Huku wakiwa wameyafungia Maboya kwa makufuli, Mabaharia wa Meli katika Ziwa Victoria hutuliwaza abiria: Meli inazama taratibu, haiwezi kuzama ghafula.

Daimler

JF-Expert Member
Sep 11, 2018
556
973
Wakati tukiendelea kuomboleza vifo vya Watanzania wenzetu waliotutoka, ni muda pia wetu sisi wananchi wa Kanda ya Ziwa, ku-revise way back kuangalia namna ambavyo tumekuwa tukisafiri katika Ziwa Victoria. Kampuni ya Huduma za Meli nchini inayomilikiwa na Serikali (MSCL) inamiliki meli kadhaa za abiria katika Ziwa Victoria, zikiwemo: MV Victoria (Bukoba), MV Serengeti (Uzinza), MV Butiama na MV Clarias (Ukerewe).
Tunajua adha ya usalama ilivyo ya muda mrefu. Meli ya mwisho ya abiria kuundwa na Serikali ni MV Serengeti mwaka 1988 na tangu hapo, tumekuwa tukijionea meli ndogo ndogo tu ndizo zikiundwa na watu binafsi licha ya abiria kuongezeka maradufu katika Ziwa Victoria, hali iliyopelekea abiria wanaotumia Meli hizo kubwa kupungua kutoka 903,000 mwaka 2006/2007 hadi 324,000 mwaka 2015/2016.
IMG_8718.jpg


Hali imekuwa ya kukatisha sana tamaa kipindi cha nyuma. Hata kwa meli hizo chache ambazo MSCL imekuwa ikiziendesha, zimekuwa mbovu na zinazofanyiwa matengenezo ya mara kwa mara, kiasi cha kuleta hisia kuwa zimekuwa zikifanyiwa hujuma na watumishi wa MSCL na hivyo kuzifungulia milango meli za watu binafsi.
Hata hivyo, kwenye tahadhari za kiusalama ni kuwa, mabaharia wa meli za umma na za binafsi wamekuwa wakiwaelekeza abiria wakati wa safari kuwa, usafiri wa meli ni wa salama zaidi na kwamba meli haiwezi kuzama kwa ghafula bali huzama taratibu (husahau kuwa meli pia zinapinduka, kama MV Nyerere). Kwa maelezo yao hayo, huwa wameyafungia maboya (life jackets) kwa makufuli kiasi kwamba hakuna mtu yeyote anayeweza kuyachukua dalili za ajali zikianza mpaka wao watakapoyafungua.
Wenyeji wa Kanda ya Ziwa, wengi wao hujua kuogelea so huwa hawana hofu yoyote kutokana na mazoea ya kusafiri mara kwa mara (japokuwa wanajua kuwa ukizama kwenye maji ya kina kirefu uogeleaji huwa ni mgumu sana kutokana na nguvu ya maji). Shida huwa kwa wageni ambao hata kuangalia ndani ya maji tu pekee huogopa, so wanapoona maboya yamefungwa hukosa amani.
IMG_8724.jpg

Maboya yakiwa yamefungiwa kwenye lock kwenye MV Nyehunge. Hapa ajali ikitokea, tutatafutana tu.

Vilevile, kutokana na meli za MSCL kuwa mbovu muda mwingi, abiria wanaokwenda Ukerewe hutumia sana meli za watu binafsi hasa Kampuni ya Nyehunge. Hata hivyo, mara nyingine (japo siyo mara zote), meli za Nyehunge zimekuwa zikikatisha tiketi bila kurekodi taarifa za abiria aliyekatiwa tiketi, hali inayoonyesha kuwa, endapo ajali ikitokea, hawawezi kujua akina nani walisafiri zaidi ya kujua idadi ya tiketi walizouza.
IMG_8716.JPG

Meli mpya ya Nyehunge iliyofunguliwa mwaka 2016. Hii ina maboya mengi. Angalia maboya kule juu.

Wakazi wa Kanda ya Ziwa, wamefurahia sana kitendo cha Serikali kutangaza kuunda meli kubwa ya kwenda Bukoba, pamoja na kukarabati Meli za Victoria (Mwanza-Bukoba)na Butiama (Mwanza-Ukerewe).
IMG_8711.JPG

Meli inayotajiwa kuundwa na Wakorea kufanya route za Mwanza - Bukoba.

Pamoja na kuishukuru Serikali kwa kuunda meli mpya kubwa na kukarabati MV Victoria na MV Butiama, tunaiomba itengeneze meli nyingine kwa ajili ya Visiwa vidogo vilivyoko Magharibi ya Kisiwa cha Ukerewe katika Tarafa ya Ilangara. Visiwa hivyo, ni: Kamasi, Galinzila, Gana, Bulubi, Izinga na Sizu. Ukerewe ndiyo inayoongoza Tanzania kwa uvuvi wa samaki hasa dagaa, huku zaidi ya nusu ya samani hao wakivuliwa kutoka katika Visiwa hivyo vilivyoko Tarafa ya Ilangara, yenye wakazi wapatao 100,000. Cha ajabu hakuna meli bali boti/mitumbwi tu, wakati ina abiria wengi kama (probably kuzidi) wa Ukara.

