Huu ndiyo Mkataba wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar (Articles of Union)

Kama mkataba wenyewe wa muunganondio huu au ndio ulivyo, basi, sasa naelewa kwa nini wanauficha! Umeaandaliwa kisanii either kwa makusudi au kwa kutojua! It is a badly drafted contract!
 
Bila kukaa kitako tukaujadili kwa kina na kukubaliana njia mwafaka za kutatua hayo matatizo tutazidi kutengeneza bomu la hatari kwa kila upande.
 
Ni kweli kabisa mkuu. Ishu haiko sawa kwani haijakamilika. Ni bora angesema huo ni mfano tu wa mkataba wenyewe.

mkuu download attachment ya sheria ya muungano. inarudia yote yaliyosemwa katika mkataba huo kwa kiingereza na ni sehemu ya sheria za Tanzania na huko imesainiwa na speaker wa bunge. so hii document ni sahihi kabisa
 
Mtoa mada.

Muungano hatukuungana kuunda jamuhuri moja huru,kwa sababu ukiangalia huo article of union wa mwanzo unasema hivi, jamuhuri ya muungano wa tanganyika na zanzibar,its means that sio jamuhuri moja ni mbili hizo ambazo ni huru,kuna tanganyika na zanzibar,wakati huo walipoungana zanzibar ilikuwa na kiti chake katika umoja wa mataifa,ilijulikana kama ni nchi huru kabisa,tanganyika wakati huo ilikuwa bado haijaomba uwanachama katika umoja wa mataifa.

Mwaka 1984 wakati walipofanya marekebisho ya katiba na kuunganisha ASP na TANU,na pia kubadilisha jina la muungano kuitwa tanzania badala ya JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR,Ndipo usanii ulipochezwa na kufanya dola moja huru,kikaondolewa kiti cha zanzibar jina pale UN na kuitwa jamuhuri ya muungano wa tanzania badala jamuhuri ya muungano wa tanganyika na zanzibar.

Haya sasa turudi katika mkataba wa muungano,kuna sehemu gani ambayo inasema muungano huu utakuwa milele au miaka kumi au miaka 1 au mitano,tunaomba ufafanuzi juu ya mkataba huu.

Katika kumbukumbu zetu ,sisi generation ya sasa tunazo kumbukumbu zinazo sema kuwa mkataba ulikuwa wa miaka kumi tu,baada ya kuasisiwa muungano huu,kabla karume kufariki ulikuwa haujatimiza miaka kumi,na hapo karume mwenyewe alikuwa tayari ameshachoka nao,na alikuwa akisubiri kwa hamu imalize hiyo miaka kumi,hadi leo hii muungano haukulizwa,na nyerere alifanya kila njia kuulinda,na hakutaka hata mtu aulize,kuongea wakati wa nyerere suala la muungano ujeu ni mhaini,unaenda jela maisha yako,yote hayo ilikuwa ya nini ?

Ukweli ni kwamba muungano ulikuwa ushapitwa na wakati,na wazanzibari walikuwa hawautaki,ulipofanywa muungano huu wananchi hawakuulizwa,na ndipo teknic aliyotumia ccm,ni kuunganisha chama tawala,kuwadhibiti viongozi wa zanzibar na tanganyika,kuwapa kila watakacho viongozi hawa na kuwaekea vikwazo kuulinda muungano huu haramu.

Wazanzibari jiulizeni wanaudai muungano huu au mkataba wa muungano kwa sababu ipi ? Sio kama haupo ila upo ispokuwa mkataba unasema kuwa muungano ulikuwa ni wa miaka kumi tu,na ndio maana viongozi wanashndwa kuutoa huo mkataba kwani hau exit tena,kitaifa na kimataifa.

Ingelikuwa hata huo muungano ni halali kabisa,basi wazanzibari wanahaki ya kuukataa muungano,kwani ni haki yetu ya msingi kabisa,huu muungano sio msahafu wala bibilia,tunayo haki ya kuhoji ,tunayo haki ya kufanya marekebisho,tunayo haki ya kuuvunja au kuujenga ukawa mzuri zaidi,tusifananishe muungano wetu kama ndoa,ever ever never.
 
Ahsante sana Subiri Jibu hiki kitu hata mimi ninacho yaani extract ya mtu ambayo ni subject to perception ya mwandishi!

Changamoto:
Tunahitaji original document iliyosainiwa na Karume na Nyerere along side their origin signatures nadhani hii ndiyo wapemba walikwenda kuidai UN! Nashukuru hiki ni kianzio but we need to go further beyond resonable mashaka
 
Heshima zako mkuu,

Hivi haiwezekani mtu kufungua kesi kwenye mahakama ya kimataifa, I mean kesi kama zile za Mtikila kudai hizi article ambazo ziwekwe wazi.

Kama ikithibitika kwamba kweli haziko, basi maana yake hazikuwahi kuweko na hivyo muungano ni batili.

Sijui unasemaje na mnasemaje?

Unajua kama humu JF kuna mwanasheria anaweza kusaidia. Haiwezekani document kama hiyo ifichwe.
 
Mtoto anapotaka kuiona hati ya ndoa baina ya baba na mama yake inakueleza nini?.. bila shaka tatizo analo mtoto mwenyewe hajiamini kama kazaliwa na wazazi hao..
 
Mtoto anapotaka kuiona hati ya ndoa baina ya baba na mama yake inakueleza nini?.. bila shaka tatizo analo mtoto mwenyewe hajiamini kama kazaliwa na wazazi hao..

Suala linabaki kwamba ili kuuimarisha muungano inabidi tuone hizo hati au mkataba, tuujadili, tuweke muungano sawa. La kama itaendelea kuwa siri, nadhani hatuutakii mema muungano. Hii ni haki ya raia.
 
Ilitakiwa na Zanzibar nako Bunge likaujadili huo Mkataba, tatizo mara baada ya Mapinduzi ya mwaka 1964 Zanzibar kulikuwa hakuna vongozi wa kuchaguliwa na wananchi. Na Zanzibar ilifanya uchaguzi wake wa kwanza miaka 16 baada ya Mapinduzi hapo mwaka 1980. Mkataba ungejadiliwa na nani wakati nchi ilikuwa inaendeshwa na wanamapinduzi chini ya Baraza la Mapinduzi Zanzibar?
 
Zanzibar kulikuwa na Bunge wakati Karume na Nyerere wanatiliana saini mkataba wa Muungano? Kwa hiyo kama nchi ilikuwa inaendeshwa kwa sheria za dharura na kauli za rais, basi muungano ni halali!!
 
Mtumaji wa post namba hii .

Jina Jamhuri ya Tanganyika na Zanzibar haifanyi kuwe na viti viwili kule UN.

Kumbuka hata UK ni United Kingdom of Great Britain and Northen Ireland.

Kuna seat moja tu kule kwa UK yote na kamwe si tatu kwa maana ya England, Scotland na Northen Ireland.
 
Ilitakiwa na Zanzibar nako Bunge likaujadili huo Mkataba, tatizo mara baada ya Mapinduzi ya mwaka 1964 Zanzibar kulikuwa hakuna vongozi wa kuchaguliwa na wananchi. Na Zanzibar ilifanya uchaguzi wake wa kwanza miaka 16 baada ya Mapinduzi hapo mwaka 1980. Mkataba ungejadiliwa na nani wakati nchi ilikuwa inaendeshwa na wanamapinduzi chini ya Baraza la Mapinduzi Zanzibar?

Mimi naomba kuuliza,

Mapinduzi ya Zanzibar yalikuwa ni ya kwanza hapa East Africa. Mapinduzi mengine hapa East Africa ni yale yaliyotokea Uganda January 25, 1971 yaliyomuondoa Obote na kumuweka Idi Amin.

Hivyo, utawala wa Idi Amin na Karume unafanana kwa kitendo cha wote wawili kuingia madarakani kwa mapinduzi. Wote wawili hawakupigiwa kura hadi walipong'oka madarakani.

Sasa linakuja swali langu.

Je, iwapo baada ya mwezi tangu Amin kumpindua Obote, Nyerere angekuwa rafiki wa Amin na kwa urafiki huo tukaungana na Uganda kama tulivyoungana na Zanzibar, je muungano huo ungehesabiwa kuwa ulikuwa na ridhaa ya watu wa Uganda?

Wakati mnanijibu kumbukeni kazi ya mapinduzi duniani kwanza kabisa huondoa katiba iliyopo na vyombo vyake kama Bunge, mahakama na kadhalika na ndivyo ilivyofanyika Uganda na Zanzibar.

Natumaini majibu tele.
 
Mimi naomba kuuliza,

Mapinduzi ya Zanzibar yalikuwa ni ya kwanza hapa East Africa. Mapinduzi mengine hapa East Africa ni yale yaliyotokea Uganda January 25, 1971 yaliyomuondoa Obote na kumuweka Idi Amin.

Hivyo, utawala wa Idi Amin na Karume unafanana kwa kitendo cha wote wawili kuingia madarakani kwa mapinduzi. Wote wawili hawakupigiwa kura hadi walipong'oka madarakani.

Sasa linakuja swali langu.

Je, iwapo baada ya mwezi tangu Amin kumpindua Obote, Nyerere angekuwa rafiki wa Amin na kwa urafiki huo tukaungana na Uganda kama tulivyoungana na Zanzibar, je muungano huo ungehesabiwa kuwa ulikuwa na ridhaa ya watu wa Uganda?

Wakati mnanijibu kumbukeni kazi ya mapinduzi duniani kwanza kabisa huondoa katiba iliyopo na vyombo vyake kama Bunge, mahakama na kadhalika na ndivyo ilivyofanyika Uganda na Zanzibar.

Natumaini majibu tele.

Kwani muungano unafanyika kwa ridhaa ya maraisi au bunge au wananchi.
 
Umepitishwa na Bunge siku ya tarehe Ishirini na Tano ya Aprili, 1964.


……………………………………………………………………………… …………………….
Pius Msekwa, Karani wa Bunge


……………………………………………………………………………… …………………….
Adam Sapi Mkwawa, Spika
25 Aprili 1964


xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
SOURCE:

1: {THE PATNERSHIP, ISBN: 9789987880553, pg. 156, Author: Aboud Jumbe, }

2: {Zanzibar hadi mwaka 2000: ISBN: 9789987898015, pg. 201, Author: Ali Shaaban Juma}
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Wapi ridhaa ya Bunge la Zanzibar?
 
sikilizeni wana jf,tusiongee pumba hapa,kama kuna huo mkataba halisi una sign ya viongozi hawa wawili basi tuekeeni hapa JF,sio munaleta mambo ambayo hajana kicha wala mguu,huo mkataba mulio andika hapo juu,hata mimi naweza ku draft .

Hata hiyo katiba ya tanzania/tanganyika kuna mambo mengi yameingizwa ya muungano kinyemela na ndio maana muungano umekuwa mbovu na lawama kubwa na unyonyaji zidi ya wazanzibari.
 
Back
Top Bottom