Huu ni mwaka wangu wa mwisho kuajiriwa

Kabla hujaacha kazi,jiulize je una plan b?ikitokea mradi haujafanikiwa utafanya nini ili kuitimizia familia mahitaji yake daily?mana kuna magonjwa,kula nk!
Ukiwa na hiyo plan b acha uende,ila kama huna usiache hiyo kazi!
 
Kabla hujaacha kazi,jiulize je una plan b?ikitokea mradi haujafanikiwa utafanya nini ili kuitimizia familia mahitaji yake daily?mana kuna magonjwa,kula nk!
Ukiwa na hiyo plan b acha uende,ila kama huna usiache hiyo kazi!
Plan b ipo,nimeandika kuwa nitamfungulia wife biashara pale nyumbani maana kuna nafasi ya kufanya hivyo..
 
Mkuu hakuna uwezekano ukafanya uwekezaji mahali huku ukiendelea na kazi nyingine?
Shida ni capital mkuu,mshahara unaishia kwenye matumizi nyumbani tu, na mda mwingine changamoto zinazidi kipato.
 
fanya hivi chukua milioni mbili au nne njo mafia kodi boti ndogo au jahazi jahazi unaweza nunua jahazi itakuwa inasafirisha mizigo au ukikodi boti na nyavu itakusaidia kuvua samak huku kukodi sawa na laki nane miezi minne au sita hio pesa unaweza irudisha kwa siku tatu au mbili uvuvi ukikubali
 
Karibu sana mtaani. Wazungu wanasema it is easier said than done. Sijajua umehesabu miaka mingapi hapo maana ulivyoelezea ni kama kila kitu ni Mtelezo sana.

Pitia hii video itakusaidia

 
Fuata ndoto zako na nafsi yako inavyokutuma .

Usiwasikilizs walimwengu.

Amini unachokitaka na fuata unachoamini .

Ajira zinachosha sometime hasa Kama maslahi Ni duni kazi nyingi muda huna ,watu wale wale hawakupi changamoto.



Sent from my TECNO P703 using JamiiForums mobile app
 
Ujasiriamali ni mgumu na ni utumwa kuliko ajira hasa hatua za mwanzoni.

Usiache kazi kuingia kwenye kilimo, ingia kwenye kilimo wakati bado una kazi.

That being said, lazima uchukue risks kufikia malengo yako but they got to be calculated risks. Good luck
 
Habari wakuu,

Baada ya kufanya kazi za kuajiriwa kwa muda sasa bila ya kuyafikia maisha ya ndoto zangu, pia baada ya kuishi maisha nisiyopendezwa nayo (kukosa uhuru wa kipato) nimekaa na kutafakari kwa kina juu ya hatma ya maisha yangu na kufikia maamuzi yafuatayo.

Mosi, kuna 4.3m PPF, hiki ni kiasi ambacho nilishindwa kukitoa enzi za mwendazake baada ya kupoteza ajira. Sasa niko kwenye kampuni nyingine ambapo michango yangu mpaka sasa ni 5m,so nataka nizihamishie huku na mpaka March mwakani unapoisha mkataba wangu nitakuwa na si chini ya 10m.

Pili,kabla ya December mwaka huu nitaenda Morogoro kufanya ziara maana kuna mshikaji wangu yupo kule naye alikuwa mwajiriwa somewhere akaamua kuacha kazi na kujikita katika kilimo na ufugaji (yuko njema sana), huyu jamaa yangu atakuwa msaada sana kwangu katika kutimiza matarajio yangu.

Tatu,nikishachukua hicho kiasi namfungulia wife mradi wa 2m nyumbani then mimi nasepa zangu porini ambapo nitafanya yafuatayo

. Kufuga nguruwe na kuku
. Kulima nyanya za kumwagilia

Hayo hapo juu nitayafanya kwa 4m na kiasi kilichobaki ambayo itakuwa ni 4m nitaiweka akiba then nitakitumia kununulia mazao kama mahindi nk kipindi cha mavuno.

Karibuni wakuu kwa ushauri zaidi.
Hizi ndio akili,leta mrejesho mambo yatakavyokuwa huko shambani,unaweza ukawa nabii mzuri na wengine tukafuata mfano.
Hizi ajira huwa tunazikimbilia kwa vile hakuna mbadala,lakini mifumo ya kujiajiri ingekuwa rafiki,nani anataka kupata taabu ya kusimama kutoka mbezi mpaka posta,unaenda kazini,na kurudi hivyo hivyo mwisho wa mwezi unakula Laki sita,hukopesheki,uwezi kununua shamba,huwezi kujenga kabla hujafika 40s
 
1.Ndio mkuu
2.Nilifanya kilimo cha nyanya kama trial hap hapa kwangu,nilifuata taratibu zote za wataalam na wazoefu na matokeo niliyaona mkuu. Pia miaka ya 2003-4 niliwahi kwenda kulima Iringa,nililima maharage karanga na alizeti ila ilikuwa ni kienyeji sana.
3.Interst ninayo tena kubwa sana,naweza kabisa kukaa shamba kwani nimeshahi kufanya hivyo miaka mingi japo sikuwa na mtaji wa kutosha.

Karibu mkuu
All the best..
Asilimia kubwa ya watu hata walioajiriwa at one point watastaafu na kulazimika kujiajiri..
Cha Msingi anza kufanya kwa kupenda(Do it with Passion)..kisha maslahi yafuate.
Ukitanguliza maslahi,mambo yakienda mrama unaweza kata tamaa kabisa ushindwe kunyanyuka..
Usisahau kutupa mrejesho huko mbeleni ili wengine tujifunze..

Sent from my SM-A405FN using JamiiForums mobile app
 
Mkuu ela za mafao usiziamini kabisa katika kuzipata zote.
Sisi kazi iliisha na tukaja kupewa mafao miezi karibia nane baada ya kukosa ajira na apo tulipewa asilimia chache sana na tukaambiwa zingine baada ya waka kupita.
Usitegemee sana NSSF wanaweza kukuangusha.
 
Back
Top Bottom