Uchaguzi 2020 Hujuma dhidi ya CHADEMA na wapinzani kwa ujumla, ni matokeo ya uvumilivu wa wapinzani unaotafsiriwa kimakosa kama uoga

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
46,996
144,329
Huu ndio ukweli ambao wapinzani tunapaswa kuutafakari na kuchukua hatua sahihi. Wameengua wagombea wa upinzani tukaa kimya, wakatuchukila poa, lakini kama tungesimama imara, leo hizi figisu za kuapisha mawakala pengine zisingetokea.

Tusisahau walianza katika zile chaguzi za marudio zilizotokana na watu kuunga mkono juhudi, kisha yakajirudia katika uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka jana mwishoni, na sasa kuna kila dalili yanakwenda kujitokeza tena katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.

Kuna msemo: maneno huumba, ila leo naomba niongeze kwa kusema,"uvumilivu pia huumba/huzaa mazoea".

Tuseme enough is enough kwa vitendo.
 
Hakuna kazi kubwa na ngumu km kuwaingiza watanzania barabaran, nadhani baada ya uchaguzi LISSU atalielewa hili.
 
Watu wamehamasika vibaya mno, hivyo ,lolote laweza tokeoa mwaka huu na tukaandika historia mpya katika nchi hii.
miaka 5 ya mateso,mtu anataka alazimishe wabunge na madiwani wa chama chake either washinde au wasishinde et lazima watangezwe hapana,tusipoamka nw jamaa anaenda kutunyanyasa sana miaka 5 inayokuja so hyo ck hakuna kulala aisee
 
Umeona kilichotokea Songwe na Musoma Leo? Endeleeni tu kuishi kwa kukariri mwaka huu ndo mtajua kuwa hamjui dadeki.
Huna lolote, mwenye chama mwenyewe mwoga kama kunguru ndio muwe ninyi washabiki.. Mbowe na genge lake watatumia njaa zenu kuwatanguliza, hapo ndio mtajuta. Jitekenyeni tu.
 
Huna lolote, mwenye chama mwenyewe mwoga kama kunguru ndio muwe ninyi washabiki.. Mbowe na genge lake watatumia njaa zenu kuwatanguliza, hapo ndio mtajuta. Jitekenyeni tu.
Hakuna wa kujuta. Ni Heri tuumie sisi ili vizazi na vizazi vya Tanzania vipone na udhalimu wa Ccm!
 
Huu ndio ukweli ambao wapinzani tunapaswa kuutafakari na kuchukua hatua sahihi. Wameengua wagombea wa upinzani tukaa kimya, wakatuchukila poa, lakini kama tungesimama imara, leo hizi figisu za kuapisha mawakala pengine zisingetokea.

Tusisahau walianza katika zile chaguzi za marudio zilizotokana na watu kuunga mkono juhudi, kisha yakajirudia katika uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka jana mwishoni, na sasa kuna kila dalili yanakwenda kujitokeza tena katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.

Kuna msemo: maneno huumba, ila leo naomba niongeze kwa kusema,"uvumilivu pia huumba/huzaa mazoea".

Tuseme enough is enough kwa vitendo.
Wananchi wako tayari kabisa yaani kama ni jipu limeiva! Wanakosa wa kuwaongoza tu! Hizi tambo za kina Ali Bananga zinatakiwa ziwekwa vitendo. Leo hii kungekuwa na mkurugenzi amegawanwa na wananchi huu ujinga usingekuwapo! Tufike mahali tuseme ile "sasa basi" iwe kwa vitendo! Leo tumeishia kusemasema tu lakini nawaambia mtiti unakuja kwenye kuruhusiwa kuingia kwenye vituo! Tutalia na kusaga meno. Tundu Lissu anatakiwa ataagiza raia siku ya kupiga kura waviteke vituo vyote mpaka mawakala waruhusiwe au kama sivyo tumgawane msimamizi mmoja ili kutoa onyo! Polisi watajigawaje kwa nchi nzima hii? Wanajeshi walishachoka lazima watakuwa upande wa wananchi!
 
Huna lolote, mwenye chama mwenyewe mwoga kama kunguru ndio muwe ninyi washabiki.. Mbowe na genge lake watatumia njaa zenu kuwatanguliza, hapo ndio mtajuta. Jitekenyeni tu.
Naona ndo unaanza kufuatilia leo chaguzi za tz eti?ukiona mbunge wa upinzani katangazwa sio lele mama watu wamepambana hii imefanyika 2010, 2015 so watu wanaongea kwa experience subiri uone
 
Dr. Slaa ndio alikuwa na uwezo wa kupeleka watu barabarani sio hawa mabwabwa. Kwa njaa zenu,watawabagaza kwelikweli.
 
miaka 5 ya mateso,mtu anataka alazimishe wabunge na madiwani wa chama chake either washinde au wasishinde et lazima watangezwe hapana,tusipoamka nw jamaa anaenda kutunyanyasa sana miaka 5 inayokuja so hyo ck hakuna kulala aisee
Magufuli ndiye Rais wa Tanzania. Kula malimao kabisaaa.
 
Hakuna kazi kubwa na ngumu km kuwaingiza watanzania barabaran, nadhani baada ya uchaguzi LISSU atalielewa hili.
Kwa aina ya watu kama wewe !!. Unashangaa nini miaka 60 ya uhuru wetu nchi ni masikini ya kutupa !!.

Lissu aweza kushindwa uchaguzi kwa haki au kwa figisu. Lakini aliyoyafanya wewe huwezi kuthubutu. Endelea kusifu na kuabudu
 
Back
Top Bottom