Huolewi kamwe

Ph-25

JF-Expert Member
Nov 19, 2012
1,159
537
Mwanamke unaolewa,hujui kupika,yani unapika mchuzi wenye ladha ya
machozi,alafu unajichekesha chekesha tu,wengine wavivu hata kupika hawataki ye kila saa simu tu utadhani anafanya biashara ya unga.

Unakuta mtu ameolewa hana mwezi anataka house girl,huo ni uvivu na unapoelekea ni kubaya wanawake wengine unaolewa alafu unakuwa
mchafu mchafu tu, hujui kupendeza, unavaa magauni yako ambayo hayashiki pasi,yani unaenda kumsevia mmeo chakula ila unakuta umekanyaga maugali huko mguuni haueleweki yani mpaka anaona kinyaa aisee..

Au umejimekapua mpaka umekuwa kama mdoli,makucha marefu kama shumileta kila saa umenuna utadhani askari wa ibilisi.Mwanamke umeolewa ila kila siku mmeo anaondoka kwenda kazini we umelala,nguo ya kuvaa ananyooshewa na dada wa kazi.

Hujui kavaa nini,hujamkiss wakati anaenda kazini,akifika ofisini wadada anaofanya nao kazi ndo wanamchana nywele na kumtengeneza tai lazima uachike tu. Humwambii sweet words,unajiweka kizee zee,unasingizia wokovuacha ushamba my precious sister.

Mumeo akiwa kazini hukumbuki hata kumtext,weunamtumia tu maneno ya fumbo ,utadhani mke mwenzio, we mume wako humuiti sweet names, kama honey,darling n.k.Unamuita sijui baba Aziza,sijui baba kambi au unamwita "we mwanaume",aisee wewelazima ndoa yako iwe na majaribu sana.

Lovely sisters, hujui kupika mpaka leo jifunze sasa hivi maana unazeeka na utatutia aibu, A good wife must be positiveminded, uwe unafikiria maendeleo ,usiwe kiwavi,unafikiria kula tu. precious sisters,kupendeza sio dhambi,ilimradi hujavaa nguo za aibu.

★ Mie mke wangu nitamnunulia nguo nzuri nzuri sana tena zakutosha ila asipozivaa,akav aa ma old school yake sitembei nae njiani,yani hata mtaani sipiti nae.Wewe mwanamke lazima ujue kupendeza.kumwambia mumeo maneno mazuri na kumuita majina mazuri sio dhambi.

Achakumuita mumeo majina yasiyoeleweka,Mke mzuri anajali na kutunza familiapamoja na mume wake.Sio kununa nuna tuuu utadhani askari wamotoni,unasingizia kwamba mapenzi nirohoni, lazima laughter moments ziwepo za kutosha.Precious people of God, ndoa ni baraka, you must enjoy it ni ibada, tena holy devotion, you must respect it.

Ndoa ni neema, usiichezee.
 
AHahahahahah khaaa!!!! umetuvulia uvivu leo,,,,, haya tumekuelewa asante kwa funzo.
 
Mungu akikuandikia jambo hata iweje itakuwa tu, wacheni maneno za kukariri.
 
umegusa penyewe! ila mtoe hela za chakula na mazazi mchangie sio tubadilishe daily kwa hela ya hirani au?
 
Mungu akikuandikia jambo hata iweje itakuwa tu, wacheni maneno za kukariri.
wacha kumsingizia mungu kwa tabia na upuuzi wako, mungu hausiki na kumpangia binadam shida wala matatizo, labda mungu wako huyo ndie anapanga, flan ateseke, mwingine ale good life, mwingine aolewe mwingine aendelee kua mchepuko, huyo mungu wa kipuuzi sana uyo, ila nae muabudu mimi hana izo tabia. na anaimiza binadam tufanye kazi tena kwa bidii sana sio mchezo mchezo.
 
Mwenye masikio na asikie na mwenye macho ...................
Well said mkuuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom