidi na tulikuwa tukifanya kazi nao vizuri na huu si mwisho wetu," alisema Mwakilasa.
Mwakilasa alikanusha taarifa kuwa Ze Comedy lina mpango wa kuingia mkataba mpya na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC 1) na kuongeza kuwa sanaa ni ajira yao hivyo kama watahitajika hawasita kuingia mkataba na kituo hicho.
Kundi hilo limejipatia umaarufu mkubwa ndani na nje ya Tanzania kutokana na ubunifu wao ikiwa ni pamoja na kuwakosoa baadhi ya viongozi wa Serikali wanaokwenda kinyume na maadili ya kazi.
Kundi la The Comedy linaundwa na wasanii sita ambao ni Joseph Shamba 'Vengu', Alex Chalamila 'McRegan', Mjuni Syliveri 'Mpoki', Emmanuel Mgaya 'Masanja', Lucas Mahuvile 'Joti na Mwakilasa.