Huu ni mwaka wangu wa mwisho kuajiriwa

Umewahi kufuga kwa uchache nkimaanisha unaexperience hiyo? pia kuku unauzoefu nao mkuu?.....

Kama hauna experience ni vyema ukavifanya hata kwakuwa na nguruwe 2 na kuku hata 10 na nyanya uzilime kama kibustani kwako ili ujue changamoto ili ukiingia uweze kuifanya project yako kwa viwango vzuri na ufanikiwe maana kuacha kazi na kuingia kujiajiri inamaanisha unauhakika hautaflot account yako mkuu.....

Idea ya nguruwe na kuku ninayo pia....

Ninachijua kinyesi cha kuku unaweza kigeuza kuwa chakupa cha nguruwe,

Ni vzuri kulima mahindi ili badae uyabaraze yawe chakula cha kuku yanaounguza sana cost.

Ujifunze na uwe vizuri katika upandaji fodder za ngano, mahindi etc ili kuokoa kiasi cha fedha za chakula

Tumia sana mbegu bora za kizungu kama large white, durocs hizo ndizo zinazaa watoto 11 -12 etc na zina nyama nyingi.....

Kuku changanya kuroiler na kienyeji ili upate kuku wakubwa wemye uwezo wa kutaga na kuhatamia pia wanaouzika kwa urahisi sokoni....

Jitajidi usolve suala la maji mapema

Kuna majani ya mihogo, majani yanayoota juu ya maji, migomba ya ndizi hivyo vyote vikichemshwa ni vyakula vya nguruwe.... Unaweza panda mugomba mingi ikakusaidia kuokoa cost pia.....

Ukue utaratibu wa nguruwe kula ni mara 2 asubuh na jioni na nini wanakula mchana (wanapaswa wanywe maji kwa wingi sana)

Kuna aina ya mabanda yanayosaidia sana ukuaji wa nguruwe na kuku...

Pia fahamu hata kutengeneza mashine ya kutotoresha ya mayai 50( home made incubators itakupa faida kubwa sana katika ufugaji wako

Pia ujue kurecycle vifaa mbalimbali kwenye shamba lako kama utaweza geuza matairi kuwa kama vyombo vya kunyweshea maji kama utaweza tengeneza sprinter ya kumwagilia kwa kutumia mpira wa maji ya vyupa vya soda itakuwa vizuri...

Jitahidi sana kuwa creatibe kwakila kitu na kakila kifaa ili uokoe fedha na upate faida na bidhaa bora zaidi
 
Habari wakuu,

Baada ya kufanya kazi za kuajiriwa kwa muda sasa bila ya kuyafikia maisha ya ndoto zangu, pia baada ya kuishi maisha nisiyopendezwa nayo (kukosa uhuru wa kipato) nimekaa na kutafakari kwa kina juu ya hatma ya maisha yangu na kufikia maamuzi yafuatayo.

Mosi, kuna 4.3m PPF, hiki ni kiasi ambacho nilishindwa kukitoa enzi za mwendazake baada ya kupoteza ajira. Sasa niko kwenye kampuni nyingine ambapo michango yangu mpaka sasa ni 5m,so nataka nizihamishie huku na mpaka March mwakani unapoisha mkataba wangu nitakuwa na si chini ya 10m.

Pili,kabla ya December mwaka huu nitaenda Morogoro kufanya ziara maana kuna mshikaji wangu yupo kule naye alikuwa mwajiriwa somewhere akaamua kuacha kazi na kujikita katika kilimo na ufugaji (yuko njema sana), huyu jamaa yangu atakuwa msaada sana kwangu katika kutimiza matarajio yangu.

Tatu,nikishachukua hicho kiasi namfungulia wife mradi wa 2m nyumbani then mimi nasepa zangu porini ambapo nitafanya yafuatayo

. Kufuga nguruwe na kuku
. Kulima nyanya za kumwagilia

Hayo hapo juu nitayafanya kwa 4m na kiasi kilichobaki ambayo itakuwa ni 4m nitaiweka akiba then nitakitumia kununulia mazao kama mahindi nk kipindi cha mavuno.

