Huu ni mwaka wangu wa mwisho kuajiriwa

Ila siku Mimi nitakapoamua kuachana na ajira sitotangaza kwa mtu yeyote Ni kimya kimya watu watashutukia tu sipo .

Sometime outside energy zinaleta gundu .



Sent from my TECNO P703 using JamiiForums mobile app
Ni kweli Mkuu, ukitaka kufanya jambo usiseme sababu wengi wao wanaiogopa hio hali unayoenda kupitia, Lazima wakukatishe tamaa, amka mwenyewe watakukuta mbele mbele huko.ukisubiri uambiwe na watu wengine shetani ataitumia hio nafasi kuharibu mipango yako.

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
 
Huyu atakuja tena kuomba ushauri namna ya kurudi kazini.

Tuendeleee na kazi,mwacheni.
Lakini uweke akiba ya maneno mkuu maana unaweza jikuta unakuja kuomba kazi kwake baada ya miaka kadhaa. Mfano miaka hiyo akina Kitenge walikuwa hawapigi nyimbo za Domo wakiwa ITV lakini sasa hivi Domo ndio kawaajiri na awaweka mjini kupitia WASAFI TV. Maisha yanadunda mkuu hata kama unakomaa kwenye ajira.
 
Kuwa makini mkuu ushauri wangu usiache kazi fanya kazi huku umejiajiri kwa maana maisha ya sasa ni magumu sana kuliko miaka ile ya 90 tuliokuwa tunasoma. Mfungulie mkeo kile kitu anachokipenda kutoka moyoni siyo wewe unachokipenda ila yeye kaa chini uongee naye atakachokuambia kwamba ni ndoto yake mfungulie ila wewe usiache kazi ila na wewe jiajiri weka mtu shamba pamoja na kukuangalia shamba na mifugo na huku mkeo umemfungulia kile akipendacho yeye na huku wewe unatumikisha angalau hata miaka mitatu mbeleni unaangalia shamba na mifugo vinakwendaje na mkeo naye anakwenda vizuri kama mambo yanakwenda vizuri sana ndiyo sasa unaomba kuacha kazi kwa kuwa shamba na biashara ya mkeo vyote vimekua yaani mwendo wa faida kwenda juu.
 
Kama ajira inakulipa vizuri bora ukomae hapo hapo.

Hizi mambo za kukimbilia kufuga kuku utajikuta umepoteza kila kitu hadi huyo mwanamke.

Niko sahii kurekebishwa
Ukiwa na fikra ya kupata faida mwanzo tu baada ya kuanza biashara au ufigaji....hii itakula kwako
Kila jambo linahitaji utulivu,subra,mikakati nk
Hakuna atakaekufa na njaa(ukiwa sehemu ya amani) ikiwa ni mpambanaji
 
Mdogo wangu kwanza nakupa hongera kwa kuwa na wazo la ujasiliamali. Hongera sana

Pamoja na yote uliyoyaongea mimi naomba nikupe ushauri na naomba uufanyie kazi kikamilifu kwa kuwa mie nina uzoefu wa yote mawili unayoyapitia na kutaka kuyafanya yaani kufanya kazi na kufanya ujasiliamali.

Naanza kuwa ujumbe ambao niliusoma humu jana na kuuandika katika DIARY yangu nanukuu "Imenichukua miaka 30 kufika hapa nilipo, japo vijana wanatamani yote haya ndani ya usiku mmoja" - Aliko Dangote. Mwisho wa kunukuu

Wewe hauna mtaji hata kidogo (kwa mujibu wa maelezo yako) ila kuna hela za mafao ya kujitoa unazitegemea. Hapo ni tatizo kubwa sana. Fao la kujitoa halitoki kirahisi kama unavyofikiri mdogo wangu. Kuna watu nawajua wanasotea hilo fao toka JPM alivyoingia madarakani mpk leo hii na hawajafanikiwa kulipata. Una mfano mmoja tu wa huyo mtu hujui alikuwa na connection gani mpaka akapata hizo hela. Unaweza kukaa hata miaka mitatu unazungushwa tu. Hata wastaafu ambao wana haki kisheria nao wamekuwa wanapata shida kupata mafao yao wengine miaka miwili au zaidi sembuse wewe.

Kwenye hilo nashauri usiache kazi mpaka uhakikishe umepata mtaji wa kutosha wa kuanza hizo biashara nje ya mafao ya kujitoa unayoyafikiria. Simple logic chukulia umeacha kazi na mafao yakachelewa kwa miaka miwili, utaweza ku-survive?

Biashara inataka mipango (planning) na mipango hiyo ni kuanzia kutafuta mtaji, jinsi ya kuiendesha, mauzo unayoyategemea, faida utakayopata, gharama za uendeshaji pamoja na life span ambayo uwekezaji wako utakulipa (Business Proposal).

Usiache hiyo nia yako ya kufanya ujasiliamali ila jipange vizuri kabla hujaingia huko maana ni kugumu kuliko wengi wanavyodhani.

Mimi ni mwajiriwa wa Serikali ingawa nina cheo na elimu kubwa sana pia ni mjasiliamali mkubwa wa ufugaji kuku wa nyama, samaki pamoja na kumiliki mashamba makubwa Morogoro na Mkuranga. Pamoja na ujasiliamali sijawahi kuwaza kuacha kazi hata siku moja.

Mtumie sana mkeo kwa sababu nadhani kwa maelezo yako hana shughuli ya kuingiza kipato. Mtumie kwenye biashara unayofikira kuifanya ili yeye aianze kwa udogo na kadri siku zinavyoenda itakuwa na utapata uzoefu kupitia yeye ili baadae ukishaona mbivu na mbichi unaweza kufanya maamuzi ya kuacha kazi au lah. Mtaji ambao unaufikiria ni mdogo sana kwa jinsi ulivyojieleza. Ufugaji unahitaji mtaji kama mabanda, mifugo yenyewe, malisho, vifaa vya kulishia na utafutaji masoko. Nashauri usiingie kichwa kichwa ukakwama baadae ila usiliache hilo wazo lifanyie kazi na chukua muda kuanzia chini upande mpaka juu.

Jiwekee mipango na usikurupuke nenda taratibu kwani mafanikia yanakuja kwa mipango na yanachukua muda sana kuiva. Ndio sababu iliyonifanya nianze na ujumbe wa Dangote pale juu. Najua kama kijana una kiu ya mafanikio ila mafanikuwa hayaji ndani ya usiku mmoja mafanikia ni process tena ndefu mno.

Kama una swali au unahitaji ufafanunuzi usisite kuuliza kwani nina uzoefu kwenye yale unayoyawaza.
Nina mengi ya kueleza ila muda ndio tatizo nina kazi nyingi ila nina uhakika nimesema mengi ya msingi
Shukran sana kwa ushauri wako
 
Anza kufuga huku upo kwenye ajira usidhan biashara itakupa faida haraka haraka anza taratibu mpaka biashara ikomae
Biashara hazielewekagi
Ushauri mzuri sana mkuu huo! Asiache kazi kabla hajasimama! Ingawa changamoto ninavyoona kwa huyo mdau ni mtaji maana anataka mafao ndiyo ayatumie kama mtaji!
 
Tatu,nikishachukua hicho kiasi namfungulia wife mradi wa 2m nyumbani then mimi nasepa zangu porini ambapo nitafanya yafuatayo

. Kufuga nguruwe na kuku
. Kulima nyanya za kumwagilia

Hayo hapo juu nitayafanya kwa 4m na kiasi kilichobaki ambayo itakuwa ni 4m nitaiweka akiba then nitakitumia kununulia mazao kama mahindi nk kipindi cha mavuno.
Kufuga nguruwe ✔
Kufuga kuku✔
Kulima nyanya za kumwagilia❌🚫
Kununua mazao na kuyauza ✔

Tafadhari usiweke life savings yako kwenye kilimo cha mazao yanayo oza kama nyanya.
Nyanya kichaa kalime hizo kwa kujifurahisha ukiwa umetoboa maisha kwenye ufugaji au biashara zingine.

Kama una mtaji mzuri na unamapenzi sana na nyanya kanunue mashine na vifungashio usindike na kuuza nyanya ulizo ongeza mnyororo wa thamani ambazo zinakaa kwenye shelves miaka au miezi kibao bila kuoza.
 
Mku sikushauri hata kidogo .Tafuta likizo tumia hizo pesa kuanzisha mradi ukiwa kazin, Tafuta kijana mwaminifu hapo unatumia mshahara kuendeshea mradi mradi ukiweza kusimama ndio uache kazi.
 
bro hao PSSSF huwa wanazingua kutoa helaaaaa!
UWE NA UHAKIKA KABLA YA KUTEMA KAZI
 
Haya maisha wakati mwingine inabidi ujilipue tu. Wenye Kiingereza chao wanasema (risk taking). Vinginevyo ukiwa mwoga utabaki umedumaa
 
Back
Top Bottom