Bado sina taarifa za kutosha juu ya nini kiliendelea nyuma ya pazia juu ya muafaka wa Arusha uliopelekea kufukuzwa uanachama madiwani watano wa CHADEMA. Jambo moja, hata kama chama kilikosea, binafsi ningekuwa mmoja wa hawa madiwani bado ningetekeleza agizo la kamati kuu kwa sababu kutunishiana misuli na kamati kuu hakukinufaishi chama. Ningetafuta venue nyingine baadaye kuwaeleza viongozi wangu wakuu jinsi walivyopotoka katika suala zima. Hii ni kwasababu kuitunishia misuli kamati kuu ambayo ni kikao kikuu cha chama hakunufaishi chama, zaidi inawanufaisha wapinzani wa chama. Mtu yeyote mwenye mapenzi ya kweli na chama angekiweka chama mbele na si yeye binafsi.
Whether walikuwa na haki au walikosea jambo moja ambalo nina uhakika nalo HAWANA MAPENZI NA CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO, wao na malengo yao binafsi wamedhani ni bora kuliko chama.
Hatuhitaji viongozi wa aina hii, waondoke kuna vyama vingi tu vinawafaa, ila si CHADEMA.
CCM, these are your potential members!
Whether walikuwa na haki au walikosea jambo moja ambalo nina uhakika nalo HAWANA MAPENZI NA CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO, wao na malengo yao binafsi wamedhani ni bora kuliko chama.
Hatuhitaji viongozi wa aina hii, waondoke kuna vyama vingi tu vinawafaa, ila si CHADEMA.
CCM, these are your potential members!