Huku sisi tunaongeza KODI kila kona wengine wanapunguza.

wrong turn

JF-Expert Member
Feb 17, 2013
438
170
Uingereza kuvutia makampuni ya biashara

151021042852_uk_george_osborne_512x288_pawire_nocredit.jpg


Waziri wa fedha wa Uingereza George Osborne ameeleza mipango ya wizara yake yenye lengo la kupunguza kodi muhimu ya faida katika biashara.

Hatua ya Osborne ni sehemu ya mkakati wa kiuchumi katika harakati za kuvutia uwekezaji mpya, na hii inafuatia kura ya maoni iliyopigwa mwezi uliopita ambayo iliamua Uingereza isite kuwa mwanachama wa umoja wa ulaya.

Osborne aliliambia gazeti la Financial Times kwamba anataka kupunguza kodi ya shirikishi kutoka asilimia ishirini hadi chini ya asilimia kumi na tano.mwandishi wa BBC wa masuala ya biashara ameeleza kwamba kura ya maoni ilikuwa ni mkakati wa kuisaidia Uingereza kuvutia uwekezaji kutoka kwa kampuni mbali mbali mpango ambao inawezekana haukufanikiwa kufuatia kura hiyo ya maoni.

Chanzo: BBC/Swahili.

My take: Kiukweli sisi waAfrika kuna sehem tunakosea, hususan kwenye dhana nzima ya kujiweka huru na mambo yetu, kama Biashara, Siasa, Kilimo, Mifugo, Technology, na nk, huwa tunababaisha, kutiana hofu, hatupendani, wakurupukaj, hatupendi kushindwa ikiwa tumeshindwa, tunapenda sifa na majigambo, nahisi pia tuko tofauti na wengine kwa mengi tuu, kiukweli ni mengi ambayo yanatugarimu kwenye maisha yetu ya kila siku.
 
Tofautisha Ulaya na Africa tena nchi ya kimaskini hata sukari hamna.

swissme
 
Tofautisha Ulaya na Africa tena nchi ya kimaskini hata sukari hamna.

swissme
Tofauti ya watu wa Ulaya na Afrika ni ndogo, Rangi, lugha, na maeneo tunayoishi amabayo haiathiri maendeleo, kitu ambacho kina mata ni akili, na wote wanazo, ila tatzizo jinsi gani ya kutumia akili zetundio tatizo.
 
Back
Top Bottom