Chini ya Uangalizi wa Wizara ya Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana kupitia wakala wake wa Ajira (TaESA), Callix InfoTech ikishirikiana na Push Mobile Media Ltd imezindua rasmi huduma ya PATA KAZI ambapo watu wataweza kupata kirahisi na kwa unafuu nafasi za kazi nchini kote kwa kutumia simu zao za mikononi wakati wowote na popote pale walipo.
Huduma hii ni kwa wateja wa Vodacom, Zain na Tigo. Uongozi upo mbioni kushirikiana na Makampuni mengine ya simu.
Kufaidi urahisi wa huduma hii mtumiaji atahitajika kujiunga kwenye kundi au aina ya kazi anayotafuta halafu baada ya hapo ataweza kupata taarifa za kazi anayohitaji mara kwa mara mpaka atapopata au atapohitaji kujitoa kwenye huduma hii.Kwa mfano kujiunga Andika neno Kazi au Ajira acha nafasi ikifuatwa na jina la kazi unayotafuta halafu utume kwenda kwenye namba 15522.Mfano:Kazi Dereva kwenda namba 15522. Kujitoa andika Kazi Ondoa kwenda kwenye namba 15522.