KERO HR vyuo vikuu vya Tumaini Makumira na Tumaini Dar es Salaam (Dartu) kuna tatizo gani? Mnaita watu kwenye interview halafu mnapotea mazima. Kulikoni?

KERO HR vyuo vikuu vya Tumaini Makumira na Tumaini Dar es Salaam (Dartu) