Huduma za matibabu kwa watoto chini ya miaka mitano ni bure ama inategemea eneo ulilopo?

Kennedy

JF-Expert Member
Dec 28, 2011
48,928
54,146
Salam wana bodi,

Serikali imetutangazia na inaendelea kututangazia kuwa huduma ya mtoto chini ya miaka mitano ni bure ingawa sehemu kubwa ya watoto hutozwa pesa hasa wanapopewa huduma hizo kwenye baadhi ya zahanati,vituo vya afya na hata hospital kubwa za rufaa.

Kwenye hii thread yangu naomba ufafanuzi kwa wataalam wa afya wanaojua ni huduma zipi ambazo ni bure kwa watoto wa umri chini ya miaka mitano.

Na huduma zipi kwa watoto ambao wana umri huo huo unatakiwa usilipe hasa kwenye zahanati, vituo vya afya, hospital za rufaa hasa za serikali.

Kuna hoja nyingi na malalamiko hasa utozwaji pesa ama kwa kujua ama kutojua lolote kipi bure kipi pesa ingawa tumeambiwa hakuna bwana bure sasa hivi.
 
  • Thanks
Reactions: THT
Watawala wanatangaza tu kusherehesha genge. Hata Huduma bure kwa wazee nazo ni hivyo hivyo
 
  • Thanks
Reactions: THT
Watawala wanatangaza tu kusherehesha genge
Hata Huduma bure kwa wazee nazo ni hivyo hivyo
Huu ndiyo ukweli maana hao watoto na wazee naamini wanapoumwa pesa ndiyo ufumbuzi wa kupata tiba ila siyo kauli mbiu ya huduma bure
 
Naamini ni changamoto sana kwa hili

Pia Naibu Waziri wa Afya yupo humu Jamii Forums aje kwenye thread atupe ufafanuzi
 
Sehemu ya Tanzania huduma hizo zipo kwenye maneno ila siyo vitendo kabisa na uzuri ni kuwa wananchi yaani watoto na wazee wanaostahiri huduma hizo hawazipati bure.
 
Watawala wanatangaza tu kusherehesha genge
Hata Huduma bure kwa wazee nazo ni hivyo hivyo
Mkuu Kuna Hii Inayoitwa Bure, Halafu Unaambiwa Hapa Zahanati Dawa Tumeishiwa Maana Ukanunue.

Huelekezwi Sehemu Ya Kupata Bure Iliyo Karibu Nawe
 
Vituo vya Afya vyote huduma kwa watoto chini ya miaka 5 na huduma za uzazi na clinic kwa mama wajawazito ni bure,,

Chamgamoto ni huduma utapewa hasa ya vipimo vya malaria lakini dawa asilimia kubwa hi hazipo hivo inabidi ukajinunulie mwenyewe lakini huduma za kumuona daktari na vipimo ni bure kwa watoto chini ya miaka 5

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Changia gharama za matibabu kwa ajili ya kuboresha huduma za afya
 
Vituo vya Afya vyote huduma kwa watoto chini ya miaka 5 na huduma za uzazi na clinic kwa mama wajawazito ni bure...
Hakuna kitu kama hiki hapa tanzania, nina mfano hai, mtoto wa ndugu 6 months alilazwa tena hospital kubwa tu ya serikali, kila kitu tulikuwa tunalipia, vipimo, dawa n.k, bahati mbaya sana mtoto akafariki, mwisho wa siku tulidaiwa gharama za wodi na dawa kadhaa tulizokuwa hatujalipia, mwili ukapelekwa mochwari, tukazuiwa kutoa mwili hadi tulipie gharama za mochwari....... matibabu bure kwa watoto chini ya miaka 5 ni propoganda tu lkn katika hali halisi hakiapply
 
Hakuna kitu kama hiki hapa tanzania, nina mfano hai, mtoto wa ndugu 6 months alilazwa tena hospital kubwa tu ya serikali, kila kitu tulikuwa tunalipia, vipimo, dawa n.k, bahati mbaya sana mtoto akafariki, mwisho wa siku tulidaiwa gharama za wodi na dawa kadhaa tulizokuwa hatujalipia, mwili ukapelekwa mochwari, tukazuiwa kutoa mwili hadi tulipie gharama za mochwari....... matibabu bure kwa watoto chini ya miaka 5 ni propoganda tu lkn katika hali halisi hakiapply
Pole
 
Vituo vya Afya vyote huduma kwa watoto chini ya miaka 5 na huduma za uzazi na clinic kwa mama wajawazito ni bure,,

Chamgamoto ni huduma utapewa hasa ya vipimo vya malaria lakini dawa asilimia kubwa hi hazipo hivo inabidi ukajinunulie mwenyewe lakini huduma za kumuona daktari na vipimo ni bure kwa watoto chini ya miaka 5

Sent using Jamii Forums mobile app
Hapo Sasa Tuseme Bure Haijakamilika
 
Aisee inategemea Eneo uliliopo,Huku Njombe Ukienda Zahanati ni bure na Ukienda Hospitali ya Rufaa ya mkoa (km hana BIMA)ni malipo kwa kwenda mbele.
 
Back
Top Bottom