Huku mtaani Rais Samia hakubaliki kivile, Upinzani wangekuwa na Mikakati 2025 wangeichukua nchi

Watanganyika wengi wanajua Nchi haina Raisi na wanajua aliyejuu ni Mama ni Boshen tu
 
Hongera sana Robert Heriel ,huwa nikisoma maandishi yako nafarijika sana, naona kuwa bado tunao Watanzania wanao ona mambo kwa jicho tofauti!
 
Siku zote Taikon ni mtu asiye na unafiki, mapema ukweli mara nyingi. Hivyo ndivyo ninavyojitambulisha.

Mimi sio Mfuasi wala mwanachama wa Chama chochote au mtu yeyote Yule. Kumaanisha nipo huru kusema ukweli.

Wazazi wangu, ndugu, jamaa na marafiki zangu karibu wote ni CCM.

Kipindi cha JPM wengi wao waliniona ni nipo chama pinzani hasa CHADEMA kutokana na kuwa sikuwa navutiwa na Siasa za JPM hasa za ubabe.

Wakati nikimpinga JPM nilipata Upinzani mkubwa kutoka Kwa wazazi wangu, ndugu, jamaa na marafiki Kwa sababu wengi wao walikuwa wakimkubali.

Kitu kimoja walichoshindwa kunielewa ni kuwa, Taikon hana ushabiki, sina timu, sina chama, na sasa nakaribia kutokuwa na Dini hasa hizi dini za kigeni. Nipo huru kusema ukweli bila kuwa mnafiki.

Sasa hapa katikati mambo yamebadilika, baada ya JPM Kufariki SSH kachukua usukani.

Kinachonishangaza ni kuwa Wale wote waliokuwa wanampenda JPM ati hawamkubali SSH licha ya kuwa nao ni CCM.

Kutokana na kuwa, Taikon ni mtu wa kujichanganya vijiweni, na kwenye vilinge. Nimegundua kuwa SSH Hana ushawishi mkubwa ndani ya jamii.

Hata hivyo hilo lisimuumize SSH kwani ni Jambo la kawaida kwenye jamii ya kitanzania ambayo haijazoea kuongozwa na Mwanamke hasa kwenye nafasi ya juu Kama urais.

Sifikirii Kama kuna Jambo lolote ambalo SSH atalifanya ili jamii umekubali na apate ushawishi mkubwa ndani yake.

Kwa macho yangu, nikijaribu kuangalia mbele naona Kama karibu kila atakachokifanya SSH atapata lawama kwa sehemu kubwa.
Hiyo pia isimuumize kama nilivyotoa sababu ya Jambo hilo awali.

KINACHONISHANGAZA;

Upinzani sijui hawataki kuchukua nchi au ni kitu gani. Au pengine kuna ambao wanawahujumu, au huenda wanashindwa kusoma gap lililopo katika awamu hii.

Upinzani sijui intelligensia yao imeshindwa kuona gap la kutosha ambalo wakilitumia wanaweza kuchukua Dola 2025.

Intelejensia yangu inanambia hivi kuwahusu Watanzania;

1. Watanzania wengi wanaamini kiongozi anayewatukana matajiri ndiye mwenye mapenzi ya kweli nao.
Sio ajabu Hayatti JKN na JPM wakawa wanapendwa zaidi na kuonekana watetezi wa kweli WA wanyonge kuliko Marais wengine.

2. Watanzania wengi wanapenda zaidi kiongozi mwenye tabia za kidikteta. Unajua Kwa nini?

Udikteta haubani masikini au wajinga.
Udikteta unawabana zaidi matajiri na watu walioenda shule/wasomi.

Watanzania wengi wao ni masikini na wajinga wasio na elimu, Rais yeyote akiwa na viashiria vya udikteta lazima apendwe na Kundi Hilo zaidi.

3. Watanzania wengi huendekeza propaganda na mambo dhahania.

Rais yeyote anayewekeza huko lazima apate wafuasi, ushawishi na kupendwa Sana.

