Umasikini ndio Ugonjwa Mbaya kuliko yote Duniani

Huo ni msemo wa masikini tu Kujifariji ... Baada ya kuona kwamba hana Mali ..Hivyo basi sehemu pekee Ambayo inakuwa inatagemea faraja yake ni kwa watoto wake na Tajiri mahali pekee anapo tegemea kupata faraja ni kwenye Mali zake haswaa pale anapo kosa uwezo wa kuwa na watoto
Huu usemi kuwa, masikini na watoto wake, tajiri na mali yake una maana gani? Msaada taf.
 
tumeamua kupena makavu live,basi kila mtu asichague silaha,habari mbaya kabisa ni hii
1562937068654.JPG
 
umaskini sio ugonjwa ,kutokuwa na dini ndio ugonjwa yenyewe .tatizo asalimia kubwa ya wana jf ni wafuasi wa gwijiboy, aliyekula kondo zake.no wonder.
 
NDUGU WAPO SHULENI NA KAZINI!

BAADA ya baba kufariki dunia, mama alibaki kuhangaika kufanya kazi ngumu, ikiwemo vibarua ili kulea watoto wake mapacha. Wa kiume Kulwa na Dotto wa kike.

Siku moja Kulwa alimuuliza mama: "Mbona tangu baba afariki ndugu hawatutembelei? Wanakwenda kwa baba mdogo na shangazi peke yake." Mama akajibu: "Ndio maana naamka pwee kwenda vibaruani ili niwaletee ndugu wengi na marafiki."

Siku nyingine Dotto aliuliza: "Mbona shangazi, baba mdogo na watoto wao hawatutembelei? Sisi ndio tunaenda kwao. Na tukienda hawatuchangamkii." Mama akajibu: "Ndio maana nakurupuka asubuhi kwenda vibaruani ili nanyi muwe mnatembelewa na mchangamkiwe."

Siku nyingine Kulwa alihoji: "Mbona ulisema unaenda vibaruani kutuletea ndugu na marafiki, watutembelee na kutuchangamkia lakini hatuwaoni?" Mama akajibu: "Nafanya vibarua nawapeleke shule. Huko mtapata ndugu na marafiki wa kuwatembelea."

Wakiwa sekondari bweni, likizo walirejea na marafiki. Dotto akasema: "Mama kweli shuleni kuna marafiki. Huyu ni rafiki yangu na yule ni rafiki wa Kulwa. Likizo hii wametumbelea. Likizo nyingine Kulwa atamtembelea rafiki yake na mimi nitaenda kwa rafiki yangu. Tumepata watu wa kututembelea."

Jioni mama aliwaita wanaye pembeni akawaambia: "Sikumaanisha hao marafiki mliokuja nao. Nataka huko shuleni msome kwa bidii na mtaona ndugu na marafiki wengi wa kuwatembelea." Walisoma na kuhitimu shahada za uongozi wa biashara.

Mama akawaambia: "Sasa karibia wale ndugu na marafiki wa kuwatembelea wataanza kufurika, fanyene kazi sasa." Kulwa na Dotto walifungua kampuni yao. Biashara zikawaendea vizuri. Wakaajiri mamia ya watu. Wakajenga nyumba kubwa tatu kwenye kiwanja cha heka mbili. Moja ya mama, Kulwa yake na Dotto pia. Wakazungushia uzio mmoja.

Siku moja jioni baada ya chakula cha jioni, Dotto aliuliza: "Mama kumbe tuna ndugu kijiji cha Mshinyole? Wamenipigia simu wanakuja kututembelea wiki ijayo." Dotto akasema: "Baba mdogo na shangazi walikuja ofisini leo, wanataka tufanye kikao cha ukoo, wanasema sisi watoto tunakua vibaya, hatuna ukaribu wa kindugu."

