Huduma ya Maktaba Tanzania ikoje?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,475
39,991
JUU YA HUDUMA YA MAKTABA YA TANZANIA

maktaba2.jpg

Mheshimiwa Spika, ningependa kumuuliza mheshimiwa Waziri Mhusika maswali yafuatayo ya msingi:

a. Serikali itaanza lini kujenga maktaba mpya na za kisasa katika jiji la Dar ili kuchangia katika upatikanaji wa habari, kuchochea usomaji na kuwapatia wanafunzi na watumishi mahali mbalimbali mahali pa kukusanya taarifa, kufanya utafiti na vile vile kujisomea na kuchochea mapenzi ya vitabu?

b. Je, ni watumishi wangapi wa TLS ambao wana utaalamu katika mambo ya Maktaba na kati yao ni wangapi wako kwenye utawala wa bodi hiyo makao makuu?

c. Je Maktaba kubwa kabisa iliyo chini ya TLS ina uwezo wa kuchukua watu wangapi?

d. Je, maktaba hizi zote zimeuunganishwa katika mtandao wa kikompyuta ambapo unamuwezesha mkazi wa Mbeya kutumia maktaba ya Dar au Arusha au sehemu nyingine yoyote nchini kwa kadiri ya kwamba maktaba ziko chini ya TLS?

e. Kwanini mfumo wa sasa wa maktaba usivunjwe na kuundwa upya ambapo huduma ya maktaba iachiwe halmashauri za miji kusimamia na kugharimia kwa kadiri ya uwezo wao na kuwa watakiwe kisheria kufikia kiwango fulani ili waweze kupata kiasi cha pesa za uendeshaji wa maktaba hizo kuliko mfumo ulivyo sasa ambao uko centralized utadhani tunaishi kati nchi ya udikteta wa chama kimoja cha kisiasa?

Nitarudi tena mheshimiwa spika.
 
Last edited by a moderator:
Mzee Mwanakijiji said:
Hii mitandao itavunjisha ndoa za watu!

Hasa zile zilizo kwenye fungate, mitandao inaweza sababisha Mzee kushindwa kumtoshereza Mama
 
maktaba2.jpg


a. Serikali itaanza lini kujenga maktaba mpya na za kisasa...

b. Je, ni watumishi wangapi wa TLS ambao wana utaalamu katika mambo ya Maktaba

c. Je Maktaba kubwa kabisa iliyo chini ya TLS ina uwezo wa kuchukua watu wangapi?

d. Je, maktaba hizi zote zimeuunganishwa katika mtandao wa kikompyuta ambapo...

e. Kwanini mfumo wa sasa wa maktaba usivunjwe na kuundwa upya...
Kwa hiyo unasema hujui ukubwa wa maktaba hizo, hujui hali na ufanisi wa technolojia waliyo nayo, hujui ujuzi wa wafanyakazi wao, lakini unataka waanze kujenga maktaba mpya za kisasa. Duh...
 
Kwa hiyo unasema hujui ukubwa wa maktaba hizo, hujui hali na ufanisi wa technolojia waliyo nayo, hujui ujuzi wa wafanyakazi wao, lakini unataka waanze kujenga maktaba mpya za kisasa. Duh...

soma kilichoandikwa. Usisome unachofikiria kimeandikwa.
 
Maktaba nyingi zilizopo mikoani na hata Dar zina huduma hafifu. Hakuna vitabu vinavyoenda na wakati, na nafikiri suala la technologia kama internet, matumizi ya cd zenye kutunza taarifa etc bado ni ndoto kubwa kuviona. Kwa ufupi ipo haja ya vyombo husika kufanyia marekebisho makubwa mfumo wa maktaba zetu na kuhimiza watu, hasa vijana mashuleni wawe na tabia ya kupenda kuzitumia maktaba katika kujiendeleza
 
Kwani Dar jiji la watu karibu milioni 3 lina maktaba ngapi (za serikali na za binafsi)?
 
Kwa ukubwa wa jiji letu ilitakiwa sasa hivi tuwe na maktaba si chini ya tano kama hii iliyopo sasa, mikoani pia kuwepo na maktaba kubwa kila wilaya.
 
JUU YA HUDUMA YA MAKTABA YA TANZANIA

maktaba2.jpg

Mheshimiwa Spika, ningependa kumuuliza mheshimiwa Waziri Mhusika maswali yafuatayo ya msingi:

a. Serikali itaanza lini kujenga maktaba mpya na za kisasa katika jiji la Dar ili kuchangia katika upatikanaji wa habari, kuchochea usomaji na kuwapatia wanafunzi na watumishi mahali mbalimbali mahali pa kukusanya taarifa, kufanya utafiti na vile vile kujisomea na kuchochea mapenzi ya vitabu?

b. Je, ni watumishi wangapi wa TLS ambao wana utaalamu katika mambo ya Maktaba na kati yao ni wangapi wako kwenye utawala wa bodi hiyo makao makuu?

c. Je Maktaba kubwa kabisa iliyo chini ya TLS ina uwezo wa kuchukua watu wangapi?

d. Je, maktaba hizi zote zimeuunganishwa katika mtandao wa kikompyuta ambapo unamuwezesha mkazi wa Mbeya kutumia maktaba ya Dar au Arusha au sehemu nyingine yoyote nchini kwa kadiri ya kwamba maktaba ziko chini ya TLS?

e. Kwanini mfumo wa sasa wa maktaba usivunjwe na kuundwa upya ambapo huduma ya maktaba iachiwe halmashauri za miji kusimamia na kugharimia kwa kadiri ya uwezo wao na kuwa watakiwe kisheria kufikia kiwango fulani ili waweze kupata kiasi cha pesa za uendeshaji wa maktaba hizo kuliko mfumo ulivyo sasa ambao uko centralized utadhani tunaishi kati nchi ya udikteta wa chama kimoja cha kisiasa?

Nitarudi tena mheshimiwa spika.

Ni wazo zuri na lenye ukweli hakika. Lakini MMJ watanzania wengi hawana uhakika wa mlo mmoja kwa siku, watawezaje kujenga upendo wa kujisomea?.

Kwa Tanzania si rahisi mtu kufanyia kazi fani yake aliyosomea, na kama yupo basi atashindwa kwani atawekewa vikwazo.

Ni wafanyakazi wangapi ndani ya wizara za serikali wana elimu inayofanana na kazi zao? . Na hiki ndicho chanzo kikubwa cha kuwa na ufanisi hafifu.
Tokana na wazo lako ni vyema tuanzie mawizarani kuangalia elimu na uwezo wa wafanyakazi kabla ya kuangalia hapo TLS, tokana ukweli kwamba utendaji wa TLS una mahusiano makubwa na wizara ya elimu.
 
Ni vizuri umelileta hili la maktaba ,tukumbuke pia na majengo ya Makumbusho
 
watanzania wengi hawana kautaratibu ka kusoma soma!mmoja mmoja sana utaona ameshika hata 'novel'.sasa ivi wataanzania tumeamka TUNAJADILI UFISADI TU!

LOL!
 
Kwa kweli afadhali Maktaba Kuu ya Taifa inaridhisha kidogo kuliko huko tulikotoka. Sehemu za kusomea zimetengenezwa angalau unaweza kupata kitabu kujipinda pale kwa masaa mawili matatu bila bugudha. Na hii nafikiri ni baada ya kumpata mkuu mzuri Dr. Mcharazo.
 
Hii ni biashara ambayo kama Watanzania wangekuwa wanapenda kusoma na kujisomea ingeachiwa ikaendeshwa na watu binafsi kwa ufanisi mkubwa tu. Sioni ni kwa nini hata vyuo vyetu vya elimu ya juu havina maktaba kubwa zinazoweza kutumiwa na wananchi wanaopenda kujisomea na zikawekwa sehemu ambazo zitafikika kirahisi muda wote na siku 7 kwa wiki kwa gharama nafuu.
Ukweli ni kuwa baadhi ya Watanzania wanayo tabia ya kujisomea tatizo ni UKATA tu. Magazeti sasa hivi sio chini sh. 400 ambao ni mlo wa siku nzima wa Watanzania wa kawaida. Enzi za Mwalimu maktaba zilifunguliwa hadi vijijini, vitabu vya akina Musiba tulivisoma kwenye maktaba za vijiji, magazeti ya Uhuru, Mzalendo, Mfanyakazi na hata lile lililokuwa linatoka China, Guoz Shudiani, yalitufikia kule vijijini ingawa yalichelewa.
 
