Huduma za jamii ndani ya maeneo ya kusubiri kivuko (Busisi na Kigongo) haziridhishi

Sebakujiwe

Member
Jul 2, 2019
47
49
Heshima kwenu nyote wanajamvi.

Kama heading inavyojieleza, huduma muhimu kama chakula na maliwato zipo chini ya kiwango katika maeneo ya kusubiri kivuko ya Busisi na Kigongo hapo chini ya kiwango hali inayopelekea baadhi ya wasafiri kufurahia safari zao.

Mapungufu yaliyopo Ni mazingira kutokuwa masafi katika migahawa iliyopo, vyoo Ni vichafu na havina vifaa muhimu vya chooni kama sabuni za kunawa, tissue papers na hata huduma ya maji safi ya usafi baada ya mteja kutembelea choose/kujusaidia. Hakuna mabomba chooni, maji yanawekwa kwenye ndio na mapipa hali inayopelekea hatari ya magonjwa ya mlipuko na mengineo ya kuambukiza.

Mamlaka husika tunaomba mfanyie kazi.
 
Back
Top Bottom