The Genius
JF-Expert Member
- May 29, 2018
- 820
- 2,070
Katibu Mwenezi wa CCM, Hamfrey Polepole amesema mwisho wa dunia ni mwaka 2042. Akizungumza katika kipindi cha Sunday Worship cha WasafiTV amesema Yesu atarudi mwaka 2035 kulichukua kanisa (wateule wake) na kukaa nao mawinguni kwa miaka 7 hadi mwaka 2042 atakaposhuka kuihukumu dunia.
Lakini katika kipindi cha miaka 7 (2035-2042) kutakua na dhiki kuu duniani ambapo nzige wenye vichwa vya simba na mikia ya nge watawatesa waliobaki duniani. Ndicho kipindi ambacho Mpinga Kristo atajiinua na chapa yake ya 666 na kuiteka dunia.
Alipoulizwa mbona Yesu mwenyewe alisema hakuna ajuaye siku wala saa isipokua Mungu mwenyewe (Marko 13:32) amesema ninkweli siku na saa havijulikani lakini majira na mwaka wa Yesu kurudi vinajulikana.
Nini maoni yako?
Lakini katika kipindi cha miaka 7 (2035-2042) kutakua na dhiki kuu duniani ambapo nzige wenye vichwa vya simba na mikia ya nge watawatesa waliobaki duniani. Ndicho kipindi ambacho Mpinga Kristo atajiinua na chapa yake ya 666 na kuiteka dunia.
Alipoulizwa mbona Yesu mwenyewe alisema hakuna ajuaye siku wala saa isipokua Mungu mwenyewe (Marko 13:32) amesema ninkweli siku na saa havijulikani lakini majira na mwaka wa Yesu kurudi vinajulikana.
Nini maoni yako?