Huku ni kufukua makaburi au ni kujipaka matope?

Nyankurungu2020

JF-Expert Member
Oct 2, 2020
4,085
6,564
Nimemaliza shughuli zangu za kila siku kama ilivyo ada nimechukua gazeti la Mwananchi, nashangaa kukuta hii habari, Waziri mkuu wa nchi yetu ambae ni mkuu wa shughuli za serikali ametoa amri kuwa wakurugenzi walionunua magari ya Sh 270 wajieleze. Kwamba walitoa wapi pesa za kununulia hayo magari. Wakurugenzi hao ni wa halmashauri za Kahama, Chato, jiji la mwanza na Msalala.

Ghafla bin vuu nikakumbuka kuwa mkuu wa kaya mwenyewe aliwahi kukiri kuwa Watanzania sio wajinga na unapowaletea habari ambazo haziingii akilini watakaa kimya ila kumbuka watakuchora na kukusanifu kama katuni

Tujiulize kama watu wenye akili timamu, taratibu za kununua magari zikoje? Yaani mpaka hawa wakurugenzi wanaambiwa wajieleze,je hawakufuata taratibu?

Au ndio kuondoa aibu kisa tu Mkurugenzi wa Geita alisimamishwa kimakosa? Na hii ni baada ya wananchi kuona kuwa mkurugenzi hawezi kununua gari kwa maamuzi yake!

Kwa nini hii habari ya kuhoji gharama za magari ya wakurugenzi iwe sasa awamu hii tunapoenda kumaliza ngwe ya pili? Hapo mwanzo mbona ilikuwa kimya? Na tuliona karibu kila halmashauri zina Vx v8 yenye thamani zaidi mil 270!

Je, huku ni kujipaka matope au ndio kufukua makaburi?
 
Mi ni mnywaji mzuri tu wa lite, sinywi kila mara kwakuwa kipato hakitoshi kufanya hivyo.

Sasa hawa wanaulizana leo baada ya kutumia? Waache uchorobi, uwezo wanao, wanunue tu na sisi tuzionepo zikipita, tufurahie nchi yetu ina watabe wanatembelea SUV shikamoo.
 
Nimemaliza shughuli zangu za kila siku kama ilivyo ada nimechukua gazeti la mwananchi,nashangaa kukuta hii habari, Waziri mkuu wa nchi yetu ambae ni mkuu wa shughuli za serikali ametoa amri kuwa wagurugenzi walionunua magari ya Sh 270 wajieleze...
Kitu usichokijua ni hii kauli ya kuwa mkuu wa kaya anafanya kila jambo, na wamekuwa wakimtuhumu kwamba amekuwa one man show,

Ki ukweli inawezekana katika office ya waziri mkuu ilipitisha haya magari lakini kwa kupitia wakasimu madaraka wa waziri hasa kwenye masuara ya ndani.

Pia nakumbuka haimashauli zilipangiwa kunukua magari nadhani yasiyozidi milioni 200 kama si 150 na ni zile toyota double cabin hilux sasa hawa wa kahama na geita wanafukuzana kununua magari hayo kwa faida ipi?

Nakumbuka kipindi cha kikwete watu walilalamika sana kuhusu magari ya bei kubwa, sasa iweje kwa mbana matumizi wewe ukanunue gari la bei kubwa lisilozalisha ni mapato tena ambalo haliwezi kusaidia hata kubeba madawa kupeleka kwenye kituo cha afya?

Hao kama wanadhami wao ni special sana basi watumbuliwe tu. Niliona gari la mkuu wa mkoa wa mara baada ya ile ya zamani kupata ajari wakamletea plado sas iweje mkurugeni atembee na ya 400 au 270 wakati mkuu wa mkoa ana ya chini ya 200? Nasema hao watumbuliwe tu kwa kuwa hawakutumia akiri kufikili.

Sasa wafanya biashara tunakamliwa pesa kisha mtu umekaa offisini na mshahara kutoka kwetu unalipwa kisha ujione bishoo wakati watu bado hawana maji?

Watumbuliwe tu waje tusaidiane kuzitafuta ili nao walipe kodi kwa kusumbua akiri.
 
Nimemaliza shughuli zangu za kila siku kama ilivyo ada nimechukua gazeti la mwananchi,nashangaa kukuta hii habari, Waziri mkuu wa nchi yetu ambae ni mkuu wa shughuli za serikali ametoa amri kuwa wagurugenzi walionunua magari ya Sh 270 wajieleze...
Hiki ni Kipindi cha mwisho cha Awamu ya Tano kuwa madarakani na Wakurugenzi watakaosimamia Uchaguzi ujao kama watapewa magari mazuri, nyumba nzuri na Mishahara mkubwa watapewa na Awamu ya Sita kuwa hiyo kwa Waziri Mkuu hata wakipewa Bajaji sawa tu maana kazi ya kutangaza ushindi wa CCM walimaliza.
 
Nimemaliza shughuli zangu za kila siku kama ilivyo ada nimechukua gazeti la mwananchi,nashangaa kukuta hii habari, Waziri mkuu wa nchi yetu ambae ni mkuu wa shughuli za serikali ametoa amri kuwa wagurugenzi walionunua magari ya Sh 270 wajieleze..
Tatizo la msingi ni mfumo. Ukishakuwa na wakurugenzi ambao pia ni wasimamizi wa uchaguzi, na walishaelekezwa kuvunja Katiba na Sheria, kwamba kazi yao namba moja ni kuhakikisha bosi wao na chama chake wanashinda "ushindi wa kishindo", na wakiishatekeleza hilo, unawezaje kutarajia "maadili" kutoka kwao?

Mteule wao kwanza anachekelea tu, acha wajipongeze eti. Kwani waziri mkuu anajua makubaliano ya hawa jamaa na bosi wao???

Ufumbuzi wa uozo huu ni UTAWALA WA MAJIMBO ambapo viongozi hawa watawajibika kwa wananchi moja kwa moja na wanaweza kuondolewa madarakani muda wowote.
 
19 Reactions
Reply
Back
Top Bottom