Humphrey Polepole: Tusiwatukane wapinzani

Umenitoa Gizani

JF-Expert Member
Dec 3, 2016
387
179
Ukiwatukana mitandaoni haileti faida yoyote waache mwenyewe matendo yao yataonesha kama wao ni nyumbu au la.

WanaCCM tujenge hoja tupunguze fitna unafiki tuongeze kiwango cha kusema kweli tutaaminiwa.

CCM si ya kutukana watu maana CCM wa sasa atambulike kwa utu na ustaarabu wake, akitukanwa aseme asante sio awe bomba la lugha chafu.
 
Hivi nyumbu si ndio wale wanamfuata mwenzao mmoja anapoelekea bila kuulizia? OK basi kwa mantiki hii wana siasa na wafuasi wao kwa ujumla ni NYUMBU..maana maamuzi ya Chama huwa hayahojiwi. Iwe ni CDM au sisi wa Tawala mambo yetu hayo hayo. Maana sijaona hata mwanachama mmoja anampinga Mwenyekiti akitamka kitu. Ukiwa katika siasa wote ni nyumbu
 
Hakuna Ccm ya hivyo tena hakuna siasa ya hivyo Tanzania..
 
Huu ushauri aanze kumwambia aliyetuita wapinzani 'malofa na wapumbavu'
 
We jamaa umeuanza mwaka Kwa kuropoka.mkitaka kuamini angalieni michango yake kwenye threads mbali mbali m confirm ninachosema.punguza utoto/umuch know/pombe/dhambi
Kabla hata hajachangia nilitaka kumtaja, yaani kabla sijaandika akafanya yake kama kawaida yake. Binafsi simchukii Lupyee kwani bado natafiti ni mtu gani yeye ambaye kila uzi unaoanzishwa lazima achangie kwa matusi. Nikishamfahamu wala sitampa adhabu. Lkn nadhani watu kama hawa ndo msemaji wao amewatolea mfano wa matusi. Pia sishangai kwa sababu mtindo wa kupewa vyeo baada ya kutukana watu lazima uzalishe watu kama hawa.
 
Watumishi stahiki zao wamelipwa, malimbikizo yao na madai?
2020 is coming,
Tunataka tume huru ya uchaguzi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom