Hujafa Hujaumbika...!

PakaJimmy

JF-Expert Member
Apr 29, 2009
16,203
8,720
Jana nililazimika kumtembelea huyu rafiki yangu, amelazwa pale Hospitali kuu ya Rufaa ya KCMC.
Yuko ICU.
Yuko hoi bin taaban. Mtu mwoga hutamtazama kwa sekunde 10!
Mipira kadha imeingizwa mwilini kupitia puani.
Haongei, hasogezi kiungo, hatazami.
Ngozi yote ya asili ya mwili wake imeumuka, imetoka, kama vile amemwagiwa uji wa moto, au kama mnyama aliyechunwa ngozi, tayari kwa kitoweo!
Kwa ufupi, ni kwamba hawezi, anasikitisha!

Ni mwajiriwa wa TANAPA, ni dereva.
Jumatano iliyopita23/2/2010 ilikuwa asafiri kuwapeleka wakuu wake kwenda Mkoa wa Pwani kwaajili ya vikao, lakini jumanne yake ghafla alianza kuumwa sana.
Akakimbizwa Seliani Hospitali, ambapo walipomwangalia, moja kwa moja walimpa rufaa ya KCMC baada ya kuona ugonjwa wake si wa kawaida, na anabadilika kwa kasi ya ajabu kila sekunde zinapoongezeka, anakuwa critical!

Kwa mujibu wa ndugu zake, madaktari hawajagundua ugonjwa, zaidi ya kususpect allergy!

Tukiwa hapo Hospitali, kama kawaida kila anayeingia kumwona akitoka anasema lake!..Lakini kilichonivuta ni kauli za wengi wakisema :
-Safari iliyokuwa afanye huyu ndugu, kuwapeleka wakuu wake Pwani ndiyo inayomponza!
-Wengine wakisema, ni gari jipya alilokabidhiwa aliendeshe, ndo linalommaliza!

Mimi si muumini wa uSHIRIKINA, lakini kauli na simulizi za watu hawa zinatisha!
Wadau niambieni, kuna ukweli gani katika dhana nzima ya kauli kama hizi?

 
Poleni sana jamani.Ungekuwa DSM ningekwambia kamuulize sheikh yahya!!
 
Poleni sana jamani.Ungekuwa DSM ningekwambia kamuulize sheikh yahya!!
Mkuu Bulesi,
Du hii ni kali tena!...Uko serious?
Unamwamini kisa alitangaza kwamba atakayegombea na Kikwete atakufa?..au kuna sababu zingine.
 
Husiweke thanks kwenye maandiko yangu, nimepokea za Invisible na hansomeboy pekee kwa heshima zao hapa JF. Sitaki nyingine

Hiyo ni signature ya bwana PAZIA (hapo juu).
Tuheshimu matakwa yake PLZ!
 
Kwa kweli ushirikiana especially kwa madereva na wengine wenye kazi za kipato kidogo upo kabisa.Nakumbuka kuna dereva mmoja wa serikali alikuwa anamuenda mnene mmoja.Yule bwana kila siku alikuwa kwenye gari yake anachoma ubani na kunuia nia zake azijuazo mwenyewe.Binafsi si muuumin wa USHIRIKIANA ila haya mambo yapo na mtu hulazimishwi kuyakubali mpaka yatakapokutokea.
Pole sana kwa maswahibu yaliyomkumba huyo dereva
 
Duh Pole sana ndugu!

Kwani madaktari hapo KCMC wameshindwa kutambua kabisa ni ugonjwa gani?!
Kama wanasema ni allergy, huwa kuna sindano unachomwa ambayo baada ya half an hour unaanza kuona matokeo, amechomwa hyo sindano?!

Kama hawaoni kitu na jamaa anazidi kuzidiwa itabidi mumpeleke kwenye maombi ya kweli, kama watu wa Charismatic Catholic wapo pande hizo nashauri muwaombe wawasaidie, au Mwakasege?! All in all, itabd aombewe big time kama hospitalini hawataona chochote!

Kwasasa jipeni moyo na kuamini kuwa ni allergy au ugonjwa wa kawaida, tusikimbilie kuwa kachezewa...
 
Mimi si muumini wa uSHIRIKINA, lakini kauli na simulizi za watu hawa zinatisha!
Wadau niambieni, kuna ukweli gani katika dhana nzima ya kauli kama hizi?
wala USIJARIBIWE KIIMANI mkuu PIIJEEII!nakuombea kwa mwenyezi mungu AKUKINGE NA YULE MWOVU!...nduguyo ANAUMWA ALERG YA KAWAIDA TU.....they will need sometimes to gundua it!

POLE SANA MNDUGU!mpe pole na nduguyo...!

YOTE YAWEZEKANA KWA IMANI,YOTE YAWEZEKANA KWA IMANI
 
mleteni hapa ufufuo na uzima ubungo, ndani ya mda mfupi atapokea uponyaji

Huyu mgonjwa si wa kubebwa na kusafirishwa, kama nimemuelewa vema PJ. Kwani hapo kanisani hamuwezi kumuombea akapona akiwa kulekule? Hakuna waumini wa kanisa lenu kule Moshi wamwombee?
Ughwe Nnyambala bhule bhule?
 
Hiyo ni signature ya bwana PAZIA (hapo juu).
Tuheshimu matakwa yake PLZ!
Haswaaa!!!
Ila huyo mgonjwa jaribuni kumpeleka pale YMCA kuna dokta mmoja ni mtaalamu sana wa masuala ya mzio(allergy)

Pia msidharau dawa za kienyeji, zinahusika sana, sijasema mkapige ramli, la hasha
 
Kuna mijitu haijui hii msemo "hujafa hujaumbika" wanajiona wao ndio wao ndio mwisho wa dahari.
 
Ndugu kama unaamini Mungu yupo,pia amini uchawi upo na mtu anaweza kurogwa.Cha msingi aendelee kuwa hapo hospitalini,mara kwa mara walokole hupita hapo kuwaombea wagonjwa.Hakuna sekta inayoongoza kwa kurogana kama madereva wa kitanzania.
 
Ndugu kama unaamini Mungu yupo,pia amini uchawi upo na mtu anaweza kurogwa.Cha msingi aendelee kuwa hapo hospitalini,mara kwa mara walokole hupita hapo kuwaombea wagonjwa.Hakuna sekta inayoongoza kwa kurogana kama madereva wa kitanzania.
Actually kuna myth nyingi sana juu ya mienendo mibaya ya kishirikina ya madereva!..

Nilipata kuambiwa kuwa kuna dereva mmoja anapokaribia kwenda likizo gari yake inaharibika na kuwa grounded hadi atakapomaliza likizo, na anakuja kuiendesha mwenyewe!!

Sijui mambo haya yanaashiria nini!
 
Huyu mgonjwa si wa kubebwa na kusafirishwa, kama nimemuelewa vema PJ. Kwani hapo kanisani hamuwezi kumuombea akapona akiwa kulekule? Hakuna waumini wa kanisa lenu kule Moshi wamwombee?
Ughwe Nnyambala bhule bhule?
Huyu mgonjwa habebeki, kwa ufupi maneno ya kamusi ya kiswahili hayatoshi kuelezea hali anayoipitia huyu ndugu!

Kama alivyosema Mkuu Idimi, nami nijuavyo mimi ni kwamba Nguvu za Mungu hazina mipaka, wala mkoa wala kabila!..Zinatenda kazi kwa sala tu!

Hivyo, watu wa Mungu popote mlipo, tumwombee huyu mtu ili aponywe, mtabarikiwa sana!
 
mungu wa mbinguni aishie milele amponye kwa jina la yesu.. Amen
Amen!!! Napenda watu wanaomtanguliza MUNGU kwenye maisha yao!!! PakaJimmy kuwa na uhakika kuwa huyo mgonjwa wako amepona kwa maombi haya ya hapa yanatoa tumaini. YESU KRISTO NI MPONYAJI NA ANASIKIA MAOMBI YA WATU WANAOMAANISHA!!! Glory to GOD
 
Amen!!! Napenda watu wanaomtanguliza MUNGU kwenye maisha yao!!! PakaJimmy kuwa na uhakika kuwa huyo mgonjwa wako amepona kwa maombi haya ya hapa yanatoa tumaini. YESU KRISTO NI MPONYAJI NA ANASIKIA MAOMBI YA WATU WANAOMAANISHA!!! Glory to GOD
Naamini kabisa!..AMEEN!
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom