Hupi muda wa kuachama na mke au mme wako kisheria

Ndugu Ngilenengo1, nnachojua ni kwamba Mahakama inaangalia joint efforts katika upatikanaji wa mali, na mchango(effort) sio lazima uwe wa moja kwa moja. Rejea maamuzi ya Mahakama kwenye kesi ya Bi Hawa Mohamed.
 
asante kwa ufafanuzi mzuri mkuu.

Kuna wakati mke au mke wanatengana kwa muda hata miaka 2 au 3, then, ndo wanaamua kupeana talaka baada ya kipindi hicho. swali: mali wanayochuma wakati hawapo pamoja inakuwaje! Nayo wanagawana?. Kama nyumba ilikuwa haijapauliwa, mke akajitenga akamwacha mme akamalizia nyumba na kufanya finishing zote, inachukuliwaje kimahakama?

Mkuu, inshort labda unaongelea suala la lawful separation kwa maana hapa mahakama au kanisa na wazazi wameridhia mtengane kwa muda, hiyo hukubalika na wakati huo wa kutengana kila mtu anaweza kufanya lolote hata ukitaka kuwa na mpenzi wa kukuridhisha hakuna tabu ila kumbuka yaweza kukufanya uivunje ndoa yako kirahisi na wakati huo mkitengana huwezi kusema yule ni mkeo au mumeo umemfumania, itakucost. Hapa kuna kesi nyingi zimewahi kutokea, wanandoa wametengana then akimkuta mwenza wake maeneo analeta fujo kuwa ni mke au meme wake. Elewa kuwa mkitengana hata haki ya unyumba inasimama so usije ukaenda kumlazimisha kufanya tendo la ndoa wakati mmetengana kisheria, utakuwa umefanya kosa la ubakaji, hiyo ni tofauti mkiwa hamjatengana hakuna ubakaji mkiwa pamoja kwenye ndoa.
 
Suala la kufanya finishing ya nyumba mliyoanza kuijenga pamoja na baadae mkatengana lipo wazi kama nilivyosema hapo juu. Kama amechangia kuijenga kwa namna yeyote bado itaeleweka kuwa joint effort, kumbuka hiyo nyumba mlianza kuijenga wakati mpo pamoja, mahakama inaweza kutoangalia mchango wake katika hiyo nyumba baada ya kutengana, lakini kumbuka kuwa kuna mchango aliutoa wakati mpo pamoja kabla ya kutengana. Ila kama kuna mali ameipata wakati mmetengana na haina uhusiano na effort zenu wakati mpo pamoja itakuwa yake pindi mtakapoamua kutengua ndoa, ila itabidi ushahidi mzito uletwe kwa atakaedai hiyo mali iliyopatikana wakati mmtengana.
Ni dhahiri kuwa wakati mmekubaliana kutengana kabla ya kuamua kutengua ndoa mkawa kuna pesa au biashara ya pamoja au akaunti ya pamoja, kama atapata mali kwa kutumia mapato yoyote mliyojipa ia wakati mpo pamoja kwa namna moja au nyingine kama itadhihirika hivyo basi hiyo mali yaweza kuwekwa kwenye mgawanyo. Right?
Kuna mali itakayopatikana wakati mmetengana may be kutokana na biashara aliyoanzisha baada au kutokana na mshahara wake na kadhalika, hiyo ifahamike haitakuwa mali iliyopatikana kutokana na joint efforts, na haitahesabika kuwa matrimonial property which is subject to division upon dissolution of a marriage.
 
Ndio maana huwa nawashangaa wale wanandoa anapata mali wakati yupo kwenye ndoa halali au anaishi kinyumba na mwenza halafu anajisifu kuwa kila mali ameandika jina lake, fahamu kuwa mkishaamua kuishi kama wanandoa, hakuna kinachokuwa cha kwako bali ni vyenu wote wawili, tena kwa wale wanaofuata mohameddan laws wanatakiwa kuwa makini kwani kwa Tanzania, any law inayoleta upinzani kwenye marriage Act, basi the Act will prevail hapo ni panahitaji ufafanuzi mkubwa ila haizuii sheria za kidini.
Suala la mgawanyo wa mali na custody of children huwa ndio linaleta utata mkubwa na ubishani haswa baada ya mahakama kuridhia kutengua ndoa.
Wanandoa mnapoamua kupelekana mahakamani ni muhimu kufahamu matokeo yake, sheria inamsemo @THE COURT IS NOT YOUR MOTHER'.
 
Mkiamua kutengana tu,bila kwenda mahakamani.Mtaendelea kutambulika kama wanandoa?Hata kama kila mmoja anaishi na mwenzi mwingine na labda alishazaa huko na mwenzi alienae.
 
Mkiamua kutengana tu,bila kwenda mahakamani.Mtaendelea kutambulika kama wanandoa?Hata kama kila mmoja anaishi na mwenzi mwingine na labda alishazaa huko na mwenzi alienae.

Sheria haitatambua kama mmetengana kwa hiyo itakuwa ngumu kupata ushahidi kama mlikuwa mmetengana, kwani hujui ni wanandoa wangapi wanakuwa wametengana ether hawalali kitanda kimoja au chumba au hata nyumba ila huwezi kujua.
Kwa hiyo lawful separation ni ile inayofikiwa na baraza la usuluhisho kama kikan cha ukoo, kanisa, msikiti au mahakama. Makubaliano yenu wawili ya kutengana nani atakuwa ameyashuhudia?
Kumbuka sheria imekwisha ainisha hivyo ili kupata ushahidi madhubuti kuwa mmetengana rasmi that is why yamewekwa vyombo vya heshima kushmamia hilo ili kutoa heshima kwa utengano wenu. Kumbuka hata ukiomba talaka, mahakama inaweza kuwapa amri ya kutengana kwanza kwa muda ili mfikirie upya uamuzi wenu wa kuachana then baada ya hapo itawasikiliza kama bado mnataka kupeana talaka.
 
kama mmoja ameamua kutengana na ukaenda kuishi na mwanamke au mwanaume mwingine bado kuna tatizo hapo tena kubwa.
Kama umeamua kuachanana mwenza kwa nini msiende kuomba talaka mahakamani ili muwe huru?
Ndoa ya kwanza ya kikristo haiwezi kupotea kwa kuwepo ndoa ya pili. Kumbuka mtakuwa bado mnatambulika kisheria inakuwa bado hamjafuta kiapo.
Tena mmoja mwenzio anaweza kuwageuka na kuwapeleka mahakamani kuwadai fidia ya ugoni.
Nenda ukaitengue ndoa yenu ili uwe huru na huyo mpenzi wako.
 
Kisheria hakuna muda maalum wa kuachana, hata dakika tano baada ya kufunga ndoa mwaweza kuachana. Ila ni lazima kuwe na sababu za msingi zilizoainishwa kisheria kama kutelekeza, uzinzi na ukatili. Hayo yanaufafanuzi wake. Kuna sababu nyingine zinazoandamana na hizo kama hamjafanya tendo la ndoa baada ya ndoa, ugonjwa usiopona ambao unasababisha kutofanya unyumba na pia kama umegundua ni maharimu na mlikuwa hamfahamu.

Ndugu, ni kweli lakini kulingana na Sheria ya Ndoa ya Tanzania, mahakama ndio chombo chenye mamlaka ya kusema kuwa ndoa imevunjika, na kabla ya miaka miwili ya ndoa huwezi kufungua shauri la divorce mpaka upate ruhusa ya mahakama. Unaweza kuruhusiwa kufungua shauri la divorce kabla ya huo muda kama kuna exceptional hardship.
 
Ndugu, ni kweli lakini kulingana na Sheria ya Ndoa ya Tanzania, mahakama ndio chombo chenye mamlaka ya kusema kuwa ndoa imevunjika, na kabla ya miaka miwili ya ndoa huwezi kufungua shauri la divorce mpaka upate ruhusa ya mahakama. Unaweza kuruhusiwa kufungua shauri la divorce kabla ya huo muda kama kuna exceptional hardship.

Nadhani hiyo requirement ya miaka miwili upo sawa but otherwise hiyo exception ndiyo nilibase zaidi argument yangu, thanks for the point of addition.
 
Ndugu, ni kweli lakini kulingana na Sheria ya Ndoa ya Tanzania, mahakama ndio chombo chenye mamlaka ya kusema kuwa ndoa imevunjika, na kabla ya miaka miwili ya ndoa huwezi kufungua shauri la divorce mpaka upate ruhusa ya mahakama. Unaweza kuruhusiwa kufungua shauri la divorce kabla ya huo muda kama kuna exceptional hardship.

Nadhani hiyo requirement ya miaka miwili upo sawa but otherwise hiyo exception ndiyo nilibase zaidi argument yangu, thanks for the point of addition.
Kuvunja ndoa ni mahakama pekee naamini hayo niliyaweka wazi pia but mchango wako ni wamuhimu ndugu.
 
Tuko pamoja ndugu Bondpost, lakini kuna jambo lingine linanitatiza. Vipi kuhusu talaka tatu? Kwani hizi nazo mpaka ziende mahakamani au nikimtwanga mwenzangu inatosha? Sijaziona kwenye Sheria ya Ndoa.
 
Tuko pamoja ndugu Bondpost, lakini kuna jambo lingine linanitatiza. Vipi kuhusu talaka tatu? Kwani hizi nazo mpaka ziende mahakamani au nikimtwanga mwenzangu inatosha? Sijaziona kwenye Sheria ya Ndoa.

Talaka tatu ni moja ya viashirio kuwa the marriage has broken irretrievable kwa maana hiyo ni lazima mahakama ndio itamke kutengua ndoa. Kumbuka ni amri ya mahakama pekee ndio yenye uwezo wa kutengua ndoa. Talaka tatu ni kwa mujibu wa mohammedan laws.
 
Back
Top Bottom