Huu ndio uliokua Uzi wangu kabla ya kuajiriwa.2015

chichimizi

JF-Expert Member
Jan 17, 2015
1,074
338
Hiii ndio ilikua post yangu kabla ya kupangiwa ajira yangu mwaka 2015.

"My name is Sir Chichi, I will be with you in English and History. I need your cooperation, thenk yuu pwaa pwaaaaa." (makofi) Najua ndo nakoelekea huko! usinishangae!! sijapenda kuanza mazoezi ya kujitambulisha ila ni kwa sababu ya kumbukumbu nilizonazo kuhusu msoto nilioupitia. Ndiyo ni msoto believe me, ukiachana na jinsi nilivosoma shule kwa mbinde kingine ni hii miezi miwili iliyopita imenitesa mpaka sina hamu. We fikiria tu kuwa najifurahisha lakini nakwambia usithubutu kukutana na Bwana tetesi 'No Ajira' au kitu ajira july...weee kichwa kinavurugwa unaweza jikuta una msalimu shikamoo hata mtoto wa miaka minne na nusu.Hiyo miezi iliyopita habari za redioni, magazetini au kwenye tv hazikua habari kwangu mpaka wagusie suala la ajira za ualimu.Nasikia hapo katikati kuna issue za kitaifa kama katiba pendekezwa na suala la mb8 zilijitokeza,! hahahaaa nilikua nazipata lakini ndo nimezielewa juzi mara baada ya kauli ya ajira za wapiganaji wa taifa hili walimu.

Miezi hiyo miwili yan february na Mr March ndiyo iliyofanya hata wale walochaguaga Ilala na Moro Manispaa waseme mbele ya haraiki kuwa mi hata wakinitupa kijijini naenda tena kiroho safi kabisa! duu laiti kama tamisemi wangekua wanajua au kumpitia kila mwl tarajali ndani ya huo mda kupata maoni nadhan ajira zingetoka kama zawadi ya pasaka kwa wapiganaji.Anyway ngoja tuache hayo na kutumia mda huu mfupi kuombea yafuatayo;Walimu wote wapate ajira na pia waliokuwa na matatizo kama carry nao wawemo kwenye list hiyo kama inavokuaga miaka mingine.Kingine ni uzima, afya na kudumishwa kwa ushirikiano baina yetu na jamii kwa ujumla.Mwisho nawatakia kila la kheri wote watakaohusika kwa namna moja ama nyingine kuhakikisha tunafikia ile adhma yetu ya kuajiriwa mfano atakayeweka majina yetu kwenye web ili asiipoteze flash yake yenye majina, watangazaji wote watakaoitangaza hii habari, pia mitandao na Mb8 zao siku hiyo kusiwe na shida ya mtandao bora mtandao usumbue leo mana nimetingwa hapa naandaa TO DO LIST cjui nimesahau nini cha muhimu:

Tar 17-18 kufua nguo na kukusanya madeni

Tar 19 - kuulizia bei ya mahitaji muhimu kama godoro na power bank ya kuchajia simu kule kijijini

Tar 20 - 23 kusalimia ndugu na kupanga nguo kwenye begi

Tar 24 asubuhi kuunga vifurushi kwenye line zangu 2, line moja dkk za kuongea nyingine internet

Tar 25 kufuata cheti chuo

Tar 28 kuaga ndugu na kukata tiketi

Tar 29 kutembelea ofisi za mkurugenzi

Duuh utata utaanzia siku nikifika huko site cjui nitaanzia wapi mana cna hata kijiko cha kuanzia ila all in all mambo yatajipa in the name of Jesus Christ, amen.Walimu wenzangu wish u all da best .
 
Ulisoma ili uajiriwe? Hivi mnalipeleka wapi Taifa?! Yaani badala uwaze jinsi utasaidia wanafunzi waelimike ili wailete Tanzania maendeleo ila wwe unawaza mshahara !!!
 
Back
Top Bottom