sinzahome
New Member
- Apr 25, 2019
- 2
- 5
Mimi ni mteja wa Benki ya CRDB zaidi ya miaka 10 sasa, maana kwa ninavyokumbuka niko pale kama mteja wao tangu mwaka 2008,
Tangu nilipoijua CRDB mwaka 2008 huduma walizokuwa wanatoa ndio zilinifanya nijiunge na benki yao, ila kwasasa huduma wanazotoa zitanifanya niikimbie benki yao na kurudi kule nilikokuwa kwa maana kuna nafuu wa huduma bora za Kibenki kuliko hii CRDB ya sasa, Huduma zake kwa wateja zimekuwa mbovu kupindukia hadi kuna kuda namkumbuka DKT. CHARLES KIMEI, hadi kuwa najiuliza tuu hivi huyu mzee aliondoka na Benki yake au? Kama hali yenyewe ndio hii ya sasa sisi wateja tutakimbia wengi na kwa mtazamo wangu miaka 10 ijayo hii benki wasipo angalia inaelekea kufa kabisa.
HUDUMA MBOVU Mfano: Kadi za ATM za wateja wa CRDB zilizoisha Muda wake za tangu mwaka jana Novemba 2019 mpaka sasa Machi 2020 kwa wateja wao wa Tanzania nzima hawajapatiwa kadi mpya za kuendelea kufanya huduma za kifedha kwa kutumia KADI ZA ATM, ni malalamiko tuu kila siku kwa wateja ukienda Tawi lolote la Benki hiyo na majibu wanayotoa wafanyakazi ni hata wao hawajui hizo kadi zitakuja lini, mimi najiuliza Tuu Benki kubwa kama CRDB kweli Kadi za ATM tuu ndio zinawateteresha hivyo hii hatari.
Yako mengi tuu ya hiyo benki ila kwa sasa tuongelee hili linalokiki huko kwao ambalo kwa ukubwa wa CRDB Benki linanishangaza, kuna madudu kama kwenye mikopo, foleni kubwa benki kuliko hata benki Fulani Fulani zile tulizokuwa tunazilalamikia au kuzihama huko awali, n.k
Nadhani DKT. CHARLES KIMEI toka aondoke mwaka 2018 ameondoka na Benki yake maana huduma zimekuwa mbovu kupindukia tofauti na wakati wake alipokuwepo, na kinachonifanya niamini kuwa DR.KIMEI ameondoka na benki yake, ni tangu aondoke huduma za benki hiyo zimekuwa zinaporomoka kila siku iendayo kwa Mungu. Natamani DKT CHARLES KIMEI huko aliko sasa arudi CRDB hata Wiki 1 tuu aje kuweka mambo sawa maana hali ya Benki kwa sasa ni tete saaaaana.
Namshauri BW. ABDULMAJID NSEKELA awasiliane na DKT. CHARLES KIMEI ampe mbinu za benki alivyokuwa akiiongoza maana utendaji yeye wa sasa toka aachiwe kiti unaishusha Benki siku hadi siku
IMETOLEWA KWAKO na Mpenda Benki ya CRDB kimaendeleo.
Mlioko CDRB mna mchango gani?
Tangu nilipoijua CRDB mwaka 2008 huduma walizokuwa wanatoa ndio zilinifanya nijiunge na benki yao, ila kwasasa huduma wanazotoa zitanifanya niikimbie benki yao na kurudi kule nilikokuwa kwa maana kuna nafuu wa huduma bora za Kibenki kuliko hii CRDB ya sasa, Huduma zake kwa wateja zimekuwa mbovu kupindukia hadi kuna kuda namkumbuka DKT. CHARLES KIMEI, hadi kuwa najiuliza tuu hivi huyu mzee aliondoka na Benki yake au? Kama hali yenyewe ndio hii ya sasa sisi wateja tutakimbia wengi na kwa mtazamo wangu miaka 10 ijayo hii benki wasipo angalia inaelekea kufa kabisa.
HUDUMA MBOVU Mfano: Kadi za ATM za wateja wa CRDB zilizoisha Muda wake za tangu mwaka jana Novemba 2019 mpaka sasa Machi 2020 kwa wateja wao wa Tanzania nzima hawajapatiwa kadi mpya za kuendelea kufanya huduma za kifedha kwa kutumia KADI ZA ATM, ni malalamiko tuu kila siku kwa wateja ukienda Tawi lolote la Benki hiyo na majibu wanayotoa wafanyakazi ni hata wao hawajui hizo kadi zitakuja lini, mimi najiuliza Tuu Benki kubwa kama CRDB kweli Kadi za ATM tuu ndio zinawateteresha hivyo hii hatari.
Yako mengi tuu ya hiyo benki ila kwa sasa tuongelee hili linalokiki huko kwao ambalo kwa ukubwa wa CRDB Benki linanishangaza, kuna madudu kama kwenye mikopo, foleni kubwa benki kuliko hata benki Fulani Fulani zile tulizokuwa tunazilalamikia au kuzihama huko awali, n.k
Nadhani DKT. CHARLES KIMEI toka aondoke mwaka 2018 ameondoka na Benki yake maana huduma zimekuwa mbovu kupindukia tofauti na wakati wake alipokuwepo, na kinachonifanya niamini kuwa DR.KIMEI ameondoka na benki yake, ni tangu aondoke huduma za benki hiyo zimekuwa zinaporomoka kila siku iendayo kwa Mungu. Natamani DKT CHARLES KIMEI huko aliko sasa arudi CRDB hata Wiki 1 tuu aje kuweka mambo sawa maana hali ya Benki kwa sasa ni tete saaaaana.
Namshauri BW. ABDULMAJID NSEKELA awasiliane na DKT. CHARLES KIMEI ampe mbinu za benki alivyokuwa akiiongoza maana utendaji yeye wa sasa toka aachiwe kiti unaishusha Benki siku hadi siku
IMETOLEWA KWAKO na Mpenda Benki ya CRDB kimaendeleo.
Mlioko CDRB mna mchango gani?