Eeka Mangi
JF-Expert Member
- Jul 27, 2008
- 3,173
- 481
Hatimaye hukumu ya Chenge itasomwa tarehe 16 Desemba 2010. Hivi tutarajie huyu jamaa akipelekwa Segerea kutumikia adhabu ama itakuwa makosa yalikuwa ya marehemu?
wapendwa,
usiku wa kuamkia leo kuna jamaa kamchinja mama yake kama kuku kisha akawachinja kwa style hiyo hiyo watoto wake wawili wa kuwazaa. Tukio hili la kusikitisha lilitokea jana usiku wa saa 2:00-4:00 katika kijiji cha Kokirie huko Mamba wilaya ya Moshi Vijijini. Nimeshuhudia maiti hizi kwa kweli zinasikitisha hasa ukiangalia watoto wale wa miaka 9 na 12 walivyochinjwa kama kuku. Bahati mbaya ama nzuri wananchi wenye hasira nao wamemuua huyo jamaa na kisha kuchoma moto maiti yake. Japokuwa inaelezwa huyu jamaa huenda akili zimemruka lakini amekufa na siri ya kiini cha mauaji haya. Mungu azilaze roho za marehemu mahali pema peponi,Amen