Elections 2010 Huu ndio ukweli

mozze

Senior Member
Aug 27, 2010
185
28
Kwanza kabisa Ukweli ni kwamba kura inapigwa kwa siri.

  • Watanzania wengi sasa wanajua upi Ukweli na upi uongo
  • Yaliotendwa na CCM yanajulikana (in black&white), hata hayakuhitaji Spika au Mabango
  • Kura za maoni kwenye mitandao ya magazeti zinadhihirisha kuwa kila mtu ana siri yake ya nani atampigia kura. Maana kwa jinsi CCM wanatumia hela for sure wamewalipa watu hela ili wawapigie kura mtandaoni waone wamekubalika, lakini hawa watu wanapiga kile kilicho nafsini mwao.
  • Na hii itadhihirika pia starehe 31 Oct, maana sio wale wote wanaovaa sare za CCM na kwenda kuangalia CONCERTS wanakubalia na CCM na Mgombea wake.
  • CCM na Kikwete wameshalitambua hili ndio mana Mkuu kaamua kuanza kutumia nguvu kama kuvunja sheria, kutumia familia, mali za serekali na kila kitu kiwezekanacho.
  • Ndio mana nilisema kwenye thread moja, hata CCM wakija na propaganda za Ukabila, au Udini hawataweza kusimamisha MOTO WA MABADILIKO kwa kuwa KURA inapigwa kwa siri na binadamu wote hatuamini kitu kimoja hata kama wote ni Wasukuma, au Wote ni Wapagani.
  • FUATILIA MATOKEO YA KURA ZA KWENYE Mitandao, Magazeti na Blogs ndio Utajua Ukweli!
 
Back
Top Bottom