TWisheshagi
Member
- May 2, 2020
- 14
- 209
Chama cha Mapinduzi (CCM) kimehitimisha mchakato wa kupata mgombea wake wa urais kwa upande wa Zanzibar.
Ni Hussen Ali Hassan Mwinyi. Mwanasiasa mtulivu, mkimya na asiyependa kujikweza.
Zipo tetesi kuwa ukimya wa Hussein Mwinyi, unavuka mipaka ya kawaida. Hata kwenye vikao vya Baraza la Mawaziri hakuwa mzungumzaji mzuri.
Kuna nyakati hata alipoombwa kutoa maoni yake aliishi kusema:"Naunga mkono yote yaliokwisha kusemwa na wenzangu" na kisha aliketi.
Tetesi hizi ni vigumu sana kutoziamini kwa sababu zinaeleza tabia halisi ya Hussein Mwinyi. Ukimya wake unaacha maswali mengi kuliko majibu.
Wapo wanaoamini kuwa ukimya wa Hussein siyo Udhaifu wake. Utii wake kwa viongozi wake si Ujuha! Mawazo haya yanaweza kumshawishi yeyote.
Lakini ukweli wa MUNGU, ni hatari sana kumkabidhi madaraka makubwa mtu ambaye misimamo yake haijulikani bayana.
Nimesema ni hatari kumkabidhi "madaraka" si kwa bahati mbaya. Ukweli ni kwamba kwa siasa za Zanzibar, na ukiritimba wa CCM ulivyo, inawezekana kabisa, Hussein Mwinyi ndiye Rais ajaye wa Zanzibar.
Ni ukweli mwingine kuwa, hana ushawishi mkubwa Zanzibar, hana umahiri mkubwa wa siasa za Zanzibar, hajawahi kujipambanua kama mtetezi halisi wa maslahi ya Zanzibar ndani ya Muungano.
Hulka za ukimya wake, zimetunyima fursa wengi ya kujua na kumfuatilia kama mtetezi wa maslahi ya Zanzibar.
Katika hili ninaweza kusema kwa wazi na kujiamini kabisa kuwa, kwa Mara nyingine tena historia imeandikwa kutokea Tanganyika. Nina maana kwamba, Rais wa Zanzibar amechaguliwa kutoka bara(Tanganyika)
Wapo Wan zanzibar wanaoupenda sana Muungano, lakini daima huchukizwa sana na tabia ya dola la Tanganyika kuwachagulia Rais wao.
Watu wenye hisia kama hizi bado wapo zanzibar! Wanaupenda Muungano wetu, lakini hawapendi namna tunavyoishi nao ndani ya Muungano. Hawa wamekubali kuishi katika hali wasiyoweza kuibadili.
Hulka ya Wan zanzibar wengi ni kupenda kwanza Zanzibar kabla ya kupenda Muungano! Kwao mtu mwenye kutetea Zanzibar kwanza ni bora zaidi kuliko yule anayetetea Muungano kwanza.
Sifa hii haipo kwa Hussein Mwinyi. Sifa hii anayo Maalim Seif Sharrif. Maalim Seif amekuwa kipenzi cha Wan zanzibar kwa muda wote kwa sababu ameweza kusoma hisia zao.
Seif Sharrif, anajua Wan zanzibar wa napenda kusikia kitu gani. Kama kuna jambo linalowaunganisha Wanzibar wote popote walipo Duniani ni Uhuru wao na maslahi ya Zanzibar. Maalim Seif amekuwa wazi mno katika hili, ndio maana hachuji katika siasa za Zanzibar.
Wapo wana-CCM wanakubaliana na hilo. Tofauti pekee ni kuwa wao hawasemi hadharani. Wengi hutumia majina bandia kwenye mitandao ya kijamii kutapika nyongo zao ili wapate usingizi.
Hulka hiyo haipo kwa Hussein Mwinyi. Sioni kwa namna gani anaweza kuwaaminisha Wazanzibari kuwa anaweza kutetea maslahi yao japo kwa bahati mbaya.
Ninaona turufu ya wazi kwa Maalim Seif Sharrif Hamad. Hussen Mwinyi, atashinda Uchaguzi, Maalim Seif Hamad, atashinda kura na Mzee Jecha, atazihesabu kura tena.
Ndimi Mkulima wa Miwa, Bonde la Mto Simiyu- Magu-Mwanza
Ni Hussen Ali Hassan Mwinyi. Mwanasiasa mtulivu, mkimya na asiyependa kujikweza.
Zipo tetesi kuwa ukimya wa Hussein Mwinyi, unavuka mipaka ya kawaida. Hata kwenye vikao vya Baraza la Mawaziri hakuwa mzungumzaji mzuri.
Kuna nyakati hata alipoombwa kutoa maoni yake aliishi kusema:"Naunga mkono yote yaliokwisha kusemwa na wenzangu" na kisha aliketi.
Tetesi hizi ni vigumu sana kutoziamini kwa sababu zinaeleza tabia halisi ya Hussein Mwinyi. Ukimya wake unaacha maswali mengi kuliko majibu.
Wapo wanaoamini kuwa ukimya wa Hussein siyo Udhaifu wake. Utii wake kwa viongozi wake si Ujuha! Mawazo haya yanaweza kumshawishi yeyote.
Lakini ukweli wa MUNGU, ni hatari sana kumkabidhi madaraka makubwa mtu ambaye misimamo yake haijulikani bayana.
Nimesema ni hatari kumkabidhi "madaraka" si kwa bahati mbaya. Ukweli ni kwamba kwa siasa za Zanzibar, na ukiritimba wa CCM ulivyo, inawezekana kabisa, Hussein Mwinyi ndiye Rais ajaye wa Zanzibar.
Ni ukweli mwingine kuwa, hana ushawishi mkubwa Zanzibar, hana umahiri mkubwa wa siasa za Zanzibar, hajawahi kujipambanua kama mtetezi halisi wa maslahi ya Zanzibar ndani ya Muungano.
Hulka za ukimya wake, zimetunyima fursa wengi ya kujua na kumfuatilia kama mtetezi wa maslahi ya Zanzibar.
Katika hili ninaweza kusema kwa wazi na kujiamini kabisa kuwa, kwa Mara nyingine tena historia imeandikwa kutokea Tanganyika. Nina maana kwamba, Rais wa Zanzibar amechaguliwa kutoka bara(Tanganyika)
Wapo Wan zanzibar wanaoupenda sana Muungano, lakini daima huchukizwa sana na tabia ya dola la Tanganyika kuwachagulia Rais wao.
Watu wenye hisia kama hizi bado wapo zanzibar! Wanaupenda Muungano wetu, lakini hawapendi namna tunavyoishi nao ndani ya Muungano. Hawa wamekubali kuishi katika hali wasiyoweza kuibadili.
Hulka ya Wan zanzibar wengi ni kupenda kwanza Zanzibar kabla ya kupenda Muungano! Kwao mtu mwenye kutetea Zanzibar kwanza ni bora zaidi kuliko yule anayetetea Muungano kwanza.
Sifa hii haipo kwa Hussein Mwinyi. Sifa hii anayo Maalim Seif Sharrif. Maalim Seif amekuwa kipenzi cha Wan zanzibar kwa muda wote kwa sababu ameweza kusoma hisia zao.
Seif Sharrif, anajua Wan zanzibar wa napenda kusikia kitu gani. Kama kuna jambo linalowaunganisha Wanzibar wote popote walipo Duniani ni Uhuru wao na maslahi ya Zanzibar. Maalim Seif amekuwa wazi mno katika hili, ndio maana hachuji katika siasa za Zanzibar.
Wapo wana-CCM wanakubaliana na hilo. Tofauti pekee ni kuwa wao hawasemi hadharani. Wengi hutumia majina bandia kwenye mitandao ya kijamii kutapika nyongo zao ili wapate usingizi.
Hulka hiyo haipo kwa Hussein Mwinyi. Sioni kwa namna gani anaweza kuwaaminisha Wazanzibari kuwa anaweza kutetea maslahi yao japo kwa bahati mbaya.
Ninaona turufu ya wazi kwa Maalim Seif Sharrif Hamad. Hussen Mwinyi, atashinda Uchaguzi, Maalim Seif Hamad, atashinda kura na Mzee Jecha, atazihesabu kura tena.
Ndimi Mkulima wa Miwa, Bonde la Mto Simiyu- Magu-Mwanza