Huku ni kupotoka kwa viongozi na watendaji serikali ya CCM wilaya ya Lushoto

Mbelwa Germano

JF-Expert Member
May 7, 2011
789
289
Ukosefu wa ubunifu katika kuibua vyanzo vya mapato na udhibiti wake katika uendeshaji miradi ya maendeleo umewafanya viongozi na watendaji wa serikali ya CCM wilaya ya Lushoto wajishirikiana na madiwani wao kuendelea kuwanyonga wananchi wakiwamo walimu kwa kuwalazimisha kuchangia Tshs.20,000 kwa ajili ya ujenzi wa maabara za shule za sekondari.Wananchi hawa pamoja na kuchangia pesa taslimu wanalazimishwa kuchangia nguvu kazi.

Pamoja na ukweli kwamba moja ya jukumu la serikali ikiwemo halmashauri za wilaya ni kukusanya kodi na kutoa huduma kwa wananchi jambo hili ni tofauti chini ya utawala wa CCM kwa kuwabambikia migizo ya mateso wananchi wake kutokana na ukosefu wa ubunifu katika kubuni na kudhibiti vyanzo vya mapato.

Serikali hii sikivu ya CCM inatoa misamaha mikubwa ya kodi,inashuhudia ukwepaji mkubwa wa kodi,rushwa na ufisadi na inaruhusu wananchi waliowengi kunyonywa kwa ajili ya utukufu wa watu wachache.

Ieleweke kwamba pamoja na walimu kuwa na makato ya kodi ya mapato,bima ya afya,hifadhi ya mifuko ya jamii n.k. kutoka kwenye mishahara yao bado wanabebeshwa mzigo huu wa mateso pamoja na kufanya kazi katika mazingira magumu.

Hoja hapa si kupinga ujenzi wa maabara bali uchakato na maamuzi yasiyozingatia hali halisi ya maisha ya watanzania masikini,serikali kusahau mantiki ya ukusanyaji kodi kwa ajili ya maendeleo ya watu na mwisho ukosefu wa ubunifu na udhibiti wa mapato na matumizi ya fedha za umma.

Mbelwa Germano
(Lushoto Constituent)
 
Swala la watu wengi linahitaji umakini wala siyo la kukurupuka lazima uwajibikaji wa pamoja uwepo wala siyo la biongozi tu.
 
Ukosefu wa ubunifu katika kuibua vyanzo vya mapato na udhibiti wake katika uendeshaji miradi ya maendeleo umewafanya viongozi na watendaji wa serikali ya CCM wilaya ya Lushoto wajishirikiana na madiwani wao kuendelea kuwanyonga wananchi wakiwamo walimu kwa kuwalazimisha kuchangia Tshs.20,000 kwa ajili ya ujenzi wa maabara za shule za sekondari.Wananchi hawa pamoja na kuchangia pesa taslimu wanalazimishwa kuchangia nguvu kazi.

Pamoja na ukweli kwamba moja ya jukumu la serikali ikiwemo halmashauri za wilaya ni kukusanya kodi na kutoa huduma kwa wananchi jambo hili ni tofauti chini ya utawala wa CCM kwa kuwabambikia migizo ya mateso wananchi wake kutokana na ukosefu wa ubunifu katika kubuni na kudhibiti vyanzo vya mapato.

Serikali hii sikivu ya CCM inatoa misamaha mikubwa ya kodi,inashuhudia ukwepaji mkubwa wa kodi,rushwa na ufisadi na inaruhusu wananchi waliowengi kunyonywa kwa ajili ya utukufu wa watu wachache.

Ieleweke kwamba pamoja na walimu kuwa na makato ya kodi ya mapato,bima ya afya,hifadhi ya mifuko ya jamii n.k. kutoka kwenye mishahara yao bado wanabebeshwa mzigo huu wa mateso pamoja na kufanya kazi katika mazingira magumu.

Hoja hapa si kupinga ujenzi wa maabara bali uchakato na maamuzi yasiyozingatia hali halisi ya maisha ya watanzania masikini,serikali kusahau mantiki ya ukusanyaji kodi kwa ajili ya maendeleo ya watu na mwisho ukosefu wa ubunifu na udhibiti wa mapato na matumizi ya fedha za umma.

Mbelwa Germano
(Lushoto Constituent)
Ni vema tukajifunza kutoa mapendekezo na suruhu ya mambo kuliko kuishia kulalamika na kulaumu huku ukishindwa kutoa suruhu ya mambo huu ni uvivu wa kufikiri.
 
Kamanda Mbelwa, nasikitika sana katika hili mana kuna rafiki yangu ambaye ni mwalimu amejilaumu sana kufanya kazi Lushoto na kuona kama kituo cha adhabu maana alikuwa anafanya kazi Arumeru then akarudi kwao huku. Kuna hawa watu wa bodaboda ambao pia wamelazimishwa kulipa sh 4000 kila mmoja nao wanalia kivyao. Kumkata 20,000/- hasa walimu wa utawala wa CCM unakuwa unaitesa familia ya huyo mwalimu kwa mwezi husika kwani ni walimu wachache sana wanaochukua mshahara taslimu unaozidi laki moja, wengi wao tayari wanakatwa malipo ya mikopo waliyokopa ili waendane na kasi ya maisha katika kujikimu. Tatizo la Lushoto ni kubwa sana hasa ukizingatia Madiwani waliop[o na uwezo wao uliopo. Lushoto ina wasomi wengi sana ila kaangalie hao wasomi wa Lushoto wanawakilishwa na kina nani katika kata zao ndo utakuja kupata hasira. Fikiria kwa akili ya kawaida baraza la madiwa linapitisha bajeti ya kukarabati barabara inayoingia stand ambayo ni lami kwa kusakafia na cement? Mji upo tangu enzi za Mjerumani ila mji hauna Stand ya mabasi uliona wapi? Lushoto inahitaji mabadiliko makubwa sana hasa wazawa kubadilika na sio muda tena wa kuendeleza sisa za kiukoo ambzo zinatawaliwa na ukoo fulani tu.
 
Ni vema tukajifunza kutoa mapendekezo na suruhu ya mambo kuliko kuishia kulalamika na kulaumu huku ukishindwa kutoa suruhu ya mambo huu ni uvivu wa kufikiri.

Sa hapa umeandika nini? Suruhu ulikuwa unamanisha suluhu? Kawambwa kweli kama Nape alivyosema andoke anatuharibia elimu yetu. Suluhu ni kuwapumzisha hawa watawala kwa wameshindwa kuondoa matatizo yanayowakabili wananchi sana sana wanapiga dili la meno ya tembo tu.
 
Hili linatia hasira na kichefuchefu, huyu mfanyakazi atarudisha haka kamshahara kake ka kubangaizia siku 5 serikalini? amekatwa kodi tena huku 20 elfu, wakati wapuuzi hawakusanyi kodi na wanazokusanya wanajitimizia matakwa yao kwanza; posho ya safari, chai ya ofisi, miradi hewa, misamaha feki, Kisha muongo anajiona shujaa kusimama na kuwaambia watz makusanyo ya kodi migodi ya tanzanite ni million 30 kwa miaka 5!!!!!!!!!!!!
Shame, shame, shame!!!
Lushoto kuna dhahabu, magogo yanasafirishwa kila leo, misitu inavunwa tena kwa vibali vya council etc, wananchi tukatae huu uzulumati
 
Ni vema tukajifunza kutoa mapendekezo na suruhu ya mambo kuliko kuishia kulalamika na kulaumu huku ukishindwa kutoa suruhu ya mambo huu ni uvivu wa kufikiri.

Suluhisho ni kutambua na kudhibiti vyanzo vya mapato bila kuathiri mwananchi wa kipato cha chini.Serikali ambayo haiwezi kukusanya na kudhibiti kodi kwa manufaa ya watu wake haina uhalali wa kutawala
 
Lushoto kuna dhahabu, magogo yanasafirishwa kila leo, misitu inavunwa tena kwa vibali vya council etc, wananchi tukatae huu uzulumati

Inatia hasira kuona watu wachache ambao wanaharibu maliasili lushoto bila kuchukuluwa hatua yoyote na kibaya zaidi UVCCM lushoto wako kwenye mchakato wa kupewa msitu kijiongezea mapato.
 
Kwa manufaa ya wanajamvi Mrisho ametumia mbinu gani tofauti na Majid wa Lushoto?Ili tuweke mjadala vizuri.

Mbelwa Germano
Kwakifupi tu na sina uwakika kama ni Tofauti na za huko Lushoto.
1. Nimeona maranyingi akishiriki na kuhamasisha wananchi kujitolea hasa Nguvu kazi.

2. Last time alikuwa akiorganize wafanyabiashara na makampuni pamoja na wakaazi wa Korogwe wajitokeze kuchangia ujenzi.

3.Pia alikuwa kwenye mchakato wa kuandaa kikao cha wana Korogwe waishio Dar ili waweze Kuchangia Maaendeleo wilayani kwao.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Kibanga,kuna tofauti ya kuhamasisha na kulazimisha,walimu wilaya ya lushoto hawahamasishwi bali wanalazimishwa.

Wananchi wa lushoto wanalazimishwa sio kuhasishwa kuchangia fedha na nguvu kazi.Wananchi hawa wanachangishwa without pre-info kwamba michango inahitajika kiasi gani?Other sources ni zipi na kiasi gani?wanachangia kwa asilimia ngapi n.k.

Mchakato wa michango hii hauko wazi,kwenye community based activities lazima kuwe na uwazi katika utekelezaji wa miradi mbalimbali bila ya serikali kusahau mantiki ya ulipaji kodi na kuweka vipaumbele katika utekelezaji wa miradi mbalimbali katika jamii.
 
Hili jambo linanikera sana,hii ni aibu kwa serikali ya ccm kupitia watendaji wake wa LDC kwa kushindwa kusimamia na kukusanya kodi badala yake wanaendelea kutukamua wanacnhi maskini Magid analazimisha mambo sio mtu mbunifu hata kidogo ubabe umemtawala nadhani anajihami kutokana na elimu yake kua ya kuunga kwa soltep,mji wa lushoto una vyanzo vingi sana vya mapato tena vya uhakika ambavyo vikisimamiwa kwa uhakika LDC itakua ni leading district in tanzania lakini watendaji hovyo kabisa,wadiwani uchwara kabisa mji mzima barabara ya lami ni moja tu, stand imeoza ikinyesha mvua ndio balaa but no body cares kwa vile wao wanatembelea stk.. ukienda korogwe utashangaa ka mji kadogo tena ni product ya lushoto lakini mji uko safi kabisa tofauti na lushoto,si ajabu hata mji mdogo wa mombo in the near future ukawa next level kwa lushoto.

Lushoto kuna kilimo cha mboga mboga ambapo kila leo msururu wa malori zaidi ya mia kutoka dar,arusha yanasafirisha mzigo,misitu minene ambayo watu wanavuna mbao na magogo,lushoto kuna maeneo mazuri ya utalii, mahoteli ya kitalii kibao,camp sites kibao hivi vyote ni vyanzo vizuri kabisa vya mapato lakini bado mji ni maskini haupendezi utasema hakuna viongozi? where is shekifu? ulichaguliwa kwa kishindo na wasambaa ila umewatelekeza nakuahidi mzee 2015 you are going to feel a beat down....Viongozi wa LDC simamieni mapato vizuri mlete maendeleo kwa wananchi sio kutubebesha zigo la misumari kwa maslahi yenu binafsi "kesho kwa mungu kuna moto..."
 
Last edited by a moderator:
lushoto kuna maeneo mazuri ya utalii, mahoteli ya kitalii kibao,camp sites kibao

Sekta ya utalii haichangii chochote wilaya ya lushoto zaidi ya kuwa mradi wa watu wachache,ukitazama vyanzo vya mapato vya LDC utathibitisha hili.

CCM wamehodhi uwanja wa sabasaba na vibanda vya biashara na kuimyima mapato halmashauri,kimsingi uwanja huu ungebadilishwa matumizi ma kuwa stendi ya wilaya,ambapo vyumba vya biashara vingejengwa na kuongeza mapato kwa halmashauri.

Lushoto kuna uhaba mkubwa wa maeneo ya ujenzi wa ofisi kwa ajili ya shughuli za mashirika,taasisi n.k.Iwapo kungekuwa na ubunifu kidogo tu kwa watumishi na watendaji wa serikali ya CCM na wadiwani mizigo wa wilaya ya lushoto wasingepoteza fursa hii na LDC kujiongezea mapato.

Lushoto kuna udhibiti dhaifu wa mazao ya misitu,upo uharibifu holela wa maliasili kwa sababu ya rushwa na ufisadi wa watemdaji wa LDC,baadhi ya viongozi wanafanya uharibifu huu mkubwa ni viongozi wa CCM.
 
Fikiria kwa akili ya kawaida baraza la madiwa linapitisha bajeti ya kukarabati barabara inayoingia stand ambayo ni lami kwa kusakafia na cement?.

Huu ni udhaifu mkubwa kwa madiwani wa CCM,hakuna wa kuhoji,kuna kazi kubwa sana ya kubadilisha mindset za % kubwa ya watu wa lushoto.

Siasa za kiukoo haziwezi kuinufaisha lushoto,wananchi wengi wameruhusu hofu itawale miyoyoni mwao na kushindwa kuhoji mambo ya kimsingi,viongozi wa kisiasa wamekuwa wakicheza na fikra za wananchi bila kubainisha na kutatua matatizo halisi ya wananchi wa lushoto.Hii ni moja ya tabia mbovu za kina Shekifu and co.
 
Kuna kikundi kidogo sana cha watu watano ambao wanamini wamehodhi fikra za watu wa lushoto
 
Back
Top Bottom