Huku kujitenga kuepusha maambukizi ya corona ni Mungu tu atusaidie

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,597
215,272
Ninaishi Kwa Mtogole, nyumba tunayoishi tuko familia tano, wastani kila familia ina watu watano. Wote tunatumia choo kimoja. Mlango wa chooni ni gunia.

Mimi ninafanya kazi za kusafisha mji, mume wangu dereva wa daladala. Anaokutana nao huko anajua mwenyewe na mimi ninaokutana nao nikiwa na fagio langu ni wengi.

Jioni mimi na baba chanja tunajitenga na watoto wanalala chumbai kwao. Nyumba nzima tunachota maji kwa mwenyekiti wa mtaa ndoo ni shilingi mia.

Hayo maji ya kutiririka tunayaona kwenye Bongo Movie. Sisi tunanawa kwenye beseni.

Wataalamu wanasema tusafishe vitasa vya milango, chooni kwetu hakuna kitasa. Ukitaka aliyeko ndani ajue kuna mtu, ana kohoa.

Wanasema tutumie maji ya kutiririka. Imebidi ninunue jagi Kariakoo, watoto wanaosha mikono kwa kushikiana jagi kwa zamu.
 
Bado subiria ipitishwe sheria ya kila mwananchi kujiweka karantini nyumbani kweke mwezi mzima hamna kutoka nje.
Hii ndo raha ya kuzaliwa shithole kantris.
 
Wa kwamtogole wanachangamoto lakini wamasaki baba anajifanya amiweka karantini kumbe yuko na Mzigua hotel nyota 5

Sent using Jamii Forums mobile app
Screenshot_20200317_192710.jpg
 
Bado subiria ipitishwe sheria ya kila mwananchi kujiweka karantini nyumbani kweke mwezi mzima hamna kutoka nje.
Hii ndo raha ya kuzaliwa shithole kantris.
It won't happen. How does that work in Manzese, Mburahati, Kigogo, Mbagala etc.?
 
Ninaishi Kwa Mtogole, nyumba tunayoishi tuko familia tano, wastani kila familia ina watu watano. Wote tunatumia choo kimoja. Mlango wa chooni ni gunia.

Mimi ninafanya kazi za kusafisha mji, mume wangu dereva wa daladala. Anaokutana nao huko anajua mwenyewe na mimi ninaokutana nao nikiwa na fagio langu ni wengi.

Jioni mimi na baba chanja tunajitenga na watoto wanalala chumbai kwao. Nyumba nzima tunachota maji kwa mwenyekiti wa mtaa ndoo ni shilingi mia.

Hayo maji ya kutiririka tunayaona kwenye Bongo Movie. Sisi tunanawa kwenye beseni.

Wataalamu wanasema tusafishe vitasa vya milango, chooni kwetu hakuna kitasa. Ukitaka aliyeko ndani ajue kuna mtu, ana kohoa.

Wanasema tutumie maji ya kutiririka. Imebidi ninunue jagi Kariakoo, watoto wanaosha mikono kwa kushikiana jagi kwa zamu.
Hata hapo Ufipa hali ni hiyo hiyo manka.......choo kimoja!
 
Huku kwetu Africa ni vigumu Sana maana tukijifungia ndani bila kutoka nje njaa itatuua.
 
Ninaishi Kwa Mtogole, nyumba tunayoishi tuko familia tano, wastani kila familia ina watu watano. Wote tunatumia choo kimoja. Mlango wa chooni ni gunia.

Mimi ninafanya kazi za kusafisha mji, mume wangu dereva wa daladala. Anaokutana nao huko anajua mwenyewe na mimi ninaokutana nao nikiwa na fagio langu ni wengi.

Jioni mimi na baba chanja tunajitenga na watoto wanalala chumbai kwao. Nyumba nzima tunachota maji kwa mwenyekiti wa mtaa ndoo ni shilingi mia.

Hayo maji ya kutiririka tunayaona kwenye Bongo Movie. Sisi tunanawa kwenye beseni.

Wataalamu wanasema tusafishe vitasa vya milango, chooni kwetu hakuna kitasa. Ukitaka aliyeko ndani ajue kuna mtu, ana kohoa.

Wanasema tutumie maji ya kutiririka. Imebidi ninunue jagi Kariakoo, watoto wanaosha mikono kwa kushikiana jagi kwa zamu.

Mie nasema baada kumaliza janga la corona hizi hospitali zisafishwe vizuri ziandaliwe kuzalisha watoto disemba na january.

Haya mambo ya watu kukaa ndani na kujitenga hamna zaidi la kufanya ni kutengeneza watoto tu.
 
Ninaishi Kwa Mtogole, nyumba tunayoishi tuko familia tano, wastani kila familia ina watu watano. Wote tunatumia choo kimoja. Mlango wa chooni ni gunia.

Mimi ninafanya kazi za kusafisha mji, mume wangu dereva wa daladala. Anaokutana nao huko anajua mwenyewe na mimi ninaokutana nao nikiwa na fagio langu ni wengi.

Jioni mimi na baba chanja tunajitenga na watoto wanalala chumbai kwao. Nyumba nzima tunachota maji kwa mwenyekiti wa mtaa ndoo ni shilingi mia.

Hayo maji ya kutiririka tunayaona kwenye Bongo Movie. Sisi tunanawa kwenye beseni.

Wataalamu wanasema tusafishe vitasa vya milango, chooni kwetu hakuna kitasa. Ukitaka aliyeko ndani ajue kuna mtu, ana kohoa.

Wanasema tutumie maji ya kutiririka. Imebidi ninunue jagi Kariakoo, watoto wanaosha mikono kwa kushikiana jagi kwa zamu.
Kwani umesharudi toka kwa mabeberu??
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom