Huu ni muda muafaka Rais Magufuli kuijua sura halisi ya Prof. Muhongo

MAHANJU

JF-Expert Member
Aug 26, 2014
5,244
7,966
Kama kuna watu ambao walihisi Prof Muhongo alionewa kuhusishwa na kashfa ya ESCROW na Mkuu wa kaya nae anaamini hivyo kuwa alionewa, na hii ndio maana alimrudisha tena kwenye wadhifa wake wa awali wakati huu wa ufalme wake.

Sasa wa kuifahamu ESCROW A-Z ni Rais Magufuli baada Tanzania kuamriwa kulipa billion 320, hapa ndiko atakapojua ni nani mhusika kweli wa Sakata la ESCROW, hapa ndipo atakapojua kuwa uteuzi wake kwa Prof. Muhongo una tija kwa taifa au laah! Nina uhakika mkuu hatakubali haraka haraka kulipa zigo hilo lote pasipokujua ni nani amelitia taifa hasara.

Je, akikuta ni kweli Prof Muhongo nae alikuwemo kwenye michongo hiyo atamwacha aemdelee kuchapa kazi kunako wizara?
Je, atakuta Prof aliingizwa tu mkenge pasipo kujua na waliokuwa wamazunguka?

Mimi sina jibu kamili lakini kwa wakati huu tu pekee mkuu ataitambua taswira halisi ya Prof. Muhongo.
 
Yeye mpaka kumteua kuwa waziri maana yake alijidhihirisha sababu alikuwa anatuhumiwa na tuhuma za Eskrow kabla hajamteua sasa ikitokea akaja mtengua kwa baadae tokana na tuhuma hiyo hata yeye Rais atakuwa na makosa itanidi atuombe radhi watanzania maana alishauaminisha umma kuwa mtu huyu hana tatizo ndio mana akamuamini na kumpa uwaziri
 
Kama kuna watu ambao walihisi Prof Muhongo alionewa kuhusishwa na kashfa ya SCROW na Mkuu wa kaya nae anaamini hivyo kua alionewa, na hii ndio maana alimridisha tena kwenye wadhifa wake wa awali wakati huu wa ufalme wake.

Sasa wa kuifahamu ESCROW A-Z ni Rais Magufuli baada Tanzania kuamriwa kulipa billion 320, hapa ndiko atakapojua ni nani mhusika kweli wa Sakata la ESCROW, hapa ndipo atakapojua kua uteuzi wake kwa Prof Muhongo una tija kwa taifa au laah! Nina uhakika mkuu hatakubali haraka haraka kulipa zigo hilo lote pasipokujua ni nani amelitia taifa hasara.


Je, akikuta ni kweli Prof Muhongo nae alikuwemo kwenye michongo hiyo atamwacha aemdelee kuchapa kazi kunako wizara? Je, atakuta Prof aliingizwa tu mkenge pasipo kujua na waliokua wamazunguka? Mini sina jibu kamili lakini kwa wakati huu tu pekee mkuu ataitambua taswira halisi ya Prof.
Mkuu umetumwa au umekuja mwenyewe?
 
Sasa wa kuifahamu ESCROW A-Z ni Rais Magufuli baada Tanzania kuamriwa kulipa billion 320, hapa ndiko atakapojua ni nani mhusika kweli wa Sakata la ESCROW, hapa ndipo atakapojua kua uteuzi wake kwa Prof Muhongo una tija kwa taifa au laah! Nina uhakika mkuu hatakubali haraka haraka kulipa zigo hilo lote pasipokujua ni nani amelitia taifa hasara..
Kuweka kumbukumbu sawa ni kwamba sio JPM atakayelipa hili deni bali ni Watanzania yaani mimi na wewe.
Ili kuionyesha dunia kuwa na sisi tunazo 'organs of sense' ambazo ni active basi tulipe hili deni kwa masharti kwamba ni lazima aliyelisababisha ajulikane na hata ikibidi tujue pia alikusudia nini kutuingiza kwenye haya matatizo.

NOTE: Hata kama walifanya haya sio wanasiasa lakini walitumia siasa kutuibia hivyo katika kuwabana tusiangalie cha huyu ni Kafulila, Mbowe, TL nk bali tuungane kwa maslahi ya taifa huku tukijua 'foundations' zitapenyeza kitu kidogo kwa ajili ya propaganda!
 
Achilia mbali huyu waziri, kuna watu walipiga mpunga wengine wakasema pesa ya mboga, wengine wakajisifu wenyewe ni nyoka wa makengeza wanaojua kupiga deal, kuna watu wakagoma au kukaidi kuhojiwa na tume ya maadili. Mapendekezo ya kamati ya bunge yalipuuzwa, waziri karudi madarakani, wabunge wamerudi, hatukuambiwa akina nani walichota pesa stanbic bank hadi leo hii.

Iwe kahusika au hakuhusika, uzembe wa hali ya juu sana uliendesha hili sakata huku tukishuhudia mbunge aliyeibua huu uvundo akiitwa ngedere. Mbaya zaidi bado tunalipa pesa hadi leo hii.
Pamoja na yoooote hayo, jamaa ni mchapakazi lakini hili doa linaharibu na kumuondolea credibility yote.
 
Hivi kweli mkuu unaamini Magufuli haujui ukweli wa ESCROW? Mtu ambaye amekuwa kwenye baraza la Mawaziri tangu IPTL inaanzishwa asijue hii kitu? haiwezekani. CCM ni ile ile tu, hizi hela tutalipa na hakuna atakaye wajibishwa.
 
Kuweka kumbukumbu sawa ni kwamba sio JPM atakayelipa hili deni bali ni Watanzania yaani mimi na wewe.
Ili kuionyesha dunia kuwa na sisi tunazo 'organs of sense' ambazo ni active basi tulipe hili deni kwa masharti kwamba ni lazima aliyelisababisha ajulikane na hata ikibidi tujue pia alikusudia nini kutuingiza kwenye haya matatizo.

NOTE: Hata kama walifanya haya sio wanasiasa lakini walitumia siasa kutuibia hivyo katika kuwabana tusiangalie cha huyu ni Kafulila, Mbowe, TL nk bali tuungane kwa maslahi ya taifa huku tukijua 'foundations' zitapenyeza kitu kidogo kwa ajili ya propaganda!


Nnachokiona hapa, huenda wazee wachama wakaiunganisha kwenye operation ya Ujenzi iliyoahirishwa September mosi.
 
Ndugu Mahanju hoja yako ya msingi hasa ni ipi hapo? Kwa ufupi sijakuelewa unataka kutuma ujumbe gani funguka kama una taarifa zaidi kuhusu ESCROW na uhusika wa Prof. Muhongo.
Mkuu mada iko wazi, hujaelewa kipi?

Nikuulize swali... kwa kipindi wakati hiki ambacho ESCROW imerudi kiviingine tena na joto kali,Je, Mkuu wa kaya ataacha kuyafahamu vizuri mafisadi ya yaliyohusika na kulitia taifa hasara? Je, na Prof wetu atarudimo ndani ali zilikua ni fitina tu za kibongo?
 
Kama kuna watu ambao walihisi Prof Muhongo alionewa kuhusishwa na kashfa ya SCROW na Mkuu wa kaya nae anaamini hivyo kua alionewa, na hii ndio maana alimridisha tena kwenye wadhifa wake wa awali wakati huu wa ufalme wake.

Sasa wa kuifahamu ESCROW A-Z ni Rais Magufuli baada Tanzania kuamriwa kulipa billion 320, hapa ndiko atakapojua ni nani mhusika kweli wa Sakata la ESCROW, hapa ndipo atakapojua kua uteuzi wake kwa Prof Muhongo una tija kwa taifa au laah! Nina uhakika mkuu hatakubali haraka haraka kulipa zigo hilo lote pasipokujua ni nani amelitia taifa hasara.


Je, akikuta ni kweli Prof Muhongo nae alikuwemo kwenye michongo hiyo atamwacha aemdelee kuchapa kazi kunako wizara? Je, atakuta Prof aliingizwa tu mkenge pasipo kujua na waliokua wamazunguka? Mini sina jibu kamili lakini kwa wakati huu tu pekee mkuu ataitambua taswira halisi ya Prof.
Hakuna lolote!, deni tutalipa kwa mzigo huo kubebeshwa Watanzania wote kupitia kupandishwa kwa bili ya umeme na hakuna atakayeguswa kwa sababu kama ni Kutoa asante, ameanzia juu mpaka chini!, utamgusa nani, umuache nani?.

Kwani Richmond ilikuwaje? !. Mkataba ulivunjwa tukashitakiwa na kudaiwa tozo ya Dowans, watu bungeni wakajiapiza hatulipi na kuna wengine wakaapa kwa kiingereza "over my dead body!" (kuliko kulipa bora nife). Ukweli ni kuwa, deni lile limelipwa lote kimya kimya, gharama za umeme zimepanda kimya kimya na Watanzania wote tunalipia deni hili na hakuna yoyote aliyechukuliwa hatua zozote!, miongoni mwa wakajiapiza wengine ni mawaziri na wanaendelea kudunda!.
Pasco
 
Usipende kumlaumu muhongo!! Yeye pia alikuja akapata maji yamezidi unga, na waanzilishi wapo, iweje urukie muhongo.
Katika watu walionielewa vizuri ni wewe mkuu! Ila mkuu wa kaya lazima kwa sasa ataujua vizuri usafi wa prof.
 
Ndugu Mahanju hoja yako ya msingi hasa ni ipi hapo? Kwa ufupi sijakuelewa unataka kutuma ujumbe gani funguka kama una taarifa zaidi kuhusu ESCROW na uhusika wa Prof. Muhongo.
Hapo ni kitu gani hakijaeleweka?muhongo ni mhusika
 
Wewe ukiwa kwenu, baba akasema pesa aliyojengea nyumba yake hakuwahi kuiba, wewe mtoto utakuwa na uthubutu wa kuwaambia majirani kuwa baba aliiba? Hata kama ulikuwa unajua ukweli.
 
Kama kuna watu ambao walihisi Prof Muhongo alionewa kuhusishwa na kashfa ya ESCROW na Mkuu wa kaya nae anaamini hivyo kuwa alionewa, na hii ndio maana alimrudisha tena kwenye wadhifa wake wa awali wakati huu wa ufalme wake.

Sasa wa kuifahamu ESCROW A-Z ni Rais Magufuli baada Tanzania kuamriwa kulipa billion 320, hapa ndiko atakapojua ni nani mhusika kweli wa Sakata la ESCROW, hapa ndipo atakapojua kuwa uteuzi wake kwa Prof. Muhongo una tija kwa taifa au laah! Nina uhakika mkuu hatakubali haraka haraka kulipa zigo hilo lote pasipokujua ni nani amelitia taifa hasara.

Je, akikuta ni kweli Prof Muhongo nae alikuwemo kwenye michongo hiyo atamwacha aemdelee kuchapa kazi kunako wizara?
Je, atakuta Prof aliingizwa tu mkenge pasipo kujua na waliokuwa wamazunguka?

Mimi sina jibu kamili lakini kwa wakati huu tu pekee mkuu ataitambua taswira halisi ya Prof. Muhongo.
Mkuu tulikesha tunasema hilo jambo lkn watu wa upande wa pili walitupuuza na kutuona kama wafitini na wakaenda mbali sana kuwa tuna muonea wivu sasa matokeo yake ndiyo haya bill 320 ni robo ya makusanyo ya kodi kwa mwezi mzima tuwalipe hao magoha wakati mahospitalini dawa hatuna
 
Kama kuna watu ambao walihisi Prof Muhongo alionewa kuhusishwa na kashfa ya ESCROW na Mkuu wa kaya nae anaamini hivyo kuwa alionewa, na hii ndio maana alimrudisha tena kwenye wadhifa wake wa awali wakati huu wa ufalme wake.

Sasa wa kuifahamu ESCROW A-Z ni Rais Magufuli baada Tanzania kuamriwa kulipa billion 320, hapa ndiko atakapojua ni nani mhusika kweli wa Sakata la ESCROW, hapa ndipo atakapojua kuwa uteuzi wake kwa Prof. Muhongo una tija kwa taifa au laah! Nina uhakika mkuu hatakubali haraka haraka kulipa zigo hilo lote pasipokujua ni nani amelitia taifa hasara.

Je, akikuta ni kweli Prof Muhongo nae alikuwemo kwenye michongo hiyo atamwacha aemdelee kuchapa kazi kunako wizara?
Je, atakuta Prof aliingizwa tu mkenge pasipo kujua na waliokuwa wamazunguka?

Mimi sina jibu kamili lakini kwa wakati huu tu pekee mkuu ataitambua taswira halisi ya Prof. Muhongo.
Mimi siwezi mtetea mtu yeyote kwamba yeye ni msafi na mtumbua majipu wakati wengi walio chukua pesa hiyo kupitia kwa yule Mhindi na Stanbic bank hawajawahi kutajwa!!
 
Back
Top Bottom