Elections 2010 Huu ni mwelekeo mpya au?

WomanOfSubstance

JF-Expert Member
May 30, 2008
5,457
956
Katika hali ya kawaida, mwakilishi wa wananchi mfano Mbunge au kiongozi mwingine wa kutumikia watu huchaguliwa kutokana na kukamilisha vigezo kama vile utendaji uliotukuka, uchapa kazi unaoendana na uadilifu, umakini, usikivu nk.

Aidha kunaweza kuwepo na kigezo kingine cha "affirmative action" kwa maana ya kutoa fursa kwa makundi maalum, ili kuhakikisha wale walioko pembezoni ( marginalised) kwa sababu ya pamoja na mambo mengine jinsia/jinsi, ulemavu, umri nk.

Uchaguzi wa mwaka huu umenipa somo kuwa inawezekana mtu akapata kura tena za kutosha kwa vile "anaonewa huruma". Mfano mzuri ni hoja ya baadhi ya wachambuzi wa mambo wanaosema kuwa Mrema wa TLP alichaguliwa kwa sababu "alionewa huruma" na wapiga kura kutokana na afya yake na kwamba akiwa bungeni basi ataweza kupata matibabu nk.

Hili linanitatiza kidogo, na kuniachia swali - hivi ni kwanini tunahitaji uwakilishi bungeni? Tunachaguwa wabunge wakajiwakilishe wenyewe kwa maana ya kutatua matatizo binafsi au tunawachagua ili kuweza kuratibu maswala ya mbalimbali ya maendeleo yenye kuhitaji ufumbuzi wa kimkakati - ikiwemo kufikisha kunakohusika? Nijuavyo mimi mbunge ni mjumbe wetu tunayemtuma akatusemee maana watanzania wote milioni zaidi ya 40 hatuwezi kujipeleka bungeni tukaseme kila kinachotuhusu au kutukera.Ingekuwa vurugu na haiwezekani kamwe.Mjumbe huyu tunamtarajia atufikishie yale tunayomtuma kama yalivyo na atuletee jibu pia!

Najaribu kufikiria - endapo Mrema atatumia fursa hiyo kwa manufaa binafsi kama "ilivyobarikiwa" na wapiga kura wake ( tuseme asilimia 60 ya wana-Vunjo waliopiga kura) je wale ambao hawakumchagua wakiwemo wa vyama pinzani, na walioshindwa kupiga kura kwa sababu mbalimbali ikiwemo kutokuwa na sifa ya kupiga kura kwa mfano watoto chini ya miaka 18, watawakilishiwa vipi maslahi yao?

Swali lingine la jumla ni kwamba, mbunge ni mwakilishi wa wale tu waliompigia kura? au ni mwakilishi wa watu wote? Kama ni wa watu wote kuna sababu kwa walioshinda kuwa na viburi na kutoa kauli za kukatisha tamaa au hata kubeza kuzielekeza kwa wale wanaohisiwa hawakutoa ushirikiano? nadhani hili halieleweki vizuri kwa watu wengi.

Naomba tujadili hili maana nadhani inabidi watanzania tuelewe zaidi ya tujuavyo na JF kuna magwiji wa uchambuzi watatupiga darasa.

Nawakilisha.

Asanteni
 
Kwa kifupi wananchi wengi ni waelewa. Na especialy niwajuavyo wachaga ni watu makini sana linapokuja swala la muwakilishiwa wao. Nazani hoja kwamba wamempa kwa huruma haipo!! Mimi nazani ni utendaji wake tu. Kwa mfano hata sisi wa mikoa mingine tulishuhudia jinsi mh mrema alivyokuwa mchapakazi wakati akiwa waziri wa mambo ya ndani na naibu waziri mkuu...sasa kwa minajili hiyo naamini kwamba watu wa kilimanjaro bado wana imani nae
 
@ Mageuzi1992,
Asante kwa mchango wako.Nadhani umejibu kipengere cha track record ya enzi zileee... kwa sasa wengi walikuwa wanasema " tunampa kura akafie huko bungeni"...... meaning that wanajua kiafya atakuwa na limitation but still......
Ukiacha hilo, sidhani point yangu ni kuhusu umakini au kukosa umakini wa wachaga! Naomba urudie tena kusoma uone dimensions zote.Samahani na asante
 
Kwa kifupi wananchi wengi ni waelewa. Na especialy niwajuavyo wachaga ni watu makini sana linapokuja swala la muwakilishiwa wao. Nazani hoja kwamba wamempa kwa huruma haipo!! Mimi nazani ni utendaji wake tu. Kwa mfano hata sisi wa mikoa mingine tulishuhudia jinsi mh mrema alivyokuwa mchapakazi wakati akiwa waziri wa mambo ya ndani na naibu waziri mkuu...sasa kwa minajili hiyo naamini kwamba watu wa kilimanjaro bado wana imani nae

Kwa kuongezea, wanachi wa vunjo wamefikia mahali wakaona uwepo wa CCM ni sawa na kutokuwa na uongozi, wamejaribu kuangalia yale mazuri ambayo yalifamyika enzi za Mrema wakatumia kama kigezo cha maamuzi yao. Wengi tuliposikia kuchaguliwa kwake tulisema afadhali kwa maana ya bunge litachangamka kwa jinsi nyingine, otherwise pamoja na watu wa Vunjo kurudisha fadhila kwa mtu wao sidhani kama hawatarajii mambo mazuri toka kwake.
 
Hiyo kusema sijui asaidiwe,mara apate matibabu ni kashfa za kisiasa tu.Mrema bado anauwezo wa kuwahudumia wananchi kama bado nia ipo ya kweli.Na kilichoangaliwa hapo ni hasa uwezo wa kiutendaji aliowahi kuuonyesha huko nyuma,naamini wapiga kura wa vunjo walichuja mengi sana kabla ya kupiga kura.
 
WomanOfSubstance

Huyu Mrema wa sasa siyo wa 1995 alipoitetemesha CCM.

Kwa kweli Wana vunjo wamempa huyu mzee kwa huruma au fadhila kwa kile alichowafanyia huko miaka ya 1990s kama walivodai. Sasa hivi Mrema ni mzee na physicall and Mentally he is not ok. Nilimwona kwenye mdahalo uliokuwa unaendeshwa na TBC(Mchakato majimboni) alionekana yuko weak na hata anavyojieleza anatia huruma. Hata upinzani wake ni dhaifu maana sasa hivi ukimsikiliza kila kitu anaitetea CCM as if yuko CCM wakati yeye ni TLP. Kwa kweli Vunjo watakuwa wamemtengenezea Pensheni yake pengine na hayo matibabu. Kama ni mikikimikiki ya kisiasa Mrema is finished.

Kuhusu kama Mbunge ni mwakilishi wa wale waliomchagua tu au ni wa watu wote ni kwamba;Kuna tatizo la Watanzania wengi kutotilia maanani kuhusu haki yao kikatiba ya kupiga kura kwa maana ya kuchagua kiongozi wanayemtaka. Na hili linachangiwa na watu wengi kukosa elimu ya Uraia na hivo kutokujua umuhimu wa Kuchagua au kuchaguliwa. Hivo wengi wanaona wakipiga kura au wasipopiga kura yote ni sawa tu. After all wengi wanajua siku zote Chama Tawala CCM ndicho hushinda hata usipokichagua.

Hili swala lako la mwisho iwapo Mbunge anakuwa mwakilishi wa wote baada ya Uchaguzi hata kama hukumchagua ni kwamba;kwa vile yeye ndiye atakuwa mwakilishi wa jimbo husika automatically anawakilisha hata wale ambao hawakumchagua. Na chochote atakacho kitetea Bungeni whether ni kizuri au kibaya kitakuwa na effect kwa watu wa eneo husika,kama ni barabara,zahanati au shule wote watatumia. Kama tu ilivyo kwa Rais JK, kachaguliwa na watu milioni 5.2 among 45 million Tanzanians, yeye ni Rais wa wote 45m including hao ambao hawakumchagua. Kama akiboresha miundo mbinu,mashule,hospitals,vyuo ni kwa wote.

Tatizo linakuja pale kunapokuwa na hali ngumu za kimaisha kwa maana ya kiuchumi,kielimu,kiafya etc,utakuta wale ambao hawakupiga kura ndo wa kwanza kulalamika kuwa serikali mbovu wakti hawakushiriki kuchagua hiyo waliyofikiri itakuwa nzuri.

Naamini kwa kiasi nimegusa maeneo karibu yote.

Ubarikiwe.
 
wos
mrema ameshinda sio kwa ajili ya huruma bali kwa ajili ya mambo aliyoyafanya akiwa kiongozi
mrema bado alikuwa very popular kuliko wale wagombea wengine
 
WoS,

For the purpose of simplyfying ni hivi, Demokrasia na Siasa ni majambo ambayo watu tuna practise kila siku katika maisha yetu ya kawaida. Mfano marafiki watatu wanapoamua kwenda ku socialize bila ya kuafiki the final destination and are torn between two places chaguo la wawili ndio litakalo amua mwelekeo. Hapa ndipo demokrasia inapoanzia, kwa sababu as a group in most cases people want different things and the best way to reach a consesus is by voting.

Tukirudi kwenye ubunge kanuni ni zilezile za Demokrasia zinatumika, watu wote huwezi waridhisha kwa pamoja kwa kuwa mahitaji yanatofautiana na vipa umbele vinatofautiana. Hivyo kwenye uchaguzi tunatakiwa kuchagua kiongozi ambae tutaona ana muono karibu na ki matakwa yetu ndio atuwakilishe, na mgombea anaepata kura za wengi ndio mshindi (the theory behind it wanasema maisha sio kumridhisha kila mtu bali wengi based on resouces).

Hapo ndipo siasa za kitaifa zinapoanza na mambo ya policies, economics and so forth. Sasa kuchagua mmbunge kwa sympathetical emotions au sijui popularity ni upuuzi and it tells you the level of awareness as a nation or regional. Kwa sababu kinachofuata mbele ni technical na mmbunge lazima ajue some of those technicalities hili aweze jua wapi sawa na wapi si sawa. Tumejaza watu wa ajabu sana kwenye siasa zetu ndio maana wazungu wana interpret ya kwamba sisi bado tupo a century behind in terms of mental development as a whole (though you only need a few people to bring about radical changes).
 
Back
Top Bottom