Karibuni wakuu kwa ushauri zaidi.
Mkuu mii nilifanya hayo maamuzi ya kijasiri miaka 30 iliyopita nikiwa bado kijana.
Sikurudi nyuma na sijutii kuacha kazi serikalini.
Mi ilikuwa tofauti katika mtazamo wangu.
Sikuwa na hata senti tano nilipoacha kufanya kazi, lakii nilijiwekea malengo kuwa nikitengeneza fedha sawasawa na mshahara wangu kwa mwezi, basi nimevuka malengo.
Nilitengeneza zaidi ya mara kumi ya mshahara wangu na ikanipa motisha wa kutisha na kiwewe!
Sikutazama nyuma aslilani, na wenzangu niliowaacha kazinisasa hivi naweza kuwaajiri.
 
Mkuu mii nilifanya hayo maamuzi ya kijasiri miaka 30 iliyopita ninikwa bado kijana.
Sikurudi nyuma na sijutii kuacha kazi serikalini.
Mi ilikuwa tofauti katika mtazamo wangu.
Sikuwa na hata senti tano nilipoacha kufanya kazi, lakii nilijiwekea malengo kuwa nikitengeneza fedha sawasawa na mshahra wangu kwa mwezi, basi nimevuka malengo.
Nilitengeneza zaidi ya mara kumi ya mshahara wangu na ikanpa motisha wa kutusha na kiwewe!
Sikutazama nyuma aslilani, na wenzangu niliowaacha kazinisasa hivi naweza kuwaajiri.
Hongera sana mkuu,nipo mbioni na mimi.
Baada ya kupitia mawazo ya watu nimeona nisiache kazi kwanza bali niwatoe watoto kwenye shule za kulipia ili nipate capital ya kuanzisha mradi hapa nyumbani huku nikijipanga kuacha kazi.
 
Well said,
Mradi nitakaouanzisha nyumbani ni kwaajili ya wife kuusimamia so hatokuwa tena hana shughuli ya kufanya mkuu.
kuhusu elimu niko na degree ya elimu,nimeipata chuo kikuu huria na kuhusu kazi yangu sio mbaya sana kwani take home yangu 700,000/
Plan ya aina ya maisha niyatakayo ninayo na ndiyo imekuwa ikinisumbua sana namna na ya kuifikia...na hii imetokanana na ukweli kwamba sikutaka wanangu wasome shule za kawaida na huko ndiko pesa zangu nyingi zinakokwenda mkuu.

Kwakuwa nimeamua kuwatoa ni matumaini yangu taratiibu nitaianza safari kuelekea uhuru wa kipato.

Mkuu nakushukuru sana kwa in put yako.
Asante sana Mungu akubariki sana
 
Umewahi kufuga kwa uchache nkimaanisha unaexperience hiyo? pia kuku unauzoefu nao mkuu?.....

Kama hauna experience ni vyema ukavifanya hata kwakuwa na nguruwe 2 na kuku hata 10 na nyanya uzilime kama kibustani kwako ili ujue changamoto ili ukiingia uweze kuifanya project yako kwa viwango vzuri na ufanikiwe maana kuacha kazi na kuingia kujiajiri inamaanisha unauhakika hautaflot account yako mkuu.....

Idea ya nguruwe na kuku ninayo pia....

Ninachijua kinyesi cha kuku unaweza kigeuza kuwa chakupa cha nguruwe,

Ni vzuri kulima mahindi ili badae uyabaraze yawe chakula cha kuku yanaounguza sana cost.

Ujifunze na uwe vizuri katika upandaji fodder za ngano, mahindi etc ili kuokoa kiasi cha fedha za chakula

Tumia sana mbegu bora za kizungu kama large white, durocs hizo ndizo zinazaa watoto 11 -12 etc na zina nyama nyingi.....

Kuku changanya kuroiler na kienyeji ili upate kuku wakubwa wemye uwezo wa kutaga na kuhatamia pia wanaouzika kwa urahisi sokoni....

Jitajidi usolve suala la maji mapema

Kuna majani ya mihogo, majani yanayoota juu ya maji, migomba ya ndizi hivyo vyote vikichemshwa ni vyakula vya nguruwe.... Unaweza panda mugomba mingi ikakusaidia kuokoa cost pia.....

Ukue utaratibu wa nguruwe kula ni mara 2 asubuh na jioni na nini wanakula mchana (wanapaswa wanywe maji kwa wingi sana)

Kuna aina ya mabanda yanayosaidia sana ukuaji wa nguruwe na kuku...

Pia fahamu hata kutengeneza mashine ya kutotoresha ya mayai 50( home made incubators itakupa faida kubwa sana katika ufugaji wako

Pia ujue kurecycle vifaa mbalimbali kwenye shamba lako kama utaweza geuza matairi kuwa kama vyombo vya kunyweshea maji kama utaweza tengeneza sprinter ya kumwagilia kwa kutumia mpira wa maji ya vyupa vya soda itakuwa vizuri...

Jitahidi sana kuwa creatibe kwakila kitu na kakila kifaa ili uokoe fedha na upate faida na bidhaa bora zaidi
Nashukuru sana kwa mchango wako mkuu.
 
Kuajiriwa sio kubaya na kujiajiri pia ni jambo jema sana.Hakuna mjanja wala mjinga kuliko mwenzake endapo utaamua kuwa katika mojawapo ya makundi haya mawili.
Soon na mimi namaliza mkata wangu na nategemea kuingia katika kuifukuzia ndoto ya maisha yangu ambayo ndani yake naamin nitapata uhuru wa kipato na self fullfilment pia.
 
Kuajiriwa sio kubaya na kujiajiri pia ni jambo jema sana.Hakuna mjanja wala mjinga kuliko mwenzake endapo utaamua kuwa katika mojawapo ya makundi haya mawili.
Soon na mimi namaliza mkata wangu na nategemea kuingia katika kuifukuzia ndoto ya maisha yangu ambayo ndani yake naamin nitapata uhuru wa kipato na self fullfilment pia.
Kila la kheri sana mkuu
 
1.Biashara inahitaji mda wa kukua
2.kilimo cha nyanya hakitaki uzembe na kinahitaji mtaji mkubwa.

Nyanya inaweza kukutoa lkn laZima ukubAli kuwa na roho ngumu utashinda shamba sana unaogesha mimea na dawa kwa sana,utatumia pesa sana kwahiyo ni bora hizo nyanya walau utoe kwenye msimu wa hela mweZi wa 1,2,3

Zao lenye bei za uhakika ukiweka store ni maharage

Ufugaji wa kuku usitarajie makubwa hasa mwanzoni

Ushauri wangu
1.Km utagusa eka ya nyanya uwe na million 1.5-3 mfukoni kulingana na eneo ulilopo chini ya hapo utakuwa unaletea utani nyanya itakupiga za uso mpk ushangae.Shambani weka mweZi wa 10-11.5.

2.Zao la kuweka store iwe maharage bei isizidi 22000 debe(usafiri+gunia+gharama za kununua).Kama mahindi debe liwe 3000-4500 kwa gharama zote

3.Kuku

Pata eneo kubwa la kuwaachia huru wanakula asubuh then wanaenda zao

4.Panda pilipili kali na nyanya nyungu miche 2000 kwa kila zao

Wewe unahitaji hela za mara kwa mara za kuendeshea hago mazAo mawili hayana gharama kubwa hlf yaweza kukupa hela za mara kwa mara za kufanyia mradi mkubwa.

Tenga kibustani mchwara cha kukupa 5000 kwa siku

Note:Sio lelemama unachotaka kufanya,kilimo cha nyanya hakipatani na mtaji mdg,mazao ya kukupa hela za mara kwa mara ni LAZIMA na sio Muhimu tu.
 
Hiyo ni risk kubwa sana. Kwani huwezi kuchukua mkopo?
Kampuni ninayofanyia kazi haijatuwekea mazingira mazuri ya kukopa mkuu,ila pamoja na hayo nimepata suluhisho ambalo ni kuwapeleka watoto shule za kawaida ili niweze kupata mtaji.
 
1.Biashara inahitaji mda wa kukua
2.kilimo cha nyanya hakitaki uzembe na kinahitaji mtaji mkubwa.

Nyanya inaweza kukutoa lkn laZima ukubAli kuwa na roho ngumu utashinda shamba sana unaogesha mimea na dawa kwa sana,utatumia pesa sana kwahiyo ni bora hizo nyanya walau utoe kwenye msimu wa hela mweZi wa 1,2,3

Zao lenye bei za uhakika ukiweka store ni maharage

Ufugaji wa kuku usitarajie makubwa hasa mwanzoni

Ushauri wangu
1.Km utagusa eka ya nyanya uwe na million 1.5-3 mfukoni kulingana na eneo ulilopo chini ya hapo utakuwa unaletea utani nyanya itakupiga za uso mpk ushangae.Shambani weka mweZi wa 10-11.5.

2.Zao la kuweka store iwe maharage bei isizidi 22000 debe(usafiri+gunia+gharama za kununua).Kama mahindi debe liwe 3000-4500 kwa gharama zote

3.Kuku

Pata eneo kubwa la kuwaachia huru wanakula asubuh then wanaenda zao

4.Panda pilipili kali na nyanya nyungu miche 2000 kwa kila zao

Wewe unahitaji hela za mara kwa mara za kuendeshea hago mazAo mawili hayana gharama kubwa hlf yaweza kukupa hela za mara kwa mara za kufanyia mradi mkubwa.

Tenga kibustani mchwara cha kukupa 5000 kwa siku

Note:Sio lelemama unachotaka kufanya,kilimo cha nyanya hakipatani na mtaji mdg,mazao ya kukupa hela za mara kwa mara ni LAZIMA na sio Muhimu tu.
Mkuu nakushukuru sana kwa ushauri wako...nitaufanyia kazi mkuu.
 
Kwanini usingeanza
Habari wakuu,

Baada ya kufanya kazi za kuajiriwa kwa muda sasa bila ya kuyafikia maisha ya ndoto zangu, pia baada ya kuishi maisha nisiyopendezwa nayo (kukosa uhuru wa kipato) nimekaa na kutafakari kwa kina juu ya hatma ya maisha yangu na kufikia maamuzi yafuatayo.

Mosi, kuna 4.3m PPF, hiki ni kiasi ambacho nilishindwa kukitoa enzi za mwendazake baada ya kupoteza ajira. Sasa niko kwenye kampuni nyingine ambapo michango yangu mpaka sasa ni 5m,so nataka nizihamishie huku na mpaka March mwakani unapoisha mkataba wangu nitakuwa na si chini ya 10m.

Pili,kabla ya December mwaka huu nitaenda Morogoro kufanya ziara maana kuna mshikaji wangu yupo kule naye alikuwa mwajiriwa somewhere akaamua kuacha kazi na kujikita katika kilimo na ufugaji (yuko njema sana), huyu jamaa yangu atakuwa msaada sana kwangu katika kutimiza matarajio yangu.

Tatu,nikishachukua hicho kiasi namfungulia wife mradi wa 2m nyumbani then mimi nasepa zangu porini ambapo nitafanya yafuatayo

. Kufuga nguruwe na kuku
. Kulima nyanya za kumwagilia

Hayo hapo juu nitayafanya kwa 4m na kiasi kilichobaki ambayo itakuwa ni 4m nitaiweka akiba then nitakitumia kununulia mazao kama mahindi nk kipindi cha mavuno.

Karibuni wakuu kwa ushauri zaidi.
Kwanini usianze kwaa kulima muda huu wakati bado unafanyakazi.Anza kwa awamu mdogo mdogo upate uzoefu
 
Mdogo wangu kwanza nakupa hongera kwa kuwa na wazo la ujasiliamali. Hongera sana

Pamoja na yote uliyoyaongea mimi naomba nikupe ushauri na naomba uufanyie kazi kikamilifu kwa kuwa mie nina uzoefu wa yote mawili unayoyapitia na kutaka kuyafanya yaani kufanya kazi na kufanya ujasiliamali.

Naanza kuwa ujumbe ambao niliusoma humu jana na kuuandika katika DIARY yangu nanukuu "Imenichukua miaka 30 kufika hapa nilipo, japo vijana wanatamani yote haya ndani ya usiku mmoja" - Aliko Dangote. Mwisho wa kunukuu

Wewe hauna mtaji hata kidogo (kwa mujibu wa maelezo yako) ila kuna hela za mafao ya kujitoa unazitegemea. Hapo ni tatizo kubwa sana. Fao la kujitoa halitoki kirahisi kama unavyofikiri mdogo wangu. Kuna watu nawajua wanasotea hilo fao toka JPM alivyoingia madarakani mpk leo hii na hawajafanikiwa kulipata. Una mfano mmoja tu wa huyo mtu hujui alikuwa na connection gani mpaka akapata hizo hela. Unaweza kukaa hata miaka mitatu unazungushwa tu. Hata wastaafu ambao wana haki kisheria nao wamekuwa wanapata shida kupata mafao yao wengine miaka miwili au zaidi sembuse wewe.

Kwenye hilo nashauri usiache kazi mpaka uhakikishe umepata mtaji wa kutosha wa kuanza hizo biashara nje ya mafao ya kujitoa unayoyafikiria. Simple logic chukulia umeacha kazi na mafao yakachelewa kwa miaka miwili, utaweza ku-survive?

Biashara inataka mipango (planning) na mipango hiyo ni kuanzia kutafuta mtaji, jinsi ya kuiendesha, mauzo unayoyategemea, faida utakayopata, gharama za uendeshaji pamoja na life span ambayo uwekezaji wako utakulipa (Business Proposal).

Usiache hiyo nia yako ya kufanya ujasiliamali ila jipange vizuri kabla hujaingia huko maana ni kugumu kuliko wengi wanavyodhani.

Mimi ni mwajiriwa wa Serikali ingawa nina cheo na elimu kubwa sana pia ni mjasiliamali mkubwa wa ufugaji kuku wa nyama, samaki pamoja na kumiliki mashamba makubwa Morogoro na Mkuranga. Pamoja na ujasiliamali sijawahi kuwaza kuacha kazi hata siku moja.

Mtumie sana mkeo kwa sababu nadhani kwa maelezo yako hana shughuli ya kuingiza kipato. Mtumie kwenye biashara unayofikira kuifanya ili yeye aianze kwa udogo na kadri siku zinavyoenda itakuwa na utapata uzoefu kupitia yeye ili baadae ukishaona mbivu na mbichi unaweza kufanya maamuzi ya kuacha kazi au lah. Mtaji ambao unaufikiria ni mdogo sana kwa jinsi ulivyojieleza. Ufugaji unahitaji mtaji kama mabanda, mifugo yenyewe, malisho, vifaa vya kulishia na utafutaji masoko. Nashauri usiingie kichwa kichwa ukakwama baadae ila usiliache hilo wazo lifanyie kazi na chukua muda kuanzia chini upande mpaka juu.

Jiwekee mipango na usikurupuke nenda taratibu kwani mafanikia yanakuja kwa mipango na yanachukua muda sana kuiva. Ndio sababu iliyonifanya nianze na ujumbe wa Dangote pale juu. Najua kama kijana una kiu ya mafanikio ila mafanikuwa hayaji ndani ya usiku mmoja mafanikia ni process tena ndefu mno.

Kama una swali au unahitaji ufafanunuzi usisite kuuliza kwani nina uzoefu kwenye yale unayoyawaza.
Nina mengi ya kueleza ila muda ndio tatizo nina kazi nyingi ila nina uhakika nimesema mengi ya msingi
Japo haukuwa ushauri wangu ila nimepata kitu kikubwa sana. Thanks brother Mungu akubariki.
 
45 Reactions
Reply
Back
Top Bottom