GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,518
- 108,793
Nadhani kama kuna Watu ambao sasa hivi huko waliko na kama ni Marehemu basi Mizimu yao inaumia na hata Kuchukia basi watakuwa ni Walimu, Wakufunzi na Wahadhiri waliopata Bahati mbaya ya Kumfundisha Spika wa Bunge wa sasa Ndugu Job Ndugai. Na nawapa pole Kubwa sana tu.
Ni Mpumbavu ( Mduduna ) tu pekee ndiyo atakubalina na Uamuzi wa Kiduduna ( Kipumbavu ) uliofanya na Spika Job Ndugai jana Bungeni kwa Kutangaza kuwa Kiti cha Mbunge Tundu Lissu sasa kipo wazi kwa sababu zake Dhaifu kabisa alizozitoa ambazo katika Vichwa vya Watu wenye Akili wala hazina Mashiko n asana sana ndiyo tunazidi Kumdharau kama siyo Kumpuuza Spika pamoja na wale wanaomtuma.
Sipo hapa Kumtetea Tundu Lissu japo na Yeye kama Mwanadamu na Mwanasiasa ana Mapungufu yake kadhaa ya Msingi ila nadhani kama tukisema tuangalie Haki, tumuogope Mwenyezi Mungu na tutangulize Ubinadamu pia basi Maamuzi dhidi yake ( Tundu Lissu ) ni ya Kiuonevu na yamejaa Ukatili, Uswahili na Unafiki uliokubuhu kabisa.
Ukiangalia Mazingira yote hakuna mahala ambapo Spika Ndugai ama alikuwa hajui alipo Tundu Lissu au amekumbwa na nini na bahati mbaya sana kuna hata Kauli zake Spika Ndugai alizowahi Kuzitoa juu ya Ugonjwa wa Tundu Lissu leo hii zinamgharimu kwa Kumuumbua na ndipo hapa nasema kwamba huenda leo hii Walimu, Wakufunzi na Wahadhiri wa Spika Ndugai wakawa wanalia au wanajificha kwa Aibu Kubwa.
Sitaki kuamini kwa sasa ila kama haya Maamuzi ya Kiduduna ( Kipumbavu ) ya Spika Ndugai yana Baraka zote kutoka Ngazi ya Serikali Kuu ( Executive ) inayoongozwa na Chama Cha Mapinduzi ( CCM ) wakiwa na Malengo yao Hasi na Tundu Lissu nadhani basi watakuwa wamejiandikishia Dhambi Kubwa sana katika Kitabu cheusi cha Mwenyezi Mungu kule Mbinguni na huenda Mwenyezi Mungu akawapa Laana moja mbaya na kubwa mno ambayo itakuja Kuwatesa hadi Pumzi zao za mwisho hapa duniani.
Katika hili ( Maamuzi haya ya Spika Ndugai ) wala huhitaji na Wewe sijui kuwa Wakili Msomi kuweza Kujua kuwa Spika Ndugai na hao waliomtuma wamechemsha tena vibaya sana tu juu ya Kutangaza Kumvua Ubunge Tundu Lissu. Na ninachojua Mimi kama Tundu Lissu akiamua Kujitetea mwenyewe na akisaidiwa pia na Mawakili wengine Wabobezi kuna hatari ya Serikali / Bunge la Tanzania Kuumbuka na kujikuta Tundu Lissu anashinda na Wao wakaishia kubaki tu Midomo wazi.
Kwa wenye Akili Kubwa na pana ambazo muda wote zinafanya Kazi ipasavyo tumegundua ya kwamba haya Maamuzi yamekuja sasa kwakuwa tayari kuna Watu waliotumwa kufanya Utafiti huko Jimboni kwa Tundu Lissu ili kupima kama pamoja na Kuugua Kwake hivi anakubalika au hapana na kila Ripoti ikipelekwa jibu linakuwa kwamba hata Lissu apambanishwe na nani huko Jimboni Kwake bado tu atashinda Ubunge hivyo wameamua Kummaliza mapema mwaka huu ili wamuandae Mtu wao ambaye watamuweka kwa Kipindi hiki cha Mpito kisha watamuwezesha Kifedha na Kuungwa mkono ili afanye Maendeleo ya haraka huko Jimboni kwa Lissu ili ateke Akili za wana Jimbo kusudi hadi mwakani Kipindi cha Uchaguzi awe ameshajulikana na kukubalika na wengi kisha agombee tena na apite Kiurahisi na ikibidi hata kwa Nguvu / Mabavu.
Nina mengi bado ya Moyoni ila kwa sasa nimalizie tu kwa Kumshauri Tundu Lissu kuwa hata kama ameamua kuwa anarudi Tanzania hiyo tarehe aliyotaja na Mwezi alioutaja ila namuomba sana awe makini kuliko alivyokuwa huko nyuma na ingekuwa ni Mimi basi kwa huu Upepo na hizi dalili zote za Kikatili na Hujuma Tanzania si sehemu salama tena Kwake na kama angeweza basi angetafuta tu hata Ukimbizi wa Kisiasa nje ya Tanzania au aombe tu kuwa Mhadhiri wa Masuala ya Kisheria Vyuo Vikuu vya Nje ( Ulaya ) na hata Marekani kwani najua kwa IQ yake iliyo Kubwa anauwezo huo au anaweza akajihusisha na Mashirika mbalimbali ya Haki za Binadamu duniani na bado tu akaendelea Kuishi. Simshauri arejee Tanzania hii kwa sasa kwani naiona Hatari Kubwa ya Kiuhai mbele yake kutoka kwa wale wale Watu wasiojulikana ambao sina uhakika kama nao walishauwawa baada Kushindwa Jaribio walilopewa la Kumuondoa au walirudishwa tena Mafunzoni ili Tundu Lissu akirejea Tanzania basi safari hii wasikosee kabisa Target na wahakikishe wanammaliza na kubaki Historia.
Kwa leo yangu ni haya tu ila Tanzania ya leo inanisikitisha na hata kuniliza Machozi.
Ni Mpumbavu ( Mduduna ) tu pekee ndiyo atakubalina na Uamuzi wa Kiduduna ( Kipumbavu ) uliofanya na Spika Job Ndugai jana Bungeni kwa Kutangaza kuwa Kiti cha Mbunge Tundu Lissu sasa kipo wazi kwa sababu zake Dhaifu kabisa alizozitoa ambazo katika Vichwa vya Watu wenye Akili wala hazina Mashiko n asana sana ndiyo tunazidi Kumdharau kama siyo Kumpuuza Spika pamoja na wale wanaomtuma.
Sipo hapa Kumtetea Tundu Lissu japo na Yeye kama Mwanadamu na Mwanasiasa ana Mapungufu yake kadhaa ya Msingi ila nadhani kama tukisema tuangalie Haki, tumuogope Mwenyezi Mungu na tutangulize Ubinadamu pia basi Maamuzi dhidi yake ( Tundu Lissu ) ni ya Kiuonevu na yamejaa Ukatili, Uswahili na Unafiki uliokubuhu kabisa.
Ukiangalia Mazingira yote hakuna mahala ambapo Spika Ndugai ama alikuwa hajui alipo Tundu Lissu au amekumbwa na nini na bahati mbaya sana kuna hata Kauli zake Spika Ndugai alizowahi Kuzitoa juu ya Ugonjwa wa Tundu Lissu leo hii zinamgharimu kwa Kumuumbua na ndipo hapa nasema kwamba huenda leo hii Walimu, Wakufunzi na Wahadhiri wa Spika Ndugai wakawa wanalia au wanajificha kwa Aibu Kubwa.
Sitaki kuamini kwa sasa ila kama haya Maamuzi ya Kiduduna ( Kipumbavu ) ya Spika Ndugai yana Baraka zote kutoka Ngazi ya Serikali Kuu ( Executive ) inayoongozwa na Chama Cha Mapinduzi ( CCM ) wakiwa na Malengo yao Hasi na Tundu Lissu nadhani basi watakuwa wamejiandikishia Dhambi Kubwa sana katika Kitabu cheusi cha Mwenyezi Mungu kule Mbinguni na huenda Mwenyezi Mungu akawapa Laana moja mbaya na kubwa mno ambayo itakuja Kuwatesa hadi Pumzi zao za mwisho hapa duniani.
Katika hili ( Maamuzi haya ya Spika Ndugai ) wala huhitaji na Wewe sijui kuwa Wakili Msomi kuweza Kujua kuwa Spika Ndugai na hao waliomtuma wamechemsha tena vibaya sana tu juu ya Kutangaza Kumvua Ubunge Tundu Lissu. Na ninachojua Mimi kama Tundu Lissu akiamua Kujitetea mwenyewe na akisaidiwa pia na Mawakili wengine Wabobezi kuna hatari ya Serikali / Bunge la Tanzania Kuumbuka na kujikuta Tundu Lissu anashinda na Wao wakaishia kubaki tu Midomo wazi.
Kwa wenye Akili Kubwa na pana ambazo muda wote zinafanya Kazi ipasavyo tumegundua ya kwamba haya Maamuzi yamekuja sasa kwakuwa tayari kuna Watu waliotumwa kufanya Utafiti huko Jimboni kwa Tundu Lissu ili kupima kama pamoja na Kuugua Kwake hivi anakubalika au hapana na kila Ripoti ikipelekwa jibu linakuwa kwamba hata Lissu apambanishwe na nani huko Jimboni Kwake bado tu atashinda Ubunge hivyo wameamua Kummaliza mapema mwaka huu ili wamuandae Mtu wao ambaye watamuweka kwa Kipindi hiki cha Mpito kisha watamuwezesha Kifedha na Kuungwa mkono ili afanye Maendeleo ya haraka huko Jimboni kwa Lissu ili ateke Akili za wana Jimbo kusudi hadi mwakani Kipindi cha Uchaguzi awe ameshajulikana na kukubalika na wengi kisha agombee tena na apite Kiurahisi na ikibidi hata kwa Nguvu / Mabavu.
Nina mengi bado ya Moyoni ila kwa sasa nimalizie tu kwa Kumshauri Tundu Lissu kuwa hata kama ameamua kuwa anarudi Tanzania hiyo tarehe aliyotaja na Mwezi alioutaja ila namuomba sana awe makini kuliko alivyokuwa huko nyuma na ingekuwa ni Mimi basi kwa huu Upepo na hizi dalili zote za Kikatili na Hujuma Tanzania si sehemu salama tena Kwake na kama angeweza basi angetafuta tu hata Ukimbizi wa Kisiasa nje ya Tanzania au aombe tu kuwa Mhadhiri wa Masuala ya Kisheria Vyuo Vikuu vya Nje ( Ulaya ) na hata Marekani kwani najua kwa IQ yake iliyo Kubwa anauwezo huo au anaweza akajihusisha na Mashirika mbalimbali ya Haki za Binadamu duniani na bado tu akaendelea Kuishi. Simshauri arejee Tanzania hii kwa sasa kwani naiona Hatari Kubwa ya Kiuhai mbele yake kutoka kwa wale wale Watu wasiojulikana ambao sina uhakika kama nao walishauwawa baada Kushindwa Jaribio walilopewa la Kumuondoa au walirudishwa tena Mafunzoni ili Tundu Lissu akirejea Tanzania basi safari hii wasikosee kabisa Target na wahakikishe wanammaliza na kubaki Historia.
Kwa leo yangu ni haya tu ila Tanzania ya leo inanisikitisha na hata kuniliza Machozi.