Huduma zisizorizishwa na Benki yetu ya makabwela NMB

nema manyanya

New Member
Mar 9, 2012
2
0
Ndugu zangu wana JF, leo nina dukuduku kubwa kuhusiana na huduma zinazotolewa na benki yetu ya makabwela NMB hapa tanzania, hasa katika kipindi hiki cha karne ya 21, dukuduku langu ni kama ifuatavyo.

1. Usafirishaji wa fedha toka benki yetu ya makabwela NMB inachukua zaidi ya wiki 1 mpaka mwezi mmoja toka matawi ya nmb kwenda mabenki mengine kama NBC, Azania, crdb n.k hata kama hela hiyo inatumwa kwa TISS

2. Wateja hasa vyama vya ushirika vinavyoshirikiana na mabenki mengine kama nbc, crdb,TIB n.k wanawekewa zengwe sana katika kusafirisha pesa zao toka katika matawi ya nmb kwenda mabenki mengine bila sababu, na wakati mwingine pesa hizo zinacheleweshwa bila hata sababu.

3. Wateja ambao wanakopeshwa na mabenki mengine na mikopo hiyo kutumwa katika matawi ya nmb wanachajiwa Tshs. 5,000/= kwa kila muamala, hiyokweli ni haki??? Mfano NMB Ngara

4. Wateja wengi wanalalamikia sana benki ya NMB kwa kuibiwa katika akaunti zao, na wanapotaka maelezo toka kwa wafanyakazi hawapewa majibu ya kuridhisha, na inatokea mteja kunyimwa hata benk statement ili ajiridhishe.

Tuanomba uongozi wa nmb makao makuu na matawi wafanyie kazi mapungufu haya ili kurudisha imani kwa wateja wenu. Uwingi wa matawi isiwe tatizo la kunyanyasa wateja na kutoa huduma mbofu.
 
NMB Benki hovyo sijawahi ona Tangua nianze kutumia huduma za Mabenki......mfumo we fedha nchini pia mbovu na hulazimisha watu kusongamana Benki huku huduma za Benki zikitolewa kwa mazoea na si ubora, Mpesa, Easy Money, Tigo Pesa, Airtel Oyeeeeeeeeeeeeeeee! mnasaidia kuwatowa wenge hawa Mabenji
 
NMB Benki hovyo sijawahi ona Tangua nianze kutumia huduma za Mabenki......mfumo we fedha nchini pia mbovu na hulazimisha watu kusongamana Benki huku huduma za Benki zikitolewa kwa mazoea na si ubora, Mpesa, Easy Money, Tigo Pesa, Airtel Oyeeeeeeeeeeeeeeee! mnasaidia kuwatowa wenge hawa Mabenji
 
Mteja kwao si Mfalme,huduma mpaka wakujue? Pia hata watu wakilalamika hasikilizwi kamwe.
 
Mteja kwao si Mfalme,huduma mpaka wakujue? Pia hata watu wakilalamika hasikilizwi kamwe.

napata shida sana na jina la benki hii eti ya makabwela wakati huduma hazitolewi ipasavyo kwa makabwela.mfano kuna baadhi ya wateja wanakuta pesa zao zimepungua kwenye akaunti zao,NMB KIBONDO rudisheni pesa za wateja kwenye akaunti zao.pesa za makabwela mnaiba kwenye akaunti zao MUNGU ATAWALANI
 
nilishahamaga siku nyingi hii benki...siku moja nilitaka kutoa milion kadhaa pale tawi la morogoro road...mhudumu badala kunipa hela yangu akawa anatilia shaka kama kweli ile akaunta ni yangu. wakati anaona kabisa picha na sahihi yangu vinaendana sina hamu nao kabisa bora tuwachie wanafunzi wawe wanalipia ada ya shule tu.!
 
hiyo branch hawajui customer care kbs! Mi niliishia kufungua akaunti na kuingia mitini

nilishahamaga siku nyingi hii benki...siku moja nilitaka kutoa milion kadhaa pale tawi la morogoro road...mhudumu badala kunipa hela yangu akawa anatilia shaka kama kweli ile akaunta ni yangu. wakati anaona kabisa picha na sahihi yangu vinaendana sina hamu nao kabisa bora tuwachie wanafunzi wawe wanalipia ada ya shule tu.!
 
Siye tuliolazimishwa kupitisha mishahara benki hii tutakoma. Kuondoka natamani japo siwezi, salariiiiiiiiiii.
 
Back
Top Bottom