Watanzania wengi kutokana na umasikini, na kutokusoma wengi wao hupenda propaganda za uongo kuliko mambo ya kisayansi na kitaalamu.

Usishangae hata ishu za CORONA zinavyoendeshwa, ni rahisi kumwambia MTANZANIA kuwa Corona ni mpango wa Wazungu kuingamiza Dunia, au mpango wa Freemason kuelekea 666 na wakakuamini.

Ni rahisi kuwaambia Watanzania ugonjwa Fulani umesababishwa na Ushirikina au uchawi au laana ya Mungu wakakuelewa hata Kama ugonjwa huo unatokana na uchafu wao au mitindo mibaya ya maisha.

JPM alilijua hilo vyema, hata Manabii Uchwara kina Gwajiboy, anajua fika kuwa Watanzania wengi ni Hamnazo, ndio maana huamini Kwa urahisi Propaganda na mambo dhahania.

4. Watanzania wengi hupenda anguko la aliyefanikiwa.
Rais Kama atawekeza kwenye kuangusha, kutumbua watu au kufukuza kazi Wasaidizi wake. Basi lazima apendwe na Watanzania wengi.
Kwani Watanzania wengi kutokana na maisha yao kuwa magumu wanataka kila mtu awe na maisha magumu Kama wao.

Watanzania wengi hawapendi kiongozi anayetoa second chance Kwa kiongozi aliyekosea.
Wanataka akijaribu hata Kama ni kitu kidogo basi umtumbue.

5. Watanzania wengi wanapenda uwataje taje kwa majina ya kuwaonea huruma Kama wanyonge, masikini, wavuja jasho, watifua udongo NK.
Ukitaka uzikamate akili za Watanzania wengi ukiwa kiongozi basi karibu kila baada ya maneno yako hamsini basi chomekea mfano wa sentensi zifuatazo:

" Nawapigani wavuja jasho hawa"
" Waacheni wanyonge wafanye kazi zao Kwa Amani"
" Uchumi huu umelenga kugusa watu masikini"
" Yeyote atakayewaonea hawa watifua udongo ataona joto la jiwe"
" Ninawatumikia Hawa wasakatonge, hawa ndio mboni yangu"
Na kauli zingine Kama hizo.

Kama hutatumia kauli hizo Kwa sehemu kubwa basi jua umeumia kwenye nchi hii.

6. Watanzania wengi hasa wasioajiriwa serikali au sekta Rasmi hupenda kusikia watumishi wa Umma wanalalamika iwe Kwa kutoongezewa mishahara, iwe Kwa kunyimwa posho, au kunyanyaswa na wanasiasa.

Kiongozi yeyote ambaye atawafanya watumishi wa Umma walie lie Kama Mbuzi, anajijengea kupendwa na Watanzania wengi waliomasikini.

7. Watanzania wengi hasa waliokataa shule wanafurahia wasomi kukosa Ajira.
Unaweza usiamini lakini iko hivyo.

Mtu yeyote ambaye ataathiri suala la Ajira mpaka wasomi wakapiga mayowe lazima apendwe na watu wa chini kabisa.

8. Watanzania wengi wanapenda kutetewa kuliko kujitetea, yakikukuta watakuita kihere here. Kutokana na umasikini na ujinga WA wengi hii huwafanya kuwa wanafiki.

Unapowatetea Watanzania basi kuwa makini Sana. Watetea ukiwa na maslahi yako binafsi. Ukiingia mzima mzima yatakukuta, na yakikukuta watakuita kiherehere.

Kama nilivyowahi kuandika, usiwasaidie masikini. Kisha niliwahi kumuandikie Barua Lisu kuwa asiwatetee masikini na wajinga isipokuwa akiwa na Maslahi yake binafsi.

Upinzani nafikiri wakati huu kwao ulikuwa muhimu Sana.

SSH Hana ushawishi mkubwa kihivyo. Mlipaswa mtembee na Line hiyo Kwanza.

Kisha mtembee na makosa yanayojitokeza kama vile ishu ya Tozo za MIAMALA, suala la kukatika katika Kwa umeme, kupanda Kwa bei ya Mafuta NK.

Kwani mambo hayo ndio yanaogusa Watanzania wengi waliomasikini na wasio na elimu.

Kama mngefanya hiyo calculation hakika mngepata uungwaji Mkono na Watanzania wengi ingawaje Kama nilivyosema Watanzania wengi ni WANAFIKI lakini huenda mngeongeza Fans base ndani ya jamii.

Pia kutokana na Watanzania wengi kupenda hadithi za kufikirika na propaganda za kitoto. Hili la Chanjo ya Corona mngelipinga,
Hata Kama msingepinga wote lakini angetokea viongozi wanne wenye ushawishi walipinge Kama anavyofanya Gwajima.
Ingawaje naona ugumu Kwa upande wenu kwani wenye hizo chanjo huenda ndio wanaowafadhili.

Mnashindwa hata na Gwajima bhana. Fanyeni Calculation vizuri. Hii michezo inahitaji akili zaidi kuliko hisia.

SSH akiwashinda 2025 msitegemee Kama kuna ambaye mtamuweza.

Sababu nimeshawapa, nayo ni kuwa Hana ushawishi mkubwa ndani ya jamii kutokana na kuwa bado kuna kasumba ya mwanamke kutopewa nafasi kubwa ya uongozi.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Morogoro
Upinzani hauwezi kushindana na jeshi la polisi.

Ila wanaweza kushindana na ccm na wakashinda.
 
Si ndio vyombo vya dola hivyo. Na ndio mbeleko ya ccm iliyojificha ndani ya serekali? Wewe jamaa vp?
Hata hilo hulioni? Basi unahitaji miwani.
Ni kweli ccm imechokwa na watu lakini chama kipi kipewe nchi? Binafsi sioni mbadala mzuri. Sina imani na vyama vinavyoongozwa Kama Mali ya mtu binafsi
 
Kwakatiba ipi
Siku zote Taikon ni mtu asiye na unafiki, mapema ukweli mara nyingi. Hivyo ndivyo ninavyojitambulisha.

Mimi sio Mfuasi wala mwanachama wa Chama chochote au mtu yeyote Yule. Kumaanisha nipo huru kusema ukweli.

Wazazi wangu, ndugu, jamaa na marafiki zangu karibu wote ni CCM.

Kipindi cha JPM wengi wao waliniona ni nipo chama pinzani hasa CHADEMA kutokana na kuwa sikuwa navutiwa na Siasa za JPM hasa za ubabe.

Wakati nikimpinga JPM nilipata Upinzani mkubwa kutoka Kwa wazazi wangu, ndugu, jamaa na marafiki Kwa sababu wengi wao walikuwa wakimkubali.

Kitu kimoja walichoshindwa kunielewa ni kuwa, Taikon hana ushabiki, sina timu, sina chama, na sasa nakaribia kutokuwa na Dini hasa hizi dini za kigeni. Nipo huru kusema ukweli bila kuwa mnafiki.

Sasa hapa katikati mambo yamebadilika, baada ya JPM Kufariki SSH kachukua usukani.

Kinachonishangaza ni kuwa Wale wote waliokuwa wanampenda JPM ati hawamkubali SSH licha ya kuwa nao ni CCM.

Kutokana na kuwa, Taikon ni mtu wa kujichanganya vijiweni, na kwenye vilinge. Nimegundua kuwa SSH Hana ushawishi mkubwa ndani ya jamii.

Hata hivyo hilo lisimuumize SSH kwani ni Jambo la kawaida kwenye jamii ya kitanzania ambayo haijazoea kuongozwa na Mwanamke hasa kwenye nafasi ya juu Kama urais.

Sifikirii Kama kuna Jambo lolote ambalo SSH atalifanya ili jamii umekubali na apate ushawishi mkubwa ndani yake.

Kwa macho yangu, nikijaribu kuangalia mbele naona Kama karibu kila atakachokifanya SSH atapata lawama kwa sehemu kubwa.
Hiyo pia isimuumize kama nilivyotoa sababu ya Jambo hilo awali.

KINACHONISHANGAZA;

Upinzani sijui hawataki kuchukua nchi au ni kitu gani. Au pengine kuna ambao wanawahujumu, au huenda wanashindwa kusoma gap lililopo katika awamu hii.

Upinzani sijui intelligensia yao imeshindwa kuona gap la kutosha ambalo wakilitumia wanaweza kuchukua Dola 2025.

Intelejensia yangu inanambia hivi kuwahusu Watanzania;

1. Watanzania wengi wanaamini kiongozi anayewatukana matajiri ndiye mwenye mapenzi ya kweli nao.
Sio ajabu Hayatti JKN na JPM wakawa wanapendwa zaidi na kuonekana watetezi wa kweli WA wanyonge kuliko Marais wengine.

2. Watanzania wengi wanapenda zaidi kiongozi mwenye tabia za kidikteta. Unajua Kwa nini?

Udikteta haubani masikini au wajinga.
Udikteta unawabana zaidi matajiri na watu walioenda shule/wasomi.

Watanzania wengi wao ni masikini na wajinga wasio na elimu, Rais yeyote akiwa na viashiria vya udikteta lazima apendwe na Kundi Hilo zaidi.

3. Watanzania wengi huendekeza propaganda na mambo dhahania.

Rais yeyote anayewekeza huko lazima apate wafuasi, ushawishi na kupendwa Sana.

Watanzania wengi kutokana na umasikini, na kutokusoma wengi wao hupenda propaganda za uongo kuliko mambo ya kisayansi na kitaalamu.

Usishangae hata ishu za CORONA zinavyoendeshwa, ni rahisi kumwambia MTANZANIA kuwa Corona ni mpango wa Wazungu kuingamiza Dunia, au mpango wa Freemason kuelekea 666 na wakakuamini.

Ni rahisi kuwaambia Watanzania ugonjwa Fulani umesababishwa na Ushirikina au uchawi au laana ya Mungu wakakuelewa hata Kama ugonjwa huo unatokana na uchafu wao au mitindo mibaya ya maisha.

JPM alilijua hilo vyema, hata Manabii Uchwara kina Gwajiboy, anajua fika kuwa Watanzania wengi ni Hamnazo, ndio maana huamini Kwa urahisi Propaganda na mambo dhahania.

4. Watanzania wengi hupenda anguko la aliyefanikiwa.
Rais Kama atawekeza kwenye kuangusha, kutumbua watu au kufukuza kazi Wasaidizi wake. Basi lazima apendwe na Watanzania wengi.
Kwani Watanzania wengi kutokana na maisha yao kuwa magumu wanataka kila mtu awe na maisha magumu Kama wao.

Watanzania wengi hawapendi kiongozi anayetoa second chance Kwa kiongozi aliyekosea.
Wanataka akijaribu hata Kama ni kitu kidogo basi umtumbue.

5. Watanzania wengi wanapenda uwataje taje kwa majina ya kuwaonea huruma Kama wanyonge, masikini, wavuja jasho, watifua udongo NK.
Ukitaka uzikamate akili za Watanzania wengi ukiwa kiongozi basi karibu kila baada ya maneno yako hamsini basi chomekea mfano wa sentensi zifuatazo:

" Nawapigani wavuja jasho hawa"
" Waacheni wanyonge wafanye kazi zao Kwa Amani"
" Uchumi huu umelenga kugusa watu masikini"
" Yeyote atakayewaonea hawa watifua udongo ataona joto la jiwe"
" Ninawatumikia Hawa wasakatonge, hawa ndio mboni yangu"
Na kauli zingine Kama hizo.

Kama hutatumia kauli hizo Kwa sehemu kubwa basi jua umeumia kwenye nchi hii.

6. Watanzania wengi hasa wasioajiriwa serikali au sekta Rasmi hupenda kusikia watumishi wa Umma wanalalamika iwe Kwa kutoongezewa mishahara, iwe Kwa kunyimwa posho, au kunyanyaswa na wanasiasa.

Kiongozi yeyote ambaye atawafanya watumishi wa Umma walie lie Kama Mbuzi, anajijengea kupendwa na Watanzania wengi waliomasikini.

7. Watanzania wengi hasa waliokataa shule wanafurahia wasomi kukosa Ajira.
Unaweza usiamini lakini iko hivyo.

Mtu yeyote ambaye ataathiri suala la Ajira mpaka wasomi wakapiga mayowe lazima apendwe na watu wa chini kabisa.

8. Watanzania wengi wanapenda kutetewa kuliko kujitetea, yakikukuta watakuita kihere here. Kutokana na umasikini na ujinga WA wengi hii huwafanya kuwa wanafiki.

Unapowatetea Watanzania basi kuwa makini Sana. Watetea ukiwa na maslahi yako binafsi. Ukiingia mzima mzima yatakukuta, na yakikukuta watakuita kiherehere.

Kama nilivyowahi kuandika, usiwasaidie masikini. Kisha niliwahi kumuandikie Barua Lisu kuwa asiwatetee masikini na wajinga isipokuwa akiwa na Maslahi yake binafsi.

Upinzani nafikiri wakati huu kwao ulikuwa muhimu Sana.

SSH Hana ushawishi mkubwa kihivyo. Mlipaswa mtembee na Line hiyo Kwanza.

Kisha mtembee na makosa yanayojitokeza kama vile ishu ya Tozo za MIAMALA, suala la kukatika katika Kwa umeme, kupanda Kwa bei ya Mafuta NK.

Kwani mambo hayo ndio yanaogusa Watanzania wengi waliomasikini na wasio na elimu.

Kama mngefanya hiyo calculation hakika mngepata uungwaji Mkono na Watanzania wengi ingawaje Kama nilivyosema Watanzania wengi ni WANAFIKI lakini huenda mngeongeza Fans base ndani ya jamii.

Pia kutokana na Watanzania wengi kupenda hadithi za kufikirika na propaganda za kitoto. Hili la Chanjo ya Corona mngelipinga,
Hata Kama msingepinga wote lakini angetokea viongozi wanne wenye ushawishi walipinge Kama anavyofanya Gwajima.
Ingawaje naona ugumu Kwa upande wenu kwani wenye hizo chanjo huenda ndio wanaowafadhili.

Mnashindwa hata na Gwajima bhana. Fanyeni Calculation vizuri. Hii michezo inahitaji akili zaidi kuliko hisia.

SSH akiwashinda 2025 msitegemee Kama kuna ambaye mtamuweza.

Sababu nimeshawapa, nayo ni kuwa Hana ushawishi mkubwa ndani ya jamii kutokana na kuwa bado kuna kasumba ya mwanamke kutopewa nafasi kubwa ya uongozi.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Morogoro
 
Masikini ni watu wavivu na wajinga,hili kundi ni wanyonyaji zidi ya watu wenye akili na matajiri,kwa sababu masikini analipiwa kila kitu na tajiri, masikini hazalishi kitu wala kulipa kodi,lakini ni mtu wa kwanza kufurahia matatizo ya tajiri, na mara nyingi wana kamsemo kao ka tajiri afilisike ili tufanane,masikini hajawahi kuwa na mchango wowote nchini
 
CCM itashinda mapema maana Wapinzani bado wanafarakana badala ya kuungana ili waweze kuwarusha CCM madarakani 2025.
 
