Huu ndio ufisadi wanaoufanya walimu serikalini. Nao ni majipu, watumbuliwe

Mantombazane

JF-Expert Member
Sep 7, 2014
572
356
Wakati huu ambao Mheshimiwa rais ana fanya kazi ya kutumbua majipu, ni wajibu wetu raia kumsaidia kumuonesha majipu mengine ambayo hayaonekani kwa urahisi. Wizara ya elimu na labda wizara nyingine kuna majipu ambayo yamejificha hayaonekani kutokana na walimu kuwa na malalamiko mengi ya mishahara duni, kucheleweshewa mishara, malimbikizo, mazingira duni ya kazi nk. Pamoja na matatizo yote hayo walimu wengi wanafanya kazi yao kwa bidii na kwa moyo wa hali ya juu kuelimisha taifa hili. Hata hivyo wapo walimu wachache wanaowaachia wenzao mizigo huku wao wakilipwa bila kufanya kazi serikalini. Ufisadi wanaoufanya baadhi ya walimu hao ni huu.

Kuna baaadhi ya walimu ambao wanaomba ruhusa ya kwenda kusoma wakisingizia wamepata vyuo. Wakipewa ruhusa wanakwenda kufanya kazi katika shule za binafsi huku wakipokea mishahara miwili yaani ule wa serikali na ule wa shule binafsi anakofanya kazi huko kwa mwajiri wake akidhaniwa yuko chuoni. Walimu wa aina hii wamezagaa sana mijini hasa Dsm ambako kutokana na umbali kutoka mikoani walikotoka huwa hawagunduliki kiurahasi. Muda wa kozi aliyoomba ukiisha anarudi kituoni na kuongeza miaka mingine akidai anachukua post graduate au masters. Haya yanafanyika sana na ukiwauliza wanakwambia akirudi kazini haulizwi vyeti na asipopeleka hawana shida kwani labda uwe na kimbele mbele cha kupandishwa madaraja au cheo. Sasa kwakuwa wanajua ulikuwa ni uongo wana minya na kutafuta mwanya mwingine wa kutoka.

Haya yote yanatokea kwakuwa hakuna ufuatiliaji wa karibu kujua mwalimu kasajiliwa chuo gani na namba yake ya usajili ili kuona kama kweli anasoma huko aliko. Wakati mwingine haya hufanyika kwa kula njama na wakuu wa shule ambao humegewa kidogo kutoka katika mshahara wa mwl fisadi kila mwezi hivyo kumfichia siri. Nashauri serikali ifanye uchunguzi wa walimu wote walioomba ruhusa ya kwenda kusoma kama kweli wanasoma na ni vyuo gani na kupata uhakika kutoka vyuoni. Wale wote ambao wamerudi waamriwe kuwasilisha vyeti vyao vya kuhitimu ili kujiridhisha kuwa kweli walikuwa vyuoni vinginevyo warudishe mishahara yote waliyolipwa kwa kisingizio cha kuwa vyuoni na kisha kufukuzwa kazi na kushitakiwa kwa udanganyifu. Hili linafanyika sana upande wa sekondari.

Ujanja mwingie wanaotumia walimu ni kuondoka vituoni wakidai wanauguliwa na wazazi wao mbali hivyo huongea na mkuu wa shule ili awekwe dei waka ambaye atakuwa analipwa na mwalimu aliyepo "kuuguza" wakati si kweli wanakuwa wapo shule nyingine wakipiga mzigo. Utashangaa mwalimu anakuwa kuuguza kwa miaka miwli. kwakuwa huku nyuma kaweka dei waka kwa mapatano na mkuu wa shule akilimlipa laki moja kutoka katika mshahara wake wa labda laki 400,000 anabaki na 300,000 akijumlisha labda na ule anaolipwa private wa labda 500,000 anajikuta ana laki 800,000 na zaidi. Haya yanafanyika sana na kuwaathiri watoto wetu mashuleni kwani baadhi ya madei waka huwa hawana uwezo kwa kuwa huwa sio walimu na ni chipu leba.

Kwakuwa serikali sasa ina maafisa elimu sekondari kila wilaya ni vema ikafanya uchunguzi wa walimu wote waliowahi kuomba ruhusa za kwenda kusoma kama kweli walikwenda kwa kuthibisha vyuo walivyokwenda na namba zao za usajili huko na wa wasilishe vyeti vya kuhitimu. Kisha wathibitishe kupitia vyuo hivyo kama ni kweli waliwasajili na kusoma na kisha kuhitimu katika vyuo hivyo. Waliopo vyuoni nao wafuatiliwe kama wako huko kweli vinginevyo watimuliwe ili washitakiwe, warudishe mishahara yote waliyolipwa wakijidai wako vyuoni na kisha wabaki huko private na badala yake serikali iajiri walimu ambao watawajibika ambao wamejaa mitaani.

Jamani dawa ya majipu ni kuyatumbua na siyo kuyakuna. Watu wafanye kazi sio kulipwa wakati hawafanyi kazi.
 
Ngumu kumeza! mm muda wote niko k/koo hapa nafanya vibarua sasa wewe si ukae kmya,nyie si mna semina ngurudoto au zimekatwa umeamua kumwaga mboga baada ya kuminywa?pimbi ww.
 
Sidhani kuwa kinachoitesa Tanzania ni ufisadi wa aina ya hao walimu. Tuna mafisadi wa kuzungumzia wanaoita bil. 1.6 hela za mboga na sio hao walimu wanaohangaika kujikimu kwa mishahara midogo waliyo nayo. Tukibana mafisadi wakubwa hata hao walimu hawatafanya hivyo maana kutakuwa na fedha za kutosha kuwalipa mishahara mizuri. Labda kama una ugomvi binafsi na walimu.
 
Nadhani wewe huelewi maana ya ufisadi.Ungeuelewa wala usingetoa huu uzi.Ukitaka kujua maana ya ufisadi wasiliana na Harbinder Sigh yule Gabachori wa TEGETA ESCROW.Hizo hela unazosema walimu wanapiga ukizijumlisha kwa pamoja kwa miaka 10 hazifikii hata 1/5 anayopiga huyo jamaa kwa mwezi mmoja tu.
 
Kuna Mambo mengi sana ya kuongea.mimi ni ticha na nafanya yoote ayo uliosema...ili nikuze kipato changu..kwa sababu nmesahaulika miaka nenda rudi...

Mwaga mboga nimwage ugali..kazi ni kazi na kila kazi iheshimiwe sasa kama Mbunge analipwa mishahara na.malimbkizo ndani ya wakati alafu mimi silipwi miaka na miaka unategemea niweke pua yangu serikalin pekee??Never!!!

Mbunge ana mshahara Milioni 11.8 kila mwezio(mwalim ana mshahara laki5 na...Mbunge Ana.mkopo wa Gari milion.90 lakini mwalimu hana(na hio milion 90 ya mkopo wa mbunge nusu analipiwa na nusu analipa),,Mbunhr ana Mafao ya milion 238 baada ya miaka mitano(mwalim ni milion.60 baada ya kuhangaika kwa miaka 55_60 kazini)..Mbunge ana posho laki 3 daily ...mwalimu hana.haata sh 100 posho...

Teeh...afu unategemea mwalim ategemee mshahara wa serikalin.pekee??Haipo hioo njoo ww na magufuli wako Ntawatumbua nyie raundi hii!!
 
huna mwelekeo wewe huto ni tujijipu ambato hatuna athari JPM yupo na majipu na MIJIPU
 
Kuna Mambo mengi sana ya kuongea.mimi ni ticha na nafanya yoote ayo uliosema...ili nikuze kipato changu..kwa sababu nmesahaulika miaka nenda rudi...

Mwaga mboga nimwage ugali..kazi ni kazi na kila kazi iheshimiwe sasa kama Mbunge analipwa mishahara na.malimbkizo ndani ya wakati alafu mimi silipwi miaka na miaka unategemea niweke pua yangu serikalin pekee??Never!!!

Mbunge ana mshahara Milioni 11.8 kila mwezio(mwalim ana mshahara laki5 na...Mbunge Ana.mkopo wa Gari milion.90 lakini mwalimu hana(na hio milion 90 ya mkopo wa mbunge nusu analipiwa na nusu analipa),,Mbunhr ana Mafao ya milion 238 baada ya miaka mitano(mwalim ni milion.60 baada ya kuhangaika kwa miaka 55_60 kazini)..Mbunge ana posho laki 3 daily ...mwalimu hana.haata sh 100 posho...

Teeh...afu unategemea mwalim ategemee mshahara wa serikalin.pekee??Haipo hioo njoo ww na magufuli wako Ntawatumbua nyiee sio ninyi kuntumbua mimi!!

Mmmh, mwishoni umenipa kicheko cha moyomoyo. Yaani wewe hutatumbuliwa jipu, bali utawatumbua watumbua majipu. Kazi kwelikweli
 
Labda kama hupeleki matokeo ya kila semester. Ila sehemu nyingine kila semester unasubmit provisional results kwa mwajiri. Lakini hata yote yanasababishwa na "mishahara bikin" wanayopewa walimu. Bora askar atileast wanapewa mishahara njiwa wabunge mishahara pensi nyanya TRA ingawa wanapewa mishahara " mabwanga" ila ndo wapiga dili mbaya. Tuacheni walimu hata mafigusufigusu ya Mh. hayatuadhiri bhana
 
Acha wajiongezee kipato kwani serikali imewasahau hawana pa kukimbilia zaidi ya huko...
 
Una Mahasira Yako Huko Unakuja Kusumbua Walimu Walipe Hela Nzur Na Posho Uone Kama Watayafanya Hayo
 
mshahara wa mwalim haitoshi kununulia sofa set. walimu hawana hata viti vya kukalia mpaka wachangiane ,hii nchi walimu wamepuuzwa
 
Nilichoweza kukihisi hapa wachangiaji wengi jamii forum ni waalimu.!! Na wanasahau 1 na 1 hufanya mbili. Elimu duni kwa watoto wetu inatoa taifa duni LA watu wanaotegemea kuishi kiujanja ujanja. Halafu mnawapigia kelele wezi Wa bandarini. Na TRA. Kumbe wengine mko humu shame on you..
 
Kuna Mambo mengi sana ya kuongea.mimi ni ticha na nafanya yoote ayo uliosema...ili nikuze kipato changu..kwa sababu nmesahaulika miaka nenda rudi...

Mwaga mboga nimwage ugali..kazi ni kazi na kila kazi iheshimiwe sasa kama Mbunge analipwa mishahara na.malimbkizo ndani ya wakati alafu mimi silipwi miaka na miaka unategemea niweke pua yangu serikalin pekee??Never!!!

Mbunge ana mshahara Milioni 11.8 kila mwezio(mwalim ana mshahara laki5 na...Mbunge Ana.mkopo wa Gari milion.90 lakini mwalimu hana(na hio milion 90 ya mkopo wa mbunge nusu analipiwa na nusu analipa),,Mbunhr ana Mafao ya milion 238 baada ya miaka mitano(mwalim ni milion.60 baada ya kuhangaika kwa miaka 55_60 kazini)..Mbunge ana posho laki 3 daily ...mwalimu hana.haata sh 100 posho...

Teeh...afu unategemea mwalim ategemee mshahara wa serikalin.pekee??Haipo hioo njoo ww na magufuli wako Ntawatumbua nyie raundi hii!!

basi tufanye kila baada ya miaka mitano tuwaite wazazi wakupigie kura kama uendelee kufundisha?

Wewe mwalimu umechaguliwa na karani mmoja wa masijala, mbunge kapigiwa kura na watu laki mbili, mbunge kapiga kampeni usiku na mchana tena kachakachua na kura, wewe umesoma jina ubaoni tu unataka ulingane nao utakuwa mjinga tu, wakati watu wanachukua form na kugombea ulikuwa wapi mjinga wa kudumu.

JPM MKM wote walikuwa walimu sasa vigogo wewe upo tu, uza hata papuchi basi nayo huwezi, kenge mkubwa.
 
Nilichoweza kukihisi hapa wachangiaji wengi jamii forum ni waalimu.!! Na wanasahau 1 na 1 hufanya mbili. Elimu duni kwa watoto wetu inatoa taifa duni LA watu wanaotegemea kuishi kiujanja ujanja. Halafu mnawapigia kelele wezi Wa bandarini. Na TRA. Kumbe wengine mko humu shame on you..

Unategemea watu watu waliodunishwa watoe/wazalishe kitu bora?!Fikiri tena kuhusu "ELIMU DUNI"
 
Acha wajiongezee kipato kwani serikali imewasahau hawana pa kukimbilia zaidi ya huko...

walimu wanajionaga wa maana kweli kumbe hovyo tu, kwanza ajira yenyewe umesoma ubaoni hata kuandika maombi ya kazi hawezi, akifukuzwa ataambulia kuwa barmedi tu.
 
walimu wanajionaga wa maana kweli kumbe hovyo tu, kwanza ajira yenyewe umesoma ubaoni hata kuandika maombi ya kazi hawezi, akifukuzwa ataambulia kuwa barmedi tu.

Daah umesema kweli,!! Sijui kama wanalitambua hill nimeenda shule moja huko Sengerema Nina shida aisee!! Kuna waalimu wanadharau mpaka basi.. Nikajikuta hata shida niliyokuwa imeyeyuka ghafla. Dk 20 unamsubiri halafu anakuuliza unasemaje? Akiwa kainama wengine wanaendelea na mambo yao!! Duuh mwalimu.!
 
Kuna Mambo mengi sana ya kuongea.mimi ni ticha na nafanya yoote ayo uliosema...ili nikuze kipato changu..kwa sababu nmesahaulika miaka nenda rudi...

Mwaga mboga nimwage ugali..kazi ni kazi na kila kazi iheshimiwe sasa kama Mbunge analipwa mishahara na.malimbkizo ndani ya wakati alafu mimi silipwi miaka na miaka unategemea niweke pua yangu serikalin pekee??Never!!!

Mbunge ana mshahara Milioni 11.8 kila mwezio(mwalim ana mshahara laki5 na...Mbunge Ana.mkopo wa Gari milion.90 lakini mwalimu hana(na hio milion 90 ya mkopo wa mbunge nusu analipiwa na nusu analipa),,Mbunhr ana Mafao ya milion 238 baada ya miaka mitano(mwalim ni milion.60 baada ya kuhangaika kwa miaka 55_60 kazini)..Mbunge ana posho laki 3 daily ...mwalimu hana.haata sh 100 posho...

Teeh...afu unategemea mwalim ategemee mshahara wa serikalin.pekee??Haipo hioo njoo ww na magufuli wako Ntawatumbua nyie raundi hii!!

mkuu umemchana jamaa bila chenga
kwahiyo kama mbwahi namiwe mbwahi tu
kwani hakuna kuoneana aibu muda huu.
 
Back
Top Bottom