Huu ni mwaka wangu wa mwisho kuajiriwa

Habari wakuu,

Baada ya kufanya kazi za kuajiriwa kwa muda sasa bila ya kuyafikia maisha ya ndoto zangu, pia baada ya kuishi maisha nisiyopendezwa nayo (kukosa uhuru wa kipato) nimekaa na kutafakari kwa kina juu ya hatma ya maisha yangu na kufikia maamuzi yafuatayo.

Mosi, kuna 4.3m PPF, hiki ni kiasi ambacho nilishindwa kukitoa enzi za mwendazake baada ya kupoteza ajira. Sasa niko kwenye kampuni nyingine ambapo michango yangu mpaka sasa ni 5m,so nataka nizihamishie huku na mpaka March mwakani unapoisha mkataba wangu nitakuwa na si chini ya 10m.

Pili,kabla ya December mwaka huu nitaenda Morogoro kufanya ziara maana kuna mshikaji wangu yupo kule naye alikuwa mwajiriwa somewhere akaamua kuacha kazi na kujikita katika kilimo na ufugaji (yuko njema sana), huyu jamaa yangu atakuwa msaada sana kwangu katika kutimiza matarajio yangu.

Tatu,nikishachukua hicho kiasi namfungulia wife mradi wa 2m nyumbani then mimi nasepa zangu porini ambapo nitafanya yafuatayo

. Kufuga nguruwe na kuku
. Kulima nyanya za kumwagilia

Hayo hapo juu nitayafanya kwa 4m na kiasi kilichobaki ambayo itakuwa ni 4m nitaiweka akiba then nitakitumia kununulia mazao kama mahindi nk kipindi cha mavuno.

Karibuni wakuu kwa ushauri zaidi.
Mkuu!Kitu rahisi kukimudu ni wewe utafute kijiji chenye uhitaji wa mashine ya kukoboa na kusaga mahindi.Nunua eneo ambalo umeme njia tatu umefika na uweke mashine.Mzee kila mwezi utaendelea kupata mshahara kwa mashine yako.Ukiweza saga mwenyewe,hakika hutajuta.
 
Acha kazi baada ya kuanzisha mradi na kuona unafanya vizuri. Sio uache kazi na kuanzisha mradi.
Wazo lako ni zuri,changamoto iliyopo ni kupata huo mtaji wa kuweza kuwekeza ndio maana nimeona njia sahihi ni kuacha kazi ili nichukue mafao yangu.
 
Nyanya, ninyanyue, nyanya ni nyanyase, kideri plus homa ya nguruwe, mahindi kushuka bei, jipange jibaba, though u had a guts
 
fanya hivi chukua milioni mbili au nne njo mafia kodi boti ndogo au jahazi jahazi unaweza nunua jahazi itakuwa inasafirisha mizigo au ukikodi boti na nyavu itakusaidia kuvua samak huku kukodi sawa na laki nane miezi minne au sita hio pesa unaweza irudisha kwa siku tatu au mbili uvuvi ukikubali
Mmmmmh!Huu mchongo nimeutamani.Vp kama mimi nitaamua kujafanya hii kitu lakini nikiwa mbali,naweza toboa?.
 
Plan b ipo,nimeandika kuwa nitamfungulia wife biashara pale nyumbani maana kuna nafasi ya kufanya hivyo..
Wakati uno porini huko unamenyeka na jembe na kufuga nguruwe, biashara uliyomfungulia mkeo nyumbani haitakuwa salama.....

Mkeo watamla, pesa atahonga, na biashara itakufa arif, we kama vp beba huyo mkeo mwende wote huko chaka hiyo m2 uliyotaka kuichoma ikaongeze mtaji huko uendako

Sioni sababu ya kumuacha mkeo nyumbani apigwe mashine na wahuni wkt ww ukiwa huko vichakani ukitafuta pesa,.....

Mwanamke sio wa kuacha mbali arif, hata shetani alimdanganya hawa wakati Adam akiwa hayupo, take care
 
Mdogo wangu kwanza nakupa hongera kwa kuwa na wazo la ujasiliamali. Hongera sana

Pamoja na yote uliyoyaongea mimi naomba nikupe ushauri na naomba uufanyie kazi kikamilifu kwa kuwa mie nina uzoefu wa yote mawili unayoyapitia na kutaka kuyafanya yaani kufanya kazi na kufanya ujasiliamali.

Naanza kuwa ujumbe ambao niliusoma humu jana na kuuandika katika DIARY yangu nanukuu "Imenichukua miaka 30 kufika hapa nilipo, japo vijana wanatamani yote haya ndani ya usiku mmoja" - Aliko Dangote. Mwisho wa kunukuu

Wewe hauna mtaji hata kidogo (kwa mujibu wa maelezo yako) ila kuna hela za mafao ya kujitoa unazitegemea. Hapo ni tatizo kubwa sana. Fao la kujitoa halitoki kirahisi kama unavyofikiri mdogo wangu. Kuna watu nawajua wanasotea hilo fao toka JPM alivyoingia madarakani mpk leo hii na hawajafanikiwa kulipata. Una mfano mmoja tu wa huyo mtu hujui alikuwa na connection gani mpaka akapata hizo hela. Unaweza kukaa hata miaka mitatu unazungushwa tu. Hata wastaafu ambao wana haki kisheria nao wamekuwa wanapata shida kupata mafao yao wengine miaka miwili au zaidi sembuse wewe.

Kwenye hilo nashauri usiache kazi mpaka uhakikishe umepata mtaji wa kutosha wa kuanza hizo biashara nje ya mafao ya kujitoa unayoyafikiria. Simple logic chukulia umeacha kazi na mafao yakachelewa kwa miaka miwili, utaweza ku-survive?

Biashara inataka mipango (planning) na mipango hiyo ni kuanzia kutafuta mtaji, jinsi ya kuiendesha, mauzo unayoyategemea, faida utakayopata, gharama za uendeshaji pamoja na life span ambayo uwekezaji wako utakulipa (Business Proposal).

Usiache hiyo nia yako ya kufanya ujasiliamali ila jipange vizuri kabla hujaingia huko maana ni kugumu kuliko wengi wanavyodhani.

Mimi ni mwajiriwa wa Serikali ingawa nina cheo na elimu kubwa sana pia ni mjasiliamali mkubwa wa ufugaji kuku wa nyama, samaki pamoja na kumiliki mashamba makubwa Morogoro na Mkuranga. Pamoja na ujasiliamali sijawahi kuwaza kuacha kazi hata siku moja.

Mtumie sana mkeo kwa sababu nadhani kwa maelezo yako hana shughuli ya kuingiza kipato. Mtumie kwenye biashara unayofikira kuifanya ili yeye aianze kwa udogo na kadri siku zinavyoenda itakuwa na utapata uzoefu kupitia yeye ili baadae ukishaona mbivu na mbichi unaweza kufanya maamuzi ya kuacha kazi au lah. Mtaji ambao unaufikiria ni mdogo sana kwa jinsi ulivyojieleza. Ufugaji unahitaji mtaji kama mabanda, mifugo yenyewe, malisho, vifaa vya kulishia na utafutaji masoko. Nashauri usiingie kichwa kichwa ukakwama baadae ila usiliache hilo wazo lifanyie kazi na chukua muda kuanzia chini upande mpaka juu.

Jiwekee mipango na usikurupuke nenda taratibu kwani mafanikia yanakuja kwa mipango na yanachukua muda sana kuiva. Ndio sababu iliyonifanya nianze na ujumbe wa Dangote pale juu. Najua kama kijana una kiu ya mafanikio ila mafanikuwa hayaji ndani ya usiku mmoja mafanikia ni process tena ndefu mno.

Kama una swali au unahitaji ufafanunuzi usisite kuuliza kwani nina uzoefu kwenye yale unayoyawaza.
Nina mengi ya kueleza ila muda ndio tatizo nina kazi nyingi ila nina uhakika nimesema mengi ya msingi
Mkuu nikushukuru kwa dhati kabisa kwa huu ushauri.
Mkuu nami naamini kabisa kuwa maendeleo huchukua muda,sio swala la mda mfupi na nilitamni nianzishe mradi nikiwa bado niko kazini ila changamoto ni kwamba mshahara unaishia kwenye ada,chakula na nauli tena muda mwingine nakopa so mwisho wa mwezi ukifika unakuta pesa yote inapukutika.

Kampuni ninayofanya inatoa mikataba ya mwaka mmoja mmoja kiasi kwamba tunakosa sifa ya kukopesheka katika taasisi za kifedha,ingekuwa inatupa japo hata miaka 4 tungekopesheka na ningeutumia huo mkopo kuanzisha uwekezaji.

Sasa kutokana na ushauri wako pamoja na wadau wengine ambao wamenitahadharisha kuwa huenda mafao yasitoke mapema kama ambavyo nafikiria na muda huo nitakuwa sina kazi itasababisha niishi katika mazingira magumu zaidi...

Siwezi kupuuza ushauri hata kidogo ndio maana nimelileta hapa ili niweze kupata msaada katika kufikia malengo yangu...
kwa kuzingatia hayo yote nimeona nifanye maamuzi mengine ili niweze kupata mtaji wa kuandaa mazingira ya uwekezaji..

Mwakani watoto wangu wawili niwahamishe shule za kulipia niwapeleke za kawaida,halafu huyu mmoja aliyeko la sita nimwache amalize la 7 maana yeye kwa sasa haiwezekani na sekondari atasoma za kawaida, then kile kiasi nilichokuwa nakilipa kama ada ndio nikitumie kuwekeza hapa nyumbani.
 
mimi binafsi sikushauri kuhusu kuku,nafuga kuku ndo maana nakupa ushauri.

Ili uweze kupata faida hiyo unayotaka itakubidi ufuge kuku kuanzia 500 na kuendelea iwe ni wa kisasa,chotara au kienyeji hivyo chakula kimepanda bei hakuna mfano kuku wengi hivyo huwez sema wakajitafutie chakula(kienyeji na chotara)wakashiba lazima uchanganye uwape na mara nyingi wakiwa vifaranga uwape cha dukani ili wapate mwili haraka ndo unaanza kuchanganyA.

Labda nguruwe na kilimo ila kwa sasa kuku ni uwe na pesa ya maana na si yamawazo kwenye kuwalisha.
 
Kuwa makini mkuu ushauri wangu usiache kazi fanya kazi huku umejiajiri kwa maana maisha ya sasa ni magumu sana kuliko miaka ile ya 90 tuliokuwa tunasoma. Mfungulie mkeo kile kitu anachokipenda kutoka moyoni siyo wewe unachokipenda ila yeye kaa chini uongee naye atakachokuambia kwamba ni ndoto yake mfungulie ila wewe usiache kazi ila na wewe jiajiri weka mtu shamba pamoja na kukuangalia shamba na mifugo na huku mkeo umemfungulia kile akipendacho yeye na huku wewe unatumikisha angalau hata miaka mitatu mbeleni unaangalia shamba na mifugo vinakwendaje na mkeo naye anakwenda vizuri kama mambo yanakwenda vizuri sana ndiyo sasa unaomba kuacha kazi kwa kuwa shamba na biashara ya mkeo vyote vimekua yaani mwendo wa faida kwenda juu.
Nashukuru kwa ushauri mkuu,nitaufanyia kazi
 
Habari wakuu,

Baada ya kufanya kazi za kuajiriwa kwa muda sasa bila ya kuyafikia maisha ya ndoto zangu, pia baada ya kuishi maisha nisiyopendezwa nayo (kukosa uhuru wa kipato) nimekaa na kutafakari kwa kina juu ya hatma ya maisha yangu na kufikia maamuzi yafuatayo.

Mosi, kuna 4.3m PPF, hiki ni kiasi ambacho nilishindwa kukitoa enzi za mwendazake baada ya kupoteza ajira. Sasa niko kwenye kampuni nyingine ambapo michango yangu mpaka sasa ni 5m,so nataka nizihamishie huku na mpaka March mwakani unapoisha mkataba wangu nitakuwa na si chini ya 10m.

Pili,kabla ya December mwaka huu nitaenda Morogoro kufanya ziara maana kuna mshikaji wangu yupo kule naye alikuwa mwajiriwa somewhere akaamua kuacha kazi na kujikita katika kilimo na ufugaji (yuko njema sana), huyu jamaa yangu atakuwa msaada sana kwangu katika kutimiza matarajio yangu.

Tatu,nikishachukua hicho kiasi namfungulia wife mradi wa 2m nyumbani then mimi nasepa zangu porini ambapo nitafanya yafuatayo

. Kufuga nguruwe na kuku
. Kulima nyanya za kumwagilia

Hayo hapo juu nitayafanya kwa 4m na kiasi kilichobaki ambayo itakuwa ni 4m nitaiweka akiba then nitakitumia kununulia mazao kama mahindi nk kipindi cha mavuno.

Karibuni wakuu kwa ushauri zaidi.
Kuna mzee mmoja ofisini hua ananiambia haya na kunisistiza kutokupoteza muda kazini na kuanza kuwekeza kwenye kilimo na biashara
 
Ushauri mzuri sana mkuu huo! Asiache kazi kabla hajasimama! Ingawa changamoto ninavyoona kwa huyo mdau ni mtaji maana anataka mafao ndiyo ayatumie kama mtaji!
Nawatoa watoto shule za kulipia ili nipate kukitumia kile kiasi cha ada kuanzisha miradi.
 
