Huduma ya kuletewa maji kwa matumizi ya nyumbani - kwa water tanker

Manyovu

Member
May 20, 2011
78
71
Wadau,

Heshima yenu. Mie naishi Arusha maeneo ya Maji ya Chai. Kwa wale ambao tunaishi wote hapa au wanalisikia ni kuwa ipo shida kubwa ya maji. Jitihada zangu zote za kuona kama naweza kupata maji mpaka kwangu zimeshindikana mpaka sasa.

Kwa sababu hiyo nimeona bora niamue kuuliza kama naweza kupata huduma ya kuwa naletewa maji kwa gari zile zinazotoa huduma hii. Kwa maana ya kuwa kila mwezi angalau lita 10,000 -15,000. Anayejua kama huduma hii naweza kuipata naomba anisaidie kunipa mawasiliano na bei inaweza kuwa ngapi kwa kiasi hicho cha lita/trip.

Natanguliza shukrani
 
Wadau,

Heshima yenu. Mie naishi Arusha maeneo ya Maji ya Chai. Kwa wale ambao tunaishi wote hapa au wanalisikia ni kuwa ipo shida kubwa ya maji. Jitihada zangu zote za kuona kama naweza kupata maji mpaka kwangu zimeshindikana mpaka sasa.

Kwa sababu hiyo nimeona bora niamue kuuliza kama naweza kupata huduma ya kuwa naletewa maji kwa gari zile zinazotoa huduma hii. Kwa maana ya kuwa kila mwezi angalau lita 10,000 -15,000. Anayejua kama huduma hii naweza kuipata naomba anisaidie kunipa mawasiliano na bei inaweza kuwa ngapi kwa kiasi hicho cha lita/trip.

Natanguliza shukrani
ukiwa mjanja kidogo tu utagundua kuwa kwa hiyo hela utakayotumia kulipia maji kila mwezi inatosha kulipia mkopo benki wa kuchimba kisima na pump ya solar mradi ambao utakupatia maji ya bomba nyumbani mwako bila kuwategemea ccm na magamba yao. jaribu siku zote kufikiria kwa mapana na utafanikiwa kuboresha maisha yako pamoja na familia
 
Ongea na jamaa wa Maji Tech pale momela wakuchimbie kisima.
Au nenda pale garage kwa mchau uulizie Tanker flani hivi ya njano iko jirani nao
 
Jamani,
Sio kila mahali ukichimba pana maji!!
Tungeanza kwanza na kuangalia uwezekano wa kupata maji hapo.
 
Asante kwa walioshauri kuchimba kisima, bahati mbaya plot yangu ni ndogo kiasi kwamba hakuna sehemu ya kuchimba hicho kisima.

Puppy nashukuru nitaenda kuuliza kuhusu hiyo tanker unayosema, ungekuwa na namba zao za simu ningeshukuru zaidi.
 
kaka kuchimba kisima siyo lazima uwe na kiwanja kikubwa, mambo yamerekebishwa sana bomba linachimbiwa chini urefu hata metre 72 mpaka 90 unapata fresh water. usikate tamaa jaribu kuukataa umaskini kwa kujitegemea.
 
kaka kuchimba kisima siyo lazima uwe na kiwanja kikubwa, mambo yamerekebishwa sana bomba linachimbiwa chini urefu hata metre 72 mpaka 90 unapata fresh water. usikate tamaa jaribu kuukataa umaskini kwa kujitegemea.

Gogozito: Mimi niko Dar maeneo ya Tabata Segerea sasa maji huku ni issue na nikiangalia maji yote yanayopatikana ni ya chumvi. unaweza kutuelimisha kidogo ukichimba hizo metre 90 ni lazima upate fresh water? na kama unafahamu gharama za uchimbaji na gharama zingine za vifaa. Hebu tujuze kidogo tuone kama tunaweza kataa umasikini kwa kujitegemea. Nimepita hapa Ministry of Water - Agencies - sijaona masaada wowote.
 
Back
Top Bottom