Huko majuu, Canada, makenikia yameleta balaa...... !

Jidu La Mabambasi

JF-Expert Member
Oct 20, 2014
15,169
23,860
Kutoka kwa mpekuzi was Sukununu huko Montreal, Canada,

Wakuu nawasalimu,

Juzi niliandika uzi huu Vita dhidi ya mabepari wa madini inahitaji umoja, ilimshinda Dr Williamson wa Mwadui na Mwl Nyerere nikiwa Toronto Canada,hapo nilikuwa nyumbani kwa Mzee mmoja aliyeishi Mwadui miaka ya 1970's kabla ya kuondoka na kurudi huku.

Alinipa habari nyingi sana za "fitna" za mabepari wa madini katika dunia hii.Tunapaswa kuungana katika vita hivi,tusimuache Rais peke yake,na wala Rais asiibebe vita hii peke yake.

Leo ninapata ujumbe kuwa "Executive Chairman" wa Barrick Gold Corporation Mr.Thornton John Lawson ametua Tanzania usiku kwa usiku ili kuja kutuliza mambo.

Hali ya hapa Canada kwa Barrick sio nzuri,wanaharakati na wanasiasa wameanza kuandaa hoja za kuishutumu Barrick(Acacia) kwa "hujuma" walizoifanyia Tanzania toka mwaka 1998.

Kiukweli sakata hili la Tanzania na Accacia sio dogo tena,ni mgogoro mkubwa sana katika ulimwengu wa biashara na mashauriano ya kigeni.Kama nilivyosema juzi katika uzi ule,hii ni vita,ni vita kati ya Rais yeye binafsi na hawa mabepari wa madini,na ni vita kati ya Tanzania kama nchi na makampuni haya.TUSHIKAMANE.

Hata Rais jana alisema,yeye naye ni binadamu,ana damu na nyama,anajua kuwa anapigana na watu wenye nguvu za kiuchumi duniani,tumuombee na tumpe ushirikiano.

Safari ya Mr.Thornton kuja Tanzania ina maana kubwa sana katika kufikia mwisho wa "mgogoro" huu kati ya sisi kama Taifa na kampuni ya Barrick.

Ripoti ya pili ya kamati ya Rais iliishitua sana management ya kampuni ya Accacia na kuamuru Executive Chairman apande ndege na kuja Tanzania kuweka mambo sawa.

Hisa za Barrick katika masoko ya hisa makubwa duniani kama LSE,NYSE,Australia nk yameshuka kwa kiwango kikubwa sana.Tahadhari inahitajika mapema kwa kumuona Rais na kuweka mambo sawa.

Wakati tukiendelea kujua huko nyumbani,ni nini haswa Mr.Thornton ataongea au hata kupewa nafasi ya kumuona Rais,basi tujue huyu Mr.Thornton J. Lawson ni nani hasa??

Mr. Thornton was appointed Chairman of Barrick on April 30, 2014. From June 5, 2012 to April 29, 2014, Mr. Thornton was Co-Chairman of Barrick. He is also Non-Executive Chairman of PineBridge Investments, a global asset manager.

He is also a Professor, Director of the Global Leadership Program, and Member of the Advisory Board at the Tsinghua University School of Economics and Management in Beijing.

He is also Co-Chairman of the Board of Trustees of the Brookings Institution in Washington, D.C. He retired in 2003 as President and a member of the board of the Goldman Sachs Group.

Huyu ndio Chief Chairman wa Barrick Gold Corporation,mtikisiko wa ripoti ya Rais toka Ikulu ya Magogoni,umetikisa mpaka ardhi na viunga vya London,New York,Toronto na Paris.Tungoje na tusubiri.

Naomba kuwasilisha, as received
True ila from different source, ambayo nayo inaelekea ilikucopy!
Talk of a small world!
Hata hivyo heshima kwko, true source, barafu!
 
Kuna watu wanapatia umaarufu habari tunazoleta humu...Kuna kundi moja la WhatsApp wamebeba habari niloyoleta kuhusu Dr Williamson wa Mwadui,na aliyeileta ndio akasema kaandika yeye...Inashangaza!!

Lakini ni furaha kuwa ujumbe tunaotoa na makala tunazoandika zinawafikia watu kwa wingi,kupitia vidole vya mikono yetu,vipaji na fursa tulizonazo...Mungu mkuu anatukuzwa
 
Kuna watu wanapatia umaarufu habari tunazoleta humu...Kuna kundi moja la WhatsApp wamebeba habari niloyoleta kuhusu Dr Williamson wa Mwadui,na aliyeileta ndio akasema kaandika yeye...Inashangaza!!

Lakini ni furaha kuwa ujumbe tunaotoa na makala tunazoandika zinawafikia watu kwa wingi,kupitia vidole vya mikono yetu,vipaji na fursa tulizonazo...Mungu mkuu anatukuzwa
Ni muhimu akasema ni barafu ndiye mwandishi. Ila nakupongeza na kukuamini sana na maandiko yako. Naomba kwa niaba ya wengine utuletee angalau kwa muhtasari yanayojiri katika magazeti ya huko kuhusu hili suala. Nikushukuru kwa mara nyingine na hata ile ya ATCL maana wengi washalianzisha
 
Jibu ni kwamba watataka uchunguzi huru ili wajisafishe na si kukubali hizi data zinazowachafua na wakilipa maana yake wanakiri hii hujuma hivyo tusitarajie watakubali kirahisirahisi tu kulipa maana hii itakuwa ni damage kwao.
Bavicharian propaganda!
 
Alichokisema Mwenyekiti wa Barrick Prof Thornton leo. Najaribu kutafuta aliposema kwamba watalipa pesa yote trilion 100 sijapaona,atakayepaona aniite
............................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................ ''I have come here in order to help resolve the problem and I assure the President that we are interested in sitting down and reaching a resolution which is a win win (A win for Tanzania and a win for Barrick and our Subsidiary company, ACACIA)

After having these extensive conversations I feel very optimistic that we will reach a resolution which is a win win for all parties and we will be sitting down soon with a team designated by the President and our own team to go through the detail of that and I feel very good about the progress today.''
 
Kutoka kwa mpekuzi was Sukununu huko Montreal, Canada,

Wakuu nawasalimu,

Juzi niliandika uzi huu Vita dhidi ya mabepari wa madini inahitaji umoja, ilimshinda Dr Williamson wa Mwadui na Mwl Nyerere nikiwa Toronto Canada,hapo nilikuwa nyumbani kwa Mzee mmoja aliyeishi Mwadui miaka ya 1970's kabla ya kuondoka na kurudi huku.

Alinipa habari nyingi sana za "fitna" za mabepari wa madini katika dunia hii.Tunapaswa kuungana katika vita hivi,tusimuache Rais peke yake,na wala Rais asiibebe vita hii peke yake.

Leo ninapata ujumbe kuwa "Executive Chairman" wa Barrick Gold Corporation Mr.Thornton John Lawson ametua Tanzania usiku kwa usiku ili kuja kutuliza mambo.

Hali ya hapa Canada kwa Barrick sio nzuri,wanaharakati na wanasiasa wameanza kuandaa hoja za kuishutumu Barrick(Acacia) kwa "hujuma" walizoifanyia Tanzania toka mwaka 1998.

Kiukweli sakata hili la Tanzania na Accacia sio dogo tena,ni mgogoro mkubwa sana katika ulimwengu wa biashara na mashauriano ya kigeni.Kama nilivyosema juzi katika uzi ule,hii ni vita,ni vita kati ya Rais yeye binafsi na hawa mabepari wa madini,na ni vita kati ya Tanzania kama nchi na makampuni haya.TUSHIKAMANE.

Hata Rais jana alisema,yeye naye ni binadamu,ana damu na nyama,anajua kuwa anapigana na watu wenye nguvu za kiuchumi duniani,tumuombee na tumpe ushirikiano.

Safari ya Mr.Thornton kuja Tanzania ina maana kubwa sana katika kufikia mwisho wa "mgogoro" huu kati ya sisi kama Taifa na kampuni ya Barrick.

Ripoti ya pili ya kamati ya Rais iliishitua sana management ya kampuni ya Accacia na kuamuru Executive Chairman apande ndege na kuja Tanzania kuweka mambo sawa.

Hisa za Barrick katika masoko ya hisa makubwa duniani kama LSE,NYSE,Australia nk yameshuka kwa kiwango kikubwa sana.Tahadhari inahitajika mapema kwa kumuona Rais na kuweka mambo sawa.

Wakati tukiendelea kujua huko nyumbani,ni nini haswa Mr.Thornton ataongea au hata kupewa nafasi ya kumuona Rais,basi tujue huyu Mr.Thornton J. Lawson ni nani hasa??

Mr. Thornton was appointed Chairman of Barrick on April 30, 2014. From June 5, 2012 to April 29, 2014, Mr. Thornton was Co-Chairman of Barrick. He is also Non-Executive Chairman of PineBridge Investments, a global asset manager.

He is also a Professor, Director of the Global Leadership Program, and Member of the Advisory Board at the Tsinghua University School of Economics and Management in Beijing.

He is also Co-Chairman of the Board of Trustees of the Brookings Institution in Washington, D.C. He retired in 2003 as President and a member of the board of the Goldman Sachs Group.

Huyu ndio Chief Chairman wa Barrick Gold Corporation,mtikisiko wa ripoti ya Rais toka Ikulu ya Magogoni,umetikisa mpaka ardhi na viunga vya London,New York,Toronto na Paris.Tungoje na tusubiri.

Naomba kuwasilisha, as received
Umekopi uzi wa Barafu.
 
Jibu ni kwamba watataka uchunguzi huru ili wajisafishe na si kukubali hizi data zinazowachafua na wakilipa maana yake wanakiri hii hujuma hivyo tusitarajie watakubali kirahisirahisi tu kulipa maana hii itakuwa ni damage kwao.
Mbona wamekubali kulipa?
 
Jibu ni kwamba watataka uchunguzi huru ili wajisafishe na si kukubali hizi data zinazowachafua na wakilipa maana yake wanakiri hii hujuma hivyo tusitarajie watakubali kirahisirahisi tu kulipa maana hii itakuwa ni damage kwao.

Nadhani udakiaji wa mambo, pasipo kufikiri, umekuumbua baada ya kumsikia mmiliki mwenyewe alichokisema leo, tofauti kabisa na uzushi wako (maandishi mekundu kwenye nukuu hapo juu)!!
 
13 Reactions
Reply
Back
Top Bottom