IMG_8713.jpg
 
Changamoto za usafiri Ukerewe. Hizi ndizo meli zinazotoa usafiri mkubwa katika Visiwa vipatavyo 27 wilayani Ukerewe.
IMG_8726.JPG


IMG_8728.jpg
 
IMG_8710.jpg


IMG_8725.JPG

Abiria wakishuka kwenye boti zinazoendeshwa na mashine mbili zenye horsepower 45. Hapo unaowaona abiri ni cha mtoto. Siku ya mnada wa Kakukuru huwa ni purukushani nguo kuchanika.
 
Naomba nikusahihishe kidogo.
Hizo life jacket hazijafungiwa na kufuri. Ni wewe kuvuta mlango na kuchukua tu.
 
Naomba nikusahihishe kidogo.
Hizo life jacket hazijafungiwa na kufuri. Ni wewe kuvuta mlango na kuchukua tu.
Uzoefu ni kuwa, huwa yamefungwa na siyo rahisi mpaka wao ndio waje kuwagawia. Nimeshasafiri na MV Butiama, Clarias, Serengeti na Nyehunge meli zao mbili; kote huko sijawahi kuona namna nyepesi ya kuwaokoa abiria in case meli ikapinduka ndugu.
Fikiria ilivyo ngumu sana watu mko 100 halafu mkae tu mmetulia mnamsubiri mtu wa kuwasambazia maboya!!
 
Wamekariri meli itazama taratibu ,iwepo Sheria ukipata meli lzm uvae life jacket kama kwenye basi mkanda,wangevaa lifejacket asingekufa MTU pale wangelea majini
Kuvaa life jacket wakati Wa safari ya meli ni kutoonyesha imani n safari yenyewe
 
Wamekariri meli itazama taratibu ,iwepo Sheria ukipata meli lzm uvae life jacket kama kwenye basi mkanda,wangevaa lifejacket asingekufa MTU pale wangelea majini
Kumbuka kuvaa life jacket wakmat
 
Kwani imani ndio nini mzee? Hivi ulishawahi kusafiri hata basi lolote la kwenda mikoani ama kupanda ndege na usihofie ajali, kweli?
Mkuu mm ni baharia by professional,,, huwezi kuvaa life jacket kama hakuna hatari,,,unapovaa lafe jacket unatengeneza mazingira ya kwamba safari sio salama,,,meli Ku BIDUKA ni NADRAB SANA,,,NA MARA NYINGI meli za ABIRIA NA MIZIGO ndy hufanya hivyo sababu ya UPANGAJI VIBAYA WA MZIGO,,,au ABIRIA WALIKUWA NA TAHARUKI WAKAKIMBILIA UPANDE MMOJA MELI IKALALA,,,life jackets n life rings na MABOYA MENGINE YA KUJIOKOA NI in case of emergency.... MKUU,,, meli ni salama ZAIDI kuli
 
Mkuu mm ni baharia by professional,,, huwezi kuvaa life jacket kama hakuna hatari,,,unapovaa lafe jacket unatengeneza mazingira ya kwamba safari sio salama,,,meli Ku BIDUKA ni NADRAB SANA,,,NA MARA NYINGI meli za ABIRIA NA MIZIGO ndy hufanya hivyo sababu ya UPANGAJI VIBAYA WA MZIGO,,,au ABIRIA WALIKUWA NA TAHARUKI WAKAKIMBILIA UPANDE MMOJA MELI IKALALA,,,life jackets n life rings na MABOYA MENGINE YA KUJIOKOA NI in case of emergency.... MKUU,,, meli ni salama ZAIDI kuli
Je, unakumbuka kuwa MV Bukoba mwaka 1996 nayo ilizama kwa kupinduka?
 
Kinga ni bora kuliko tiba ndo maana tunasisitizwa kuvaa helment kwenye pkpk na kufunga mikanda kwenye bus
Mkuu lifme jackets zinavaliwa in case of emergency ,,ndy utaratibu,,meli KU CAPSIZE NI NADRA SN MKUU,,,pia unaporuhusu abiria kuvaa kabisa ni kujenga hofu. ,sababu AJALI ya meli ni tofauti na bus,,au ndege,,au train... Hapo kuna jambo lisilo kawaida lilitokea,,,ngoja survived wataongea..ndy maana hata kukiwa na tatizo mabaharia wao wanatakiwa kuwapooza abiria wasihamaki,,unapohamaki melini ni kusababisha meli Ku biduka,,maana watakuwa wanakimbia hovyo bila mpangilio na meli itayumba,,,
 
Back
Top Bottom