Ni muhimu kusoma upepo na namna hali halisi ilivyo
Kuwa makini sana kayika kutanya maamuzi yako hasa kama haya ambayo ndio muhimili na mustakabali mzima wa maisha yako ya kiuchumi

Katika ujasiliamali kwa asilimia kubwa ya waliofanikiwa ni wale wenye walau miaka mitano na kuendelea katika sekta hiyo kama uko tayari kusota miaka zaidi ya sita na katika hali tofautitofauti sawa

Lakini kujiajiri kuna raha yake ila unatakiwa kuwa na akili ua matumizi ya pesa aisee
 
Ni muhimu kusoma upepo na namna hali halisi ilivyo
Kuwa makini sana kayika kutanya maamuzi yako hasa kama haya ambayo ndio muhimili na mustakabali mzima wa maisha yako ya kiuchumi

Katika ujasiliamali kwa asilimia kubwa ya waliofanikiwa ni wale wenye walau miaka mitano na kuendelea katika sekta hiyo kama uko tayari kusota miaka zaidi ya sita na katika hali tofautitofauti sawa

Lakini kujiajiri kuna raha yake ila unatakiwa kuwa na akili ua matumizi ya pesa aise.
Nimekusoma mkuu.
 
Mkuu nikushukuru kwa dhati kabisa kwa huu ushauri.
Mkuu nami naamini kabisa kuwa maendeleo huchukua muda,sio swala la mda mfupi na nilitamni nianzishe mradi nikiwa bado niko kazini ila changamoto ni kwamba mshahara unaishia kwenye ada,chakula na nauli tena muda mwingine nakopa so mwisho wa mwezi ukifika unakuta pesa yote inapukutika.

Kampuni ninayofanya inatoa mikataba ya mwaka mmoja mmoja kiasi kwamba tunakosa sifa ya kukopesheka katika taasisi za kifedha,ingekuwa inatupa japo hata miaka 4 tungekopesheka na ningeutumia huo mkopo kuanzisha uwekezaji.

Sasa kutokana na ushauri wako pamoja na wadau wengine ambao wamenitahadharisha kuwa huenda mafao yasitoke mapema kama ambavyo nafikiria na muda huo nitakuwa sina kazi itasababisha niishi katika mazingira magumu zaidi...

Siwezi kupuuza ushauri hata kidogo ndio maana nimelileta hapa ili niweze kupata msaada katika kufikia malengo yangu...
kwa kuzingatia hayo yote nimeona nifanye maamuzi mengine ili niweze kupata mtaji wa kuandaa mazingira ya uwekezaji..

Mwakani watoto wangu wawili niwahamishe shule za kulipia niwapeleke za kawaida,halafu huyu mmoja aliyeko la sita nimwache amalize la 7 maana yeye kwa sasa haiwezekani na sekondari atasoma za kawaida, then kile kiasi nilichokuwa nakilipa kama ada ndio nikitumie kuwekeza hapa nyumbani.
Sawa kabisa kuhusu issue za shule za watoto. Vipi kuhusu mkeo? unamtumia vipi katika uzalishaji wa pato la familia? Kumwacha awe mama wa nyumbani bila shughuli yoyote ni kosa kubwa linalochangia kuanguka kwenu.

Mtengenezee mradi mdogo wenye kutumia mtaji mdogo ili ajifunze ujasiliamali. Mke ni nguvu kazi tosha sana ambayo ikifanikiwa utapata amani ya moyo.

Option nyingine ni wewe kama wewe kujiendeleza kielimu ili upate maarifa zaidi yatakayokupa kazi nzuri ambayo itakupa mtaji wa biashara. Hilo ni wazo la muda mrefu sana ambalo kama huna haraka unaweza kulifanyia kazi.

Jaribu kuyaandika maisha yako unayotaka kuishi na mipango ya kufanikisha hayo malengo na dira yako. Hauna mtaji so ukiingia kwenye hiyo mipango ya ujasiliamali bila mtaji na kuacha kazi itakuwa anguko kubwa sana kimaisha. Kaa chini andaa plan ya maisha ya muda mrefu kisha tafuta njia za kupita ili ufike unapopataka.

Nakupa mfano wangu binafsi, baada ya kuajiriwa nilitaka kuwa na cheo na pia kuwa na uwezo hivyo nikajiwekea malengo kuwa ili nipate cheo lazima nifanye kazi kwa bidii, kujituma na kuongeza elimu. Nikayafanyia kazi hayo katika kipindi cha miaka mitano nikawa na elimu ya kutosha na cheo kikapanda. Baada ya hapo nikawa na uwezo wa kukopa parefu na pia posho zikawa nyingi ndio nikaanza ujasiliamali na uwekezaji

Imenichukua miaka 15 kufikia kuwa mfanyakazi mwenye cheo na mjasiliamali. Siongei kwa kujisifia ila nakupa hamasa ili upitie njia sahihi ambayo mara nyingi uwa ni ndefu

Kaa chini chora ramani ya maisha yako halafu anza kufanyia kazi mpaka ufikie unapotaka. Bila kuwa na dira sahihi utapotea mazima. Naona kama una haraka kwa kuangali mwenzako amefanya nini. Kila mtu ana njia yake ambayo amepiga hesabu zake vizuri
 
Kama ajira inakulipa vizuri bora ukomae hapo hapo.

Hizi mambo za kukimbilia kufuga kuku utajikuta umepoteza kila kitu hadi huyo mwanamke.

Niko sahii kurekebishwa
Hapo kwenye kupoteza hadi Mwanamke------ JF kiboko kabisaaaaaaaaaaaaa
 
Sawa kabisa kuhusu issue za shule za watoto. Vipi kuhusu mkeo? unamtumia vipi katika uzalishaji wa pato la familia? Kumwacha awe mama wa nyumbani bila shughuli yoyote ni kosa kubwa linalochangia kuanguka kwenu.

Mtengenezee mradi mdogo wenye kutumia mtaji mdogo ili ajifunze ujasiliamali. Mke ni nguvu kazi tosha sana ambayo ikifanikiwa utapata amani ya moyo.

Option nyingine ni wewe kama wewe kujiendeleza kielimu ili upate maarifa zaidi yatakayokupa kazi nzuri ambayo itakupa mtaji wa biashara. Hilo ni wazo la muda mrefu sana ambalo kama huna haraka unaweza kulifanyia kazi.

Jaribu kuyaandika maisha yako unayotaka kuishi na mipango ya kufanikisha hayo malengo na dira yako. Hauna mtaji so ukiingia kwenye hiyo mipango ya ujasiliamali bila mtaji na kuacha kazi itakuwa anguko kubwa sana kimaisha. Kaa chini andaa plan ya maisha ya muda mrefu kisha tafuta njia za kupita ili ufike unapopataka.

Nakupa mfano wangu binafsi, baada ya kuajiriwa nilitaka kuwa na cheo na pia kuwa na uwezo hivyo nikajiwekea malengo kuwa ili nipate cheo lazima nifanye kazi kwa bidii, kujituma na kuongeza elimu. Nikayafanyia kazi hayo katika kipindi cha miaka mitano nikawa na elimu ya kutosha na cheo kikapanda. Baada ya hapo nikawa na uwezo wa kukopa parefu na pia posho zikawa nyingi ndio nikaanza ujasiliamali na uwekezaji

Imenichukua miaka 15 kufikia kuwa mfanyakazi mwenye cheo na mjasiliamali. Siongei kwa kujisifia ila nakupa hamasa ili upitie njia sahihi ambayo mara nyingi uwa ni ndefu

Kaa chini chora ramani ya maisha yako halafu anza kufanyia kazi mpaka ufikie unapotaka. Bila kuwa na dira sahihi utapotea mazima. Naona kama una haraka kwa kuangali mwenzako amefanya nini. Kila mtu ana njia yake ambayo amepiga hesabu zake vizuri
Well said,
Mradi nitakaouanzisha nyumbani ni kwaajili ya wife kuusimamia so hatokuwa tena hana shughuli ya kufanya mkuu.
kuhusu elimu niko na degree ya elimu,nimeipata chuo kikuu huria na kuhusu kazi yangu sio mbaya sana kwani take home yangu 700,000/
Plan ya aina ya maisha niyatakayo ninayo na ndiyo imekuwa ikinisumbua sana namna na ya kuifikia...na hii imetokanana na ukweli kwamba sikutaka wanangu wasome shule za kawaida na huko ndiko pesa zangu nyingi zinakokwenda mkuu.

Kwakuwa nimeamua kuwatoa ni matumaini yangu taratiibu nitaianza safari kuelekea uhuru wa kipato.

Mkuu nakushukuru sana kwa in put yako.
 
Back
Top Bottom