Huu ndiyo utaratibu wa kuondoa ukomo wa Urais kwenye katiba ya JMT ya 1977

Kuondoa ukomo au kumuongezea Rais ukomo wa uongozi bila shaka unataka umakini wa hali ya juu, vinginevyo tunakaribisha shetani awe miongoni mwetu bila sababu ya msingi.

Kunahitajika kutumia fedha nyingi ambazo hatunazo kupiga kura ya kujua nani wanapenda na nani hawapendi. Wale wanaopenda ni kwanini na wale ambao hawapendi ni kwanini.

Mtu ambae ni mnufaika wa moja kwa moja hawezi kuwa chanzo cha kubadilisha Katiba ili aendelee kunufaika kupitia mabadiliko pendekezwa. Wazo la kuongeza, kupunguza au kubakiza vilevile ni swala la wananchi sio kikundi.
Naunga mkono hoja,
Hili la rais Magufuli kuongezewa muda, wengi ndio wanalisikia sasa, angalia hapa limependekezwa toka lini

Hili ni bandiko la 2015

Kwa Kasi hii ya Magufuli, kuna haja Kufanya Uchaguzi wa Rais 2020?
4. Na hiyo 2025 tukimuona Magufuli bado anaweza, na anatufaa, jee kuna ubaya kuibadili hiyo katiba yetu ili tumpatie extension of time ya kutosha kuinyoosha Tanzania hadi inyooke kabisa?!.

5. Kwani katiba ni nini?, si ni kipande tuu cha karatasi?!, ingekuwa katiba ni muhimu kihivyo kama ambavyo watu wanataka kutuaminisha humu, nini muhimu zaidi kwa taifa letu Tanzania, kati ya katiba ambayo ni kipande tuu cha karatasi na maamuzi ya rais Magufuli ambaye ni rais wa nchi, aliyechaguliwa na watu, katika uchaguzi huru na wa haki?.

6. Na Katiba ni ya nani?!, ni yetu?!, na iko kwa manufaa ya nani?!, si ipo kwa manufaa yetu?!, hivyo sisi ndio muhimu kuliko katiba, hivyo kama sisi Watanzania, katika umoja wetu, tukiamua tunamtaka Magufuli aendelee tuu idefinately, si tunaweza kuiweka tuu pembeni hiyo katiba, na tukaendelea na Magufuli wetu mpaka tutosheke naye?!.

7. Sasa kama Magufuli anatufaa sana kuliko hata katiba na ndio maana anaweza hata kuikanyaga, na katiba haitamruhusu kuendelea baada ya 2025, kuna ubaya gani kuibadili katiba kwa manufaa yetu, na kumwacha aendelee tuu kama Kagame, Museveni na Mugabe?.

8. Au kwani Katiba ni Msahafu kusema haiwezi kubadilishwa?!. Kama katiba inakanywa na hakuna kinachofanyika, Jee kuna ubaya kama tutaibadili katiba na Magufuli akapatiwa muda wa kutosha kabisa wa kuinyoosha nchi yetu kama Kagame anainyoosha Rwanda, , Museveni anavyoinyoosha Uganda na Mugabe anavyoinyoosha Zimbabwe?.

Jee wewe una maoni gani kuhusu hoja zangu hizi?!.

Paskali
Wanabodi, kwanza angalieni tarehe ya bandiko hili, kisha angalia hoja No. 4, 5, 6, 7 na 8 za bandiko hili, kisha sikiliza kilichozungumzwa jana Bungeni Dodoma kuhusu hoja hii.



P
 
Naunga mkono hoja,
Hili la rais Magufuli kuongezewa muda, wengi ndio wanalisikia sasa, angalia hapa limependekezwa toka lini

Hili ni bandiko la 2015

Kwa Kasi hii ya Magufuli, kuna haja Kufanya Uchaguzi wa Rais 2020?

Wanabodi, kwanza angalieni tarehe ya bandiko hili, kisha angalia hoja No. 4, 5, 6, 7 na 8 za bandiko hili, kisha sikiliza kilichozungumzwa jana Bungeni Dodoma kuhusu hoja hii.



P

Nakubaliana na mawazo ya mdau mmoja hivi kuwa kama ukikurupuka kusoma nyuzi za Pascal unaweza elewa kingine wakati yeye alichomaanisha ni kitu kingine,
Leo nimefungua hiyo link ya thread nikasoma kwa utulivu mkubwa na kwa kutumia sehemu kubwa ya ubongo fikirishi nikachanganya na za mwalimu wangu Tabora school nimeelewa hadi nikaishia kucheka tu ndio maana hata sasa nimeelewa kwa nini P hujapewa hata ukuu wa wilaya
 
Kama katiba iliwekwa kwa nini hamkubadilisha wakati wa kikwete au Mkapa mlipoitwa Dodoma mlienda kufanya nini .10yrs aondoke ajenge mfumo imara wa uwajibikaji ninachokiona hi kila Rais anajenga team yake na watu wake matokeo yake mpaka team ifanikiwe wanaona muda hautoshi kwani team developments stages kama hatukuwa mfumo ni ndefu from Forming,Storming,Norming,Reframimg etc
 
Hivi unafikiri hakuna mtu mzuri zaidi ya Magufuli? Kwani akizaliwa peke yake duniani? Akifa kesho nchi haiwezi kuendelea bila yeye? Kwani kikubwa alichofanya ambacho hakuna awezaye kufanya chini ya mbingu? Inamaana maraisi wengine hawakufanya mazuri kwa nchi hii? Uzuri ni kwamba kila ukimpata demu mpya, lazima utamwona wa zamani hafai. Wapo wengi sana, tena sana. Acheni akili za mgando, maana cku hizi mshaanza kumsujudia kama mungu wenu! Shameful Tanzanian for short-minded brains and thinking
 
Kuondoa ukomo au kumuongezea Rais ukomo wa uongozi bila shaka unataka umakini wa hali ya juu, vinginevyo tunakaribisha shetani awe miongoni mwetu bila sababu ya msingi.

Kunahitajika kutumia fedha nyingi ambazo hatunazo kupiga kura ya kujua nani wanapenda na nani hawapendi. Wale wanaopenda ni kwanini na wale ambao hawapendi ni kwanini.

Mtu ambae ni mnufaika wa moja kwa moja hawezi kuwa chanzo cha kubadilisha Katiba ili aendelee kunufaika kupitia mabadiliko pendekezwa. Wazo la kuongeza, kupunguza au kubakiza vilevile ni swala la wananchi sio kikundi.

Wakati wanaweka huo ukomo wewe uliombwa ushauri kwa njia ya kura?
 
Back
Top Bottom