Shida siyo udhaifu wa SSH ni muundo na uhuru wa majambazi yaitwayo CCM na askariZa waliojimilikisha chama hicho.
Historia itakusaidia- Upinzani umeshinda mara nyingi ajabu

1995 Mrema Lyatonga alimgalaza Mkapa- Mfumo ukafanya yake! hatukujua sana kwa sababu uhuru wa habari ulikuwa gerezani sana na hata zanzibar Maalim alimgalagaza Salmin komandoo vibaya hadi hatua ya gazeti la majira na motomoto kutoa breakdown ya ushindi wa maalim jimbo kwa jimbo - nyerere akaongoza figisu

2000- Zanzibar tena wakaliwa kichwa na wakataka kugoma na fujo kibao hadi mauaji yakatokea na wakimbizi wa kwanza wakapatikana tz huko shimoni mombasa

2005 - Jakaya akachukua kwa kura nyingi lakini zenji figisu zikaendelea

2010- Dr Slaa akamkalagaza mkwere kwa mbali mfumo ukaingilia

2015- Lowasa akalitafuna jiwe bila huruma mfumo ukaiba kama kawaida. Zanzibar ilibidi wafute uchaguzi kumnusuru Shein ambaye alishakubali mapigo

2020- Jiwe akapondwa pondwa kabisa na kijana Antipas Lisu ikabidi waibe mchakato wa uchaguzi wote na kuachana na kura walizozoea kukwapua.

Hivyo CCM iliwahi kushinda mara moja tu! nacho ni kipindi cha kwanza cha Jakaya.

Tuache utani wapiga kura wamechoka- Dawa hapa ni katiba MPYA, Tume huru baaaaasi
Ninachowapendea wapinzani nchi hii HAWAJAWAHI kushindwa UCHAGUZI hata siku moja🤣🤣
 
Natamani mabadoliko makubwa ya utawala yayokee tukiwa na katiba mpya, CCM wanachelewa kufanya mabadiliko katika katiba lakini nyakati zaja ambapo watatolewa.Watanzania watasema heri Zimwi likujualo, na ccm watalia kusaga meno.Huu ni wakati wa CCM kutengeneza mazingira yatakayo wapa nafuu, katiba hii wakitolewa Kwa nguvu ama ya kura au maandamano itawawaumiza sana.
 
Ukweli ni kuwa kama tungekuwa na katiba ya kisasa na kuwa na tume huru ya uchaguzi ,hakuna kiongozi wa ccm angeshinda uchaguzi nchi hii
 
Shida siyo udhaifu wa SSH ni muundo na uhuru wa majambazi yaitwayo CCM na askariZa waliojimilikisha chama hicho.
Historia itakusaidia- Upinzani umeshinda mara nyingi ajabu

1995 Mrema Lyatonga alimgalaza Mkapa- Mfumo ukafanya yake! hatukujua sana kwa sababu uhuru wa habari ulikuwa gerezani sana na hata zanzibar Maalim alimgalagaza Salmin komandoo vibaya hadi hatua ya gazeti la majira na motomoto kutoa breakdown ya ushindi wa maalim jimbo kwa jimbo - nyerere akaongoza figisu

2000- Zanzibar tena wakaliwa kichwa na wakataka kugoma na fujo kibao hadi mauaji yakatokea na wakimbizi wa kwanza wakapatikana tz huko shimoni mombasa

2005 - Jakaya akachukua kwa kura nyingi lakini zenji figisu zikaendelea

2010- Dr Slaa akamkalagaza mkwere kwa mbali mfumo ukaingilia

2015- Lowasa akalitafuna jiwe bila huruma mfumo ukaiba kama kawaida. Zanzibar ilibidi wafute uchaguzi kumnusuru Shein ambaye alishakubali mapigo

2020- Jiwe akapondwa pondwa kabisa na kijana Antipas Lisu ikabidi waibe mchakato wa uchaguzi wote na kuachana na kura walizozoea kukwapua.

Hivyo CCM iliwahi kushinda mara moja tu! nacho ni kipindi cha kwanza cha Jakaya.

Tuache utani wapiga kura wamechoka- Dawa hapa ni katiba MPYA, Tume huru baaaaasi
Umenena vyema!
 
Back
Top Bottom