GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,466
- 108,621
Akiwa anaongea ' mubashara ' kabisa sasa hivi kupitia Kipindi cha 360 cha Clouds tv Waziri mpya wa TAMISEMI, Mchezaji mpira / kandanda mzuri tu wa zamani na mtoto wa mjini hasa Seleman Jaffo amesikika akisema ' Kauli ' ambayo ni ya ' Kimkwara ' kabisa kwa Viongozi walio chini yake hasa Wakuu wa Mikoa na Wilaya.
Waziri huyo wa TAMISEMI Jaffo amesema namnukuu..." Nawaomba Wakuu wa Mikoa na Wilaya wote nchi nzima kuhakikisha kuwa katika maeneo yao kunakuwa na Maendeleo makubwa, wasimamie vizuri Sera za Serikali na wawe Wabunifu na zaidi ya hapo hatutaelewana kabisa kwani sitaki ugoigoi chini ya huu Uongozi wangu "...mwisho wa Kumnukuu.
Namalizia kwa swali ' dogo ' tu je haya maneno ya Jaffo yanamuhusu pia / moja kwa moja Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul C. Makonda ambaye ana ushawishi mkubwa Serikalini na kwa ' Taita ' mwenyewe wa Magogoni au inawahusu tu Wakuu wa Mikoa na wa Wilaya wa Mikoa mingineyo?
Na swali pia la ' nyongeza ' hivi ' Kiitifaki ' kati ya RC Makonda na Waziri Jaffo ni nani ana ' Cheo ' kikubwa kuliko mwenzake? Na je ni nani anatakiwa kuaminika haraka / upesi mbele ya ' Taita ' wa Magogoni kama pakiwa na tatizo?
Naamini leo nitapata majibu ' Kuntu ' kabisa hasa kutoka kwa Members wa JF ambao huwa nawaamini siku zote ni Watu Werevu / Vipanga sana na hakuna hata siku moja wamewahi kuniangusha katika kunipa ' ufafanuzi ' wa jambo ambalo huwa nina ' utata ' nalo.
Nawasilisha.
Waziri huyo wa TAMISEMI Jaffo amesema namnukuu..." Nawaomba Wakuu wa Mikoa na Wilaya wote nchi nzima kuhakikisha kuwa katika maeneo yao kunakuwa na Maendeleo makubwa, wasimamie vizuri Sera za Serikali na wawe Wabunifu na zaidi ya hapo hatutaelewana kabisa kwani sitaki ugoigoi chini ya huu Uongozi wangu "...mwisho wa Kumnukuu.
Namalizia kwa swali ' dogo ' tu je haya maneno ya Jaffo yanamuhusu pia / moja kwa moja Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul C. Makonda ambaye ana ushawishi mkubwa Serikalini na kwa ' Taita ' mwenyewe wa Magogoni au inawahusu tu Wakuu wa Mikoa na wa Wilaya wa Mikoa mingineyo?
Na swali pia la ' nyongeza ' hivi ' Kiitifaki ' kati ya RC Makonda na Waziri Jaffo ni nani ana ' Cheo ' kikubwa kuliko mwenzake? Na je ni nani anatakiwa kuaminika haraka / upesi mbele ya ' Taita ' wa Magogoni kama pakiwa na tatizo?
Naamini leo nitapata majibu ' Kuntu ' kabisa hasa kutoka kwa Members wa JF ambao huwa nawaamini siku zote ni Watu Werevu / Vipanga sana na hakuna hata siku moja wamewahi kuniangusha katika kunipa ' ufafanuzi ' wa jambo ambalo huwa nina ' utata ' nalo.
Nawasilisha.