MAFILILI
JF-Expert Member
- Apr 28, 2011
- 2,377
- 1,194
Chama chetu kinachojipambanua kuwa ni muasisi wa demokrasia kinaendelea kujimaliza chenyewe kwa kuendesha zoezi la uteuzi ndani ya chama kugombea uongozi serikali za mitaa pasipo uwazi. Kila kiongozi wa chama akiulizwa anatoa jibu la mkato kuwa "siku ikifika mtajulishwa". Huku kuna mchezo mchafu vikao vya uteuzi vinafanyika sehemu za starehe, bar nyakati za usiku.
Dodosa zetu zimeonyesha walengwa wanaotakiwa kupata fursa za kugombea ni wazaliwa wa kanda pendwa ndani ya chama chetu. Huo ni ubaguzi kututenga Wakwere, Wamatumbi, Wandengereko na Wazaramo eti hatuna sifa za kuwakilisha CHADEMA. Uongozi wetu hapo Ufipa, muje mlifanyie kazi huku Mbagala msije mkaona wanachama wenu tulio watiifu kwa chama tukafuata demokrasia na kuunga mkono juhudi za Rais kuinyosha Tanzania!
Dodosa zetu zimeonyesha walengwa wanaotakiwa kupata fursa za kugombea ni wazaliwa wa kanda pendwa ndani ya chama chetu. Huo ni ubaguzi kututenga Wakwere, Wamatumbi, Wandengereko na Wazaramo eti hatuna sifa za kuwakilisha CHADEMA. Uongozi wetu hapo Ufipa, muje mlifanyie kazi huku Mbagala msije mkaona wanachama wenu tulio watiifu kwa chama tukafuata demokrasia na kuunga mkono juhudi za Rais kuinyosha Tanzania!