Hukumu ya Mapenzi

Ryan The King

JF-Expert Member
Oct 6, 2016
2,788
2,688
Nyota pekee ndizo ziliweza kushuhudia uzuri wa tukio lile zuri lakupendeza. Tukio ambalo dunia nzima ilikuwa imelala kutokana na uchovu wa mchana.

Wakati wengine wakiwa fofofo. Michaelray na Rukaya walikuwa katika mapenzi mazito sana. Wawili hawa walikuwa katika Bustani nzuri. Miti na maua ndivyo viliweza kuona mchezo huu wenye kutamanika. Sauti za wadudu ndizo ziligeuka ala nzuri na yenye kuvutia kwa wapenzi hawa. Ulikuwa Uhondo Usiosemeka.

Rukaya ni mtoto Mrembo sana. Umbile lake lenye urefu wa futi sita ulimfanya azidi kuonekana wa kuvutia. Rangi yake ya nyeupe kiasi yenye vidoti kadhaa vya rangi nyeusi vilizidi kumpamba Mrembo huyu. Ilikuwa ni bahati kubwa sana kwa mwanaume yoyote kumpata mwanamke Mrembo kama Rukaya.

Ilikuwa ni siku ya kwanza ya Rukaya kufanya mapenzi. Kama wanawake wengi waogopavyo kufanya mapenzi siku ya kwanza kwa kuhofia maumivu basi ndivyo Jambo hili pia lilimkuta Rukaya. Rukaya aliogopa sana.

Lakini Utundu wa Michaelray uliyeyusha woga wote wa Rukaya. Michael alitumia mbinu azijuazo ambazo huenda yeye pekee dunia nzima ndio anazo.

Ufundi huu ndio ulizidisha miguno ya mahaba na kufanya eneo zima la bustani kuwa na sauti zenye akapera nzuri sana. Akapera ya sauti ya miguno ya Rukaya pamoja na sauti ya wadudu wa Usiku.

Walimaliza kupeana mambo moto moto na kila mmoja alimshukuru mwenzake. Ilikuwa umefika muda wa Rukaya kurudi nyumbani. Michaelray alimsihi Rukaya kulala usiku ule ili ikifika asubuhi ndio aondoke.

Rukaya alikataa kata kata. Alisema kuwa endapo Baba yake ambaye ni JPM akijua analala nje ya Hostel anaweza kumuua. Michael alivyosikia hivyo alikosa chaguo. Alimruhusu kwa moyo Mweupe kwa mabusu kemkem.

Walitoka mpaka Getini. Na kupeana denda wakiwa nje ya Geti. Ilikuwa yapata saa nane za usiku.

Wakiwa wamekumbatiana huku ndimi zao zikichezeana. Michaelray alishangaa kuona damu zinammwagikia mdomoni. Pia alishangaa kuona Rukaya anamuelemea kwa uzito na Ulimi wake hauchezi tena.

Michaelray alisitisha zoezi la denda na kumshika Rukaya aliyekuwa kafumba macho akiwa amelowa damu kichwa kizima.

Michaelray aliogopa. Alijiuliza nini kimempata Rukaya. Rukaya alikuwa wabaridi sana. Alimlaza chini na kummulika na simu kuona damu inapotoka. Alishtuka kuona shimo kubwa linalovuja damu nyuma ya kichwa.Alimtazama Rukaya aliyekuwa amelala akiwa hapumui kabisa. Alijaribu kugusa mapigo ya moyo wa Rukaya na kugundua hayapigi. Ndipo alipogundua Rukaya amekufa.

Aliita kwa Sauti ya kutokuamini kile kinachotokea. Alijiona katika Mkosi. Ni kweli alikuwa katika Mkosi, katika Shimo la Matatizo. Moyoni alijuta kumuita Rukaya nyumbani kwake.

Kwa mbali taa ya gari ilimulika ikiwa inakuja. Michael aliona hatari ya kuhusishwa na mauaji. Alifikiri kwa haraka afanye kitu gani. Hakutaka kusikia habari za kwenda kufia jela achilia mbali kutembelea wafungwa.

Wazo pekee la kumbia ndilo liliibuka na ushindi katika kichwa cha Michael.
Aliutazama mwili wa Rukaya na kusema;
"Sorry Mpenzi kwa kukuacha hapa. Umeniacha nikiwa bado nakupenda. I love you Rukaya"

Tayari gari lilikuwa limekaribia kabisa. Michael hakutaka kuonekana na wale waliokuwamo ndani ya gari Aliingia ndani ya Geti.

Itaendelea....
 
Wakati wewe unatoa bikra ya Rukaya mm niko natafuta bao la saba na mtoto mzuri Jf nzima Kapeace huku yy akiwa nimeshamkojoza kama mara 18..



Kwa kiganja bafuni lkn..
Ni kusema bikra ya Rukaya imeungana na kichogo ndo maana imetolewa chini damu zimetoka kichwani au sijafahamu wakuuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom