Hukumu kesi iliyofunguliwa na DC mstaafu, Dahn Makanga dhidi ya Mathew Mollel yakwama kusomwa leo

buswelu moja

JF-Expert Member
Aug 24, 2014
226
147
MAHAKAMA ya hakimu mkazi Arusha leo imehairisha kusoma hukumu ya kesi iliyofunguliwa na mkuu wa wilaya mstaafu nchini,Dahn Makanga dhidi ya Mathew Mollel ambaye ni mkazi wa jijini Arusha.

Hukumu ya kesi hiyo ilikuwa inatarajiwa kusomwa leo mnamo Novemba 14 mwaka huu na hakimu mkazi wa mahakama hiyo, Gwantwa Mwankuga baada ya upande wa mashtaka na utetezi kufunga ushahidi wao.

Akitangaza kuharisha kusoma hukumu hiyo hakimu Gantwa alisema kwamba amehairisha kusoma hukumu hiyo kutokana na sababu mbalimbali ambazo hakuzitaja hadharani.

Mara baada ya kutangaza uamuzi huo ndipo aliposema ya kwamba amefanya hairisho fupi kutangaza hukumu hivyo na kupanga kuisoma ifikapo Novemba 24 mwaka huu.

MY TAKE:

Haijajulikana mpaka sasa ni kwanini Hakimu Gantwa amehairisha kutangaza hukumu hiyo kwa kuwa hizo sababu hajaziweka hadharani.

Leo mahakamani watu walikuwa wamefurika hakika wengi wakisubiri kusikia hukumu hiyo kwa hamu kwa kuwa kesi hiyo imejizolea umaarufu na kuvuta hisia za watu hapa Arusha kutokana na kwamba mlalamikaji na mlalamikiwa wana nasaba na wameoa nyumba moja kwani mlalamikaji ameoa dada mtu na mlalamikiwa ameoa mdogo mtu.

Tukutane ijumaa ijayo nitawajuza nini kimejiri mahakamani stay tuned
 
Kesi inahusu nini?umeandika kama upo Arusha forum wote wanafahamu hiyo kesi
 
mkuu du hii sasa ni shidaa kwa nini walioweyana ilikuwa kulipiziana kisasi au kuimarisha undugu? yaani hii ndiyo inaitwa Civil war
 
mkuu du hii sasa ni shidaa kwa nini walioweyana ilikuwa kulipiziana kisasi au kuimarisha undugu? yaani hii ndiyo inaitwa Civil war
Wewe Akili Unazo lakini hutaki kizitumia sijui kwa nini? Kwani kuoa familia moja kuna ubaya gani? Yaani kwa mfano wewe na dada yako mwolewe na wanaume tofauti, ndicho hicho mleta mada alichosema. Kwamba Danhi Makanga na huyo Mollel wameoa familia moja!!
 
Kesi inahusu nini kwani?
Nakumbuka kulikuwaga na ugomvi wa shamba/kiwanja kule Burka nafikri itakuwa hiyo kesi ya kutaka kudhulumiana wanandugu! Inavyosemekana wqkati Makanga akiwa kwenye siasa alimtumia huyo Mme mwenzie kumnunulia hilo shamba sasa M-Arusha akaingia tamaa akataka amdhulumu jamaa yake!
 
Nakumbuka kulikuwaga na ugomvi wa shamba/kiwanja kule Burka nafikri itakuwa hiyo kesi ya kutaka kudhulumiana wanandugu! Inavyosemekana wqkati Makanga akiwa kwenye siasa alimtumia huyo Mme mwenzie kumnunulia hilo shamba sasa M-Arusha akaingia tamaa akataka amdhulumu jamaa yake!
Kazi ipo
 
Back
Top Bottom