Ndallo
JF-Expert Member
- Oct 1, 2010
- 7,619
- 4,292
Rejea heading yangu hapo juu ni kua kwa mtazamo wangu na tembea yangu Tanzania mikoa mingi palipo na kabila la mchaga lazima kuna kamaendeleo fulani na pia kama ukiwachunguza hili kabila utaona ni watu wanaopenda sana maendeleo na si kwao binafsi tu la hasha hata kwa jamii inayowazunguka! Tafadhali sana mniwie radhi sijaleta mada hii kwamba naingiza ukabila na wala mimi sio mchaga bali ni mtazamo wangu tu. Ili tuondokane na umasikini uliokidhiri hapa nchini kwetu na ndoto ya maisha bora kwakila mtanzania ni sawa na ile ndoto yakutaka kujenga gorofa angani! basi ni mchango wangu tu na mawazo yangu tu hembu tujaribu kuwatesti hawa jamaa na kama kuna mtu anapendekeza kabila jingine anakaribishwa kuchangia mada hii.