Nakumbuka maneno ya Mwalimu J.K Nyerere, kuwa siku atakapokuwa akitembea kwenye kila nyumba ya mTanzania na kukuta baba, mama na watoto wanasoma vitabu...atajua sasa Tanzania imeendelea.
Watu wanapuuza tu, mbumbu wengi miaka ya siku hizi nikutokana na watu kutokuwa na tabia ya kupenda kusoma!
 
Nakumbuka maneno ya Mwalimu J.K Nyerere, kuwa siku atakapokuwa akitembea kwenye kila nyumba ya mTanzania na kukuta baba, mama na watoto wanasoma vitabu...atajua sasa Tanzania imeendelea.
Watu wanapuuza tu, mbumbu wengi miaka ya siku hizi nikutokana na watu kutokuwa na tabia ya kupenda kusoma!

Ndugu yangu huwezi kufikiria kusoma vitabu kama chakula hakuna. Familia nyingi ndani ya Tanzania mlo moja kwa siku ni shida. Watapata wapi wazo la kufikiria kusoma wakati tumboni hakuna kitu?.

Mimi nilipata bahati ya kufundisha watu wazima enzi zile za ngumbalu sijui kama unakumbuka. Kuwapata watu darasani ilikuwa ni shida kubwa. Sababu kubwa ilikuwa ni kwamba wamekwenda kutafuta mlo kwa ajili ya familia. Pamoja na kwamba tulikuwa na tabia ya kuita majina kujua nani yupo na nani hayupo darasani ili kutoa taarifa kwa serikali za vijiji, lakini bado tuliona wazi kwamba watu hawaji madarasani bila ya kuwa na uhakika wa mlo wa familia kwa siku ile.

Ingekuwa busara sana kwa Nyerere kama angefikiria kuwalisha kwanza hawa familia then awape vitabu. Bila shaka wangesoma na kuvielewa vitabu vyema kabisa.
 
Ndugu yangu huwezi kufikiria kusoma vitabu kama chakula hakuna. Familia nyingi ndani ya Tanzania mlo moja kwa siku ni shida. Watapata wapi wazo la kufikiria kusoma wakati tumboni hakuna kitu?.

Mimi nilipata bahati ya kufundisha watu wazima enzi zile za ngumbalu sijui kama unakumbuka. Kuwapata watu darasani ilikuwa ni shida kubwa. Sababu kubwa ilikuwa ni kwamba wamekwenda kutafuta mlo kwa ajili ya familia. Pamoja na kwamba tulikuwa na tabia ya kuita majina kujua nani yupo na nani hayupo darasani ili kutoa taarifa kwa serikali za vijiji, lakini bado tuliona wazi kwamba watu hawaji madarasani bila ya kuwa na uhakika wa mlo wa familia kwa siku ile.

Ingekuwa busara sana kwa Nyerere kama angefikiria kuwalisha kwanza hawa familia then awape vitabu. Bila shaka wangesoma na kuvielewa vitabu vyema kabisa.[/QUOTE]

Nadhani umesema vema, ila pia naona umeishia njiani kutafakari. Ukienda mbele zaidi, kusoma huleta maarifa mengi hadi jinsi ya kujipatia chakula..hata kama unakula Muhogo mmoja kwa siku jitahidi kusoma ukipata muda utaona tu faida zake. Hili la kuwalisha watu woote kwa muda woote hata MANABII mmaarufu sana hawakuweza!
 
Haya bwana, lakini ni vigumu sana hata kupata huduma ya internet kw wanafunzi wa chuo Kikuu maana unaweza kupata huduma hiyo kupitia internet
 
kusoma huleta maarifa mengi hadi jinsi ya kujipatia chakula..hata kama unakula Muhogo mmoja kwa siku jitahidi kusoma ukipata muda utaona tu faida zake. Hili la kuwalisha watu woote kwa muda woote hata MANABII mmaarufu sana hawakuweza![/QUOTE]

Nahisi kuna baadhi ya ndugu zetu watanzania hamjui kabisa hali za watanzania wenzenu, hivi kweli unaweza kutoa wazo hili eti soma tu hata ukipata mhogo mmoja, ndugu yangu tema mate chini kama haujawahi kuisikia njaa au umebahatika kupitiwa mbali na janga hili.
 
Back
Top Bottom