mizambwa
JF-Expert Member
- Oct 8, 2008
- 4,422
- 1,790
Ajali zaua 1,800 nchini
na Mwandishi wetu
JUMLA ya Watanzania 1,800 wamepoteza maisha katika ajali mbalimbali zilizotokea nchini kati ya Januari na Juni mwaka huu.
Kauli hiyo ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Pereira Silima, alipokuwa akikabidhiwa stika za Wiki ya Nenda kwa Usalama zilizotolewa na Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel kwa kushirikiana na Kampuni ya mafuta ya Puma.
Alisema katika katika kipindi hicho zilitokea ajali 11,163 ambazo mbali na kusababisha vifo hivyo, pia zimesababisha watu 9,000 kupata ulemavu wa kudumu.
Kulingana na takwimu hizo, maana yake ni kwamba kila siku watu 10 wanapoteza maisha kwa ajali. Hatuwezi kuruhusu hali hii iendelee.
Nawashukuru wadhamini kwa kampeni ya Wiki ya Nenda kwa Usalama mwaka huu Kampuni ya Airtel na Puma kwa kutoa mchango wao pamoja na kushirikiana na Jeshi la Polisi Usalama Barabarani kufikia malengo kwa kuhakikisha usalama wa raia na kupunguza ajali za barabarani, alisema.
Pamoja na hilo, aliwahimiza watu wanaomiliki vyombo vya moto kwenda kukaguliwa ndani ya wiki hiyo na kwamba wasiofanya hivyo watachukuliwa hatua za kisheria.
Aidha, alisema katika wiki ya maadhimisho hayo watatoa mafunzo maalumu kwa waendesha pikipiki, kwani ajali nyingi zinazotokea zinahusu vyombo hivyo.
Kwa upande wake, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Airtel, Beatrice Singano, alisema kampuni hiyo inajivunia kuwa sehemu ya juhudi za kuokoa maisha ya Watanzania na mali zao.
Naye Mkurugenzi Mkuu wa Puma, Maregesi Manyama, alisema moja ya malengo ya kampuni hiyo ni usalama kazini kwa kutopata ajali, hivyo mchango wao huo utafanikiwa ikiwa utafanikisha kuepusha kifo hata kimoja.
========================================================================================================
Source: Tanzania Daima, Mwananchi tarehe 13/09/2012 Pia Taarifa ya Habari saa mbili usiku ITV tarehe 13/09/2012.
====================================================================================================
MYTAKE: Sasa waandishi wa habari ambao walisema kuwa wanagoma kuandika habari zote zinazohusu jeshi la Polisi, na hususani wiki ya "Usalama Barabarani", wameishia wapi??? kwani habari hii inahusu Wiki ya Usalama barabarani na wanaohusika ni jeshi la Polisi, tena Waziri Nchimbi ameongea, hata jana ITV tumemuona!!!!
Je, kwanini walimfukuza pale jangwani?? au ndio unafiki wetu Watanzania????
Sikutegemea habari zhizi kutoka katika vyombo hivi ningeona katika gazeti Habari Leo, uhuru, Mzalendo au Radio Uhuru, TBC1 hapo nisingelikuwa na la kusema.
Waandishi tuelezeni harakati zenu zimeishia wapi??????
MIZAMBWA
IANNIUMA SANA!!!
na Mwandishi wetu
JUMLA ya Watanzania 1,800 wamepoteza maisha katika ajali mbalimbali zilizotokea nchini kati ya Januari na Juni mwaka huu.
Kauli hiyo ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Pereira Silima, alipokuwa akikabidhiwa stika za Wiki ya Nenda kwa Usalama zilizotolewa na Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel kwa kushirikiana na Kampuni ya mafuta ya Puma.
Alisema katika katika kipindi hicho zilitokea ajali 11,163 ambazo mbali na kusababisha vifo hivyo, pia zimesababisha watu 9,000 kupata ulemavu wa kudumu.
Kulingana na takwimu hizo, maana yake ni kwamba kila siku watu 10 wanapoteza maisha kwa ajali. Hatuwezi kuruhusu hali hii iendelee.
Nawashukuru wadhamini kwa kampeni ya Wiki ya Nenda kwa Usalama mwaka huu Kampuni ya Airtel na Puma kwa kutoa mchango wao pamoja na kushirikiana na Jeshi la Polisi Usalama Barabarani kufikia malengo kwa kuhakikisha usalama wa raia na kupunguza ajali za barabarani, alisema.
Pamoja na hilo, aliwahimiza watu wanaomiliki vyombo vya moto kwenda kukaguliwa ndani ya wiki hiyo na kwamba wasiofanya hivyo watachukuliwa hatua za kisheria.
Aidha, alisema katika wiki ya maadhimisho hayo watatoa mafunzo maalumu kwa waendesha pikipiki, kwani ajali nyingi zinazotokea zinahusu vyombo hivyo.
Kwa upande wake, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Airtel, Beatrice Singano, alisema kampuni hiyo inajivunia kuwa sehemu ya juhudi za kuokoa maisha ya Watanzania na mali zao.
Naye Mkurugenzi Mkuu wa Puma, Maregesi Manyama, alisema moja ya malengo ya kampuni hiyo ni usalama kazini kwa kutopata ajali, hivyo mchango wao huo utafanikiwa ikiwa utafanikisha kuepusha kifo hata kimoja.
========================================================================================================
Source: Tanzania Daima, Mwananchi tarehe 13/09/2012 Pia Taarifa ya Habari saa mbili usiku ITV tarehe 13/09/2012.
====================================================================================================
MYTAKE: Sasa waandishi wa habari ambao walisema kuwa wanagoma kuandika habari zote zinazohusu jeshi la Polisi, na hususani wiki ya "Usalama Barabarani", wameishia wapi??? kwani habari hii inahusu Wiki ya Usalama barabarani na wanaohusika ni jeshi la Polisi, tena Waziri Nchimbi ameongea, hata jana ITV tumemuona!!!!
Je, kwanini walimfukuza pale jangwani?? au ndio unafiki wetu Watanzania????
Sikutegemea habari zhizi kutoka katika vyombo hivi ningeona katika gazeti Habari Leo, uhuru, Mzalendo au Radio Uhuru, TBC1 hapo nisingelikuwa na la kusema.
Waandishi tuelezeni harakati zenu zimeishia wapi??????
MIZAMBWA
IANNIUMA SANA!!!