Mama akacheka, akasema: "Anzeni sasa kupokea ndugu. Fungueni milango mtembelewe. Msingeyashinda maisha msingetambulika. Baba mdogo wenu na shangazi yenu walikuwa wapi kuwakusanya kipindi kile? Sababu mlikuwa hamvutii. Baada ya kusoma na kufanikiwa kimaisha, tayari mnavutia. Jibu mnalo sasa, muwaambie na wajukuu zangu kama sitawaona kuwa ndugu na marafiki huja kwa wingi baada ya kufaulu shuleni na kufanikiwa kimaisha."

Basi sawa! Tuwaabie watoto wetu kuwa ndugu na marafiki wengi watawafuata kama watafaulu shuleni. Tusemezane kwamba tupige kazi tuyashinde maisha, ndugu na marafiki mbona ni wengi tu!

Ndimi Luqman MALOTO
 
Nyerere aliposema tuna maadui watatu. Umaskini ulikuwa ni adui akauvika uhai.kumbuka kuwa adui ni kitu chenye uhai. Hiyo ni lugha ya sanaa. So naposema umaskini ni ugonjwa nmetumia umahili wa lugha tu ili wenye kuelewa waelewe. Ni ugonjwa na ndo maana unatibika. Na pia si wa kujivunia hata kidogo.

Umeongea point boss,, ila ikumbukwe kwamba umaskin si ugonjwa wala laana kama inavo ongelewa mama mada zinazo husu umaskini naona zinajiongeza kwa wingi hapa JF,, bin adam wengi tunafeli kwa kujua kwamba alie nacho ndie anae pendwa na Mungu na asie nacho ndie adui ao labda anaecukiwa na Mungu,,,, tufanye kazi kwa bidi na tukumbuke kwamba Mungu humpa amtakae na wewe ulonacho leo usifkri kwamba Wewe ni kipenzi namba 1 wa Mungu na maskini ajuwe kwamba kuto kupata wala kuwa kwake maskini si kwamba Mungu anamchukia hamna ni mtihani tuu!!!?
 
huwezi amini ila kaa tu fikiria kwa makini. Ugonjwa mbaya kuliko wote ni Umaskini. Huu ni mbaya sana. huu ndo chanzo cha mambo mengi sana ambayo yamekuwa kikwazo katika maisha yetu. fikiria tu ukiwa maskini.
1. maskini mara nyingi hana haki... Mungu tu ndo humtolea haki maskini lakini kwa binadamu wenyewe kwa wenyewe maskini anakosa haki nyingi sana za kimsingi. ndo maana hata maskini akifa si issue kubwa. nenda amana, nenda muhimbili na hospital nyingine. maskini wanakufa kwa malaria,kujifungua,typhoid,kuhara n.k wanakufa daily na hakuna anayeshtuka. alipokufa mtoto wa Abbas Tarimba hadi Rais alienda mpa pole. unadhani ni kwa nini?

2. kwenye vikao michango ya maskini huwa inatupwa kapuni. watu wanataka mchango wa pesa wewe unachangia mawazo. hayo mawazo si yangekusaidia mwenyewe? maskini huwa wana maneno mengi sana ,mengi sana kutafuta justification ya anachotaka kiwe. tajiri huwa hawaongei sana. wanasema tu hili liwe hivi. watu wanapiga makofi.

3. ukiwa maskini ukataka kuchangia kwenye kikao.wanaweza kukuzuia na kusema unataka kuleta fujo. hawaamini kma utakuwa na mawazo jengefu. unayatoa wapi sasa? wewe mwenyewe umeshashindwa kujijenga kiuchumi yatajengaje wengine? kwa hiyo unanyoosha mkono wanakwambia " aaahhh .... sasa usitake kuleta fujo.. acha kwanza wengine wachangie"

4. ukiwa maskini huwezi chagua. unajua dhana ya kuchagua inakuwepo kama kuna vitu zaidi ya viwili. but kama kuna kitu kimoja huwezi chagua. so poor people cant choose. wanatumia wanachopata. hata marafiki huwezi chagua. utachaguaje wakati huna kichagulio?

5. ukiwa maskini hata aina ya mademu unaotaka unakuwa huna.... ukiwa na aina utaipataje?mbuzi hula kutokana na urefu wa kamba yake na kile kilichopo kwenye himaya yake. huwezi chagua demu sababu huna kichagulio. mkono mtupu haulambwi. maskini hutumia muda mwingi sana kufuatilia demu... na maneno mengi sana. kuna jamaa mpaka hufikia hatua ya kulia... ili aonewe huruma apewe K. umaskini ni tatizo kubwa sana.sisi wenye vijicent tunasema "xxx nadhani unafaa kugegedwa na mimi, unasemaje?" :D:D:D:D:D:D:D:D akisita sita unaendelea kwa mwingine.huna muda wa kubembeleza.

tajiri huwa haongei sana kwa demu. siyo mwanamke. demu.siyo msichana.demu. haongei sana. anampiga na wekundu kadhaa, kabla demu hajasikilizia utamu ukaisha anapigwa na kitu kingine then anakuwa laini analiwa. ndani ya masaa 24 mpaka 72 demu analiwa bila shida kabisa.

6. sifa kubwa ya maskini ni unafiki. maskini anakuwa mnafiki sana. anacheka cheka kila wakati na kwa kila jambo linalosemwa na tajiri. maskini hawezi kosoa.. hata akiambiwa we fala anacheka sana na kumsifia tajiri kuwa yupo social sana hadi anaweza watukana watu wengine. ila maskini hawezi mwambia tajiri yake fala mwenyewe. yeye anaona tajiri mtu poa kwa kupokea matusi toka kwa tajiri bila kurudisha. umaskini ni kupoteza self esteem. ni kunyanyasika. ndo maana kuna maskini mpaka hushikwa makalio na wao huishia kucheka tu.

7. maskini hata sauti hana... akiongea Mengi au Bakhresa atasikika. ongea wewe Pangu Pakavu Tia Mchuzi. nobody knows unasema nini and nobody cares. why should they? huna mchango wowote katika jamii.

8. maskini anakuwa muoga sana. muoga hata kwa kivuli chake mwenyewe... ni mtu mwenye waswasi wakati wote. ona tu akisimamishwa na polisi, akikamatwa na polisi au akiwa na tatizo flani. maskini anakuwa muoga anatetemeka sana. anakosa confidence kabisa.

9. maskini anakufa mara nyingi zaidi kuliko tajiri. mapambano anayokutana nayo maskini ni kama kila wakati anakufa kwa kukoswa koswa na vibaka, magonjwa,mawazo,njaa, kukosa kujiamini n.k tajiri mara nyingi anaelewa moja ya silaha kubwa aliyo nayo ni pesa. ndo maana akikutana na vibaka wakataka kumpora simu anawapa tu anajua kesho atanunua nyingine. maskini anataka afight nao.. sababu anajua simu kaipata kwa mbinde sana haiwezekani waje watu wachukue kirahisi tu..mwishowe wanamchoma na bisibisi anakufa anaoza. wakati tajiri hafi kirahisi maana mpaka leo hi kuna watu wanamzungumzia mengi reginald.

10. sifa nyingine ya maskini ni Ulalamishi. maskini ni walalamishi sana. watalaumu kila kitu. ukipita na gari bahati mbaya ukamwagia maji atakulaani sana... ukitimua vumbi kidogo atalaani sana. usipompa lift atalaani sana. ukimpa akishuka atalalamika kuwa umempa lift kumringishia gari. ukivaa vizuri wewe atalalamika yeye.... ukila vizuri wewe atalalamika yeye. maskini anamlaumu kila mtu kwa umaskini wake. anailaumu serikali, anamalumu mbunge,anamlaumu mjumbe wa nyumba kumi ,anamlaumu jirani... anamlaumu Mungu, analaumu nchi, analaumu hali ya hewa, analaumu wadudu,anawalaumu wanyama, analaumu ndege... analaumu kila kitu. hii humsaidia kushusha mzigo moyoni mwake.

tajiri huwezi kuta analalamika lalamika kipuuzi. kuna siku nlikuwa natembea bahati mbaya gari ikakanyaga maji yakanirukia nguoni.sikuona shida...zilikuwa siku za mvua...nilielewa ni jambo la kawaida kwa magari wakati flani kufanya hivyo na dereva asiwe amekusudia.jamaa mmoja pembeni akasema " wenye magari wa****i sana hata hawajali watembeao kwa miguu" nlimwambia mbona sasa na mimi umenitukana? akaniuliza kwa nini?nikamwambia hata mimi nina magari na si ajabu siku nikatembea nikakanyaga maji bahati mbaya yakamrukia mtu"

utagundua maskini anakuwa na hasira. tena hasira kali sana,stress au msongo wa mawazo. ole wako umkanyage bahati mbaya.. atakulaumu sana... atatukana hasira zake zoote ziishie kwake. ukiandika uzi wako atakushambulia bila sababu za maana. yaani kutokuwa kwake yeye na pesa atajaribu kuhusisha na uzi wako hata kama unazungumzia suala la mapenzi au mpira. atatokwa na povu sana na utashangaa haya yanatoka wapi?

anyway kuna matatizo mengi yanatokana na umaskini. hebu tujaribu kuungana kuupiga vita umaskini. mimi si maskini ila nimewah kipindi flani kuishi maisha ya kimaskini. niliteseka sana moyoni.niligundua mambo mengi sana miaka hiyo.nikazidisha chuki dhidi ya umaskini. maskini hata marafiki zako sometime wanakukwepa, wanakukimbia. wanakuona huna akili. unajua siku zote mwenye pesa ndo mwenye akili?

ukiwa maskini kila mtu anakuja kukupa ushauri. na wewe huwezi toa ushauri ukaonekana wa maana.si ungeutumia mwenyewe? so wewe unakuwa na kazi ya kushauriwa kila wakati.unakuwa na kazi ya kupokea tu. TUPIGANE KWANZA VITA NA UMASKINI. YALE MENGINE YATAKUWA SOLVED TU. AMA SIVYO VIJANA WENGI MTAISHIA KULA TU KWA MACHO NA KUWA NA MSONGO WA MAWAZO HATA HUMU JF.

NYONGEZA.
Ukiwa maskini halafu mkawa kwenye jumuiya kisha simu ya mtu ikawa haionekani... unaanza kupoteza amani.. unahisi jamaa wanakuhisi wewe ndo umechukua. hivyo unalazimika kuongoza katika kuitafuta mpaka ipatikane.ama sivyo utaacha impression wewe ndo umeichukua.

ukiwa maskini hata uikitokea mmekaa watu wengi halafu mmoja akatoa gesi chafu.. watu wanakutizama wewe wanaamini wewe ndo umeharibu hali ya hewa.eneo hilo. yaani kila kitu kibaya kinahusishwa na maskini na kila kizuri kinahusishwa na utajiri.
Umesema kweli na haitabadilika!
 
huwezi amini ila kaa tu fikiria kwa makini. Ugonjwa mbaya kuliko wote ni Umaskini. Huu ni mbaya sana. huu ndo chanzo cha mambo mengi sana ambayo yamekuwa kikwazo katika maisha yetu. fikiria tu ukiwa maskini.
1. maskini mara nyingi hana haki... Mungu tu ndo humtolea haki maskini lakini kwa binadamu wenyewe kwa wenyewe maskini anakosa haki nyingi sana za kimsingi. ndo maana hata maskini akifa si issue kubwa. nenda amana, nenda muhimbili na hospital nyingine. maskini wanakufa kwa malaria,kujifungua,typhoid,kuhara n.k wanakufa daily na hakuna anayeshtuka. alipokufa mtoto wa Abbas Tarimba hadi Rais alienda mpa pole. unadhani ni kwa nini?

2. kwenye vikao michango ya maskini huwa inatupwa kapuni. watu wanataka mchango wa pesa wewe unachangia mawazo. hayo mawazo si yangekusaidia mwenyewe? maskini huwa wana maneno mengi sana ,mengi sana kutafuta justification ya anachotaka kiwe. tajiri huwa hawaongei sana. wanasema tu hili liwe hivi. watu wanapiga makofi.

3. ukiwa maskini ukataka kuchangia kwenye kikao.wanaweza kukuzuia na kusema unataka kuleta fujo. hawaamini kma utakuwa na mawazo jengefu. unayatoa wapi sasa? wewe mwenyewe umeshashindwa kujijenga kiuchumi yatajengaje wengine? kwa hiyo unanyoosha mkono wanakwambia " aaahhh .... sasa usitake kuleta fujo.. acha kwanza wengine wachangie"

4. ukiwa maskini huwezi chagua. unajua dhana ya kuchagua inakuwepo kama kuna vitu zaidi ya viwili. but kama kuna kitu kimoja huwezi chagua. so poor people cant choose. wanatumia wanachopata. hata marafiki huwezi chagua. utachaguaje wakati huna kichagulio?

5. ukiwa maskini hata aina ya mademu unaotaka unakuwa huna.... ukiwa na aina utaipataje?mbuzi hula kutokana na urefu wa kamba yake na kile kilichopo kwenye himaya yake. huwezi chagua demu sababu huna kichagulio. mkono mtupu haulambwi. maskini hutumia muda mwingi sana kufuatilia demu... na maneno mengi sana. kuna jamaa mpaka hufikia hatua ya kulia... ili aonewe huruma apewe K. umaskini ni tatizo kubwa sana.sisi wenye vijicent tunasema "xxx nadhani unafaa kugegedwa na mimi, unasemaje?" :D:D:D:D:D:D:D:D akisita sita unaendelea kwa mwingine.huna muda wa kubembeleza.

tajiri huwa haongei sana kwa demu. siyo mwanamke. demu.siyo msichana.demu. haongei sana. anampiga na wekundu kadhaa, kabla demu hajasikilizia utamu ukaisha anapigwa na kitu kingine then anakuwa laini analiwa. ndani ya masaa 24 mpaka 72 demu analiwa bila shida kabisa.

6. sifa kubwa ya maskini ni unafiki. maskini anakuwa mnafiki sana. anacheka cheka kila wakati na kwa kila jambo linalosemwa na tajiri. maskini hawezi kosoa.. hata akiambiwa we fala anacheka sana na kumsifia tajiri kuwa yupo social sana hadi anaweza watukana watu wengine. ila maskini hawezi mwambia tajiri yake fala mwenyewe. yeye anaona tajiri mtu poa kwa kupokea matusi toka kwa tajiri bila kurudisha. umaskini ni kupoteza self esteem. ni kunyanyasika. ndo maana kuna maskini mpaka hushikwa makalio na wao huishia kucheka tu.

7. maskini hata sauti hana... akiongea Mengi au Bakhresa atasikika. ongea wewe Pangu Pakavu Tia Mchuzi. nobody knows unasema nini and nobody cares. why should they? huna mchango wowote katika jamii.

8. maskini anakuwa muoga sana. muoga hata kwa kivuli chake mwenyewe... ni mtu mwenye waswasi wakati wote. ona tu akisimamishwa na polisi, akikamatwa na polisi au akiwa na tatizo flani. maskini anakuwa muoga anatetemeka sana. anakosa confidence kabisa.

9. maskini anakufa mara nyingi zaidi kuliko tajiri. mapambano anayokutana nayo maskini ni kama kila wakati anakufa kwa kukoswa koswa na vibaka, magonjwa,mawazo,njaa, kukosa kujiamini n.k tajiri mara nyingi anaelewa moja ya silaha kubwa aliyo nayo ni pesa. ndo maana akikutana na vibaka wakataka kumpora simu anawapa tu anajua kesho atanunua nyingine. maskini anataka afight nao.. sababu anajua simu kaipata kwa mbinde sana haiwezekani waje watu wachukue kirahisi tu..mwishowe wanamchoma na bisibisi anakufa anaoza. wakati tajiri hafi kirahisi maana mpaka leo hi kuna watu wanamzungumzia mengi reginald.

10. sifa nyingine ya maskini ni Ulalamishi. maskini ni walalamishi sana. watalaumu kila kitu. ukipita na gari bahati mbaya ukamwagia maji atakulaani sana... ukitimua vumbi kidogo atalaani sana. usipompa lift atalaani sana. ukimpa akishuka atalalamika kuwa umempa lift kumringishia gari. ukivaa vizuri wewe atalalamika yeye.... ukila vizuri wewe atalalamika yeye. maskini anamlaumu kila mtu kwa umaskini wake. anailaumu serikali, anamalumu mbunge,anamlaumu mjumbe wa nyumba kumi ,anamlaumu jirani... anamlaumu Mungu, analaumu nchi, analaumu hali ya hewa, analaumu wadudu,anawalaumu wanyama, analaumu ndege... analaumu kila kitu. hii humsaidia kushusha mzigo moyoni mwake.

tajiri huwezi kuta analalamika lalamika kipuuzi. kuna siku nlikuwa natembea bahati mbaya gari ikakanyaga maji yakanirukia nguoni.sikuona shida...zilikuwa siku za mvua...nilielewa ni jambo la kawaida kwa magari wakati flani kufanya hivyo na dereva asiwe amekusudia.jamaa mmoja pembeni akasema " wenye magari wa****i sana hata hawajali watembeao kwa miguu" nlimwambia mbona sasa na mimi umenitukana? akaniuliza kwa nini?nikamwambia hata mimi nina magari na si ajabu siku nikatembea nikakanyaga maji bahati mbaya yakamrukia mtu"

utagundua maskini anakuwa na hasira. tena hasira kali sana,stress au msongo wa mawazo. ole wako umkanyage bahati mbaya.. atakulaumu sana... atatukana hasira zake zoote ziishie kwake. ukiandika uzi wako atakushambulia bila sababu za maana. yaani kutokuwa kwake yeye na pesa atajaribu kuhusisha na uzi wako hata kama unazungumzia suala la mapenzi au mpira. atatokwa na povu sana na utashangaa haya yanatoka wapi?

anyway kuna matatizo mengi yanatokana na umaskini. hebu tujaribu kuungana kuupiga vita umaskini. mimi si maskini ila nimewah kipindi flani kuishi maisha ya kimaskini. niliteseka sana moyoni.niligundua mambo mengi sana miaka hiyo.nikazidisha chuki dhidi ya umaskini. maskini hata marafiki zako sometime wanakukwepa, wanakukimbia. wanakuona huna akili. unajua siku zote mwenye pesa ndo mwenye akili?

ukiwa maskini kila mtu anakuja kukupa ushauri. na wewe huwezi toa ushauri ukaonekana wa maana.si ungeutumia mwenyewe? so wewe unakuwa na kazi ya kushauriwa kila wakati.unakuwa na kazi ya kupokea tu. TUPIGANE KWANZA VITA NA UMASKINI. YALE MENGINE YATAKUWA SOLVED TU. AMA SIVYO VIJANA WENGI MTAISHIA KULA TU KWA MACHO NA KUWA NA MSONGO WA MAWAZO HATA HUMU JF.

NYONGEZA.
Ukiwa maskini halafu mkawa kwenye jumuiya kisha simu ya mtu ikawa haionekani... unaanza kupoteza amani.. unahisi jamaa wanakuhisi wewe ndo umechukua. hivyo unalazimika kuongoza katika kuitafuta mpaka ipatikane.ama sivyo utaacha impression wewe ndo umeichukua.

ukiwa maskini hata uikitokea mmekaa watu wengi halafu mmoja akatoa gesi chafu.. watu wanakutizama wewe wanaamini wewe ndo umeharibu hali ya hewa.eneo hilo. yaani kila kitu kibaya kinahusishwa na maskini na kila kizuri kinahusishwa na utajiri.
Ni kweli mkuu,tukazane kuupiga umaskini
 
Sure, hata watoto wa masikini hujiona dhaifu mbele ya watoto wa tajiri.pia mke wa masikini anaweza kuwa na hasira zisizo na sababu kwa mke wa tajiri, ni shida tupu, ni sawa na kusema one crisis leads to another ni mnyororo wa matatizo kwa kwenda mbele, tutafuteni hizi hela enyi watu japo juhudi haishindi kudra.
 
66 Reactions
Reply
Back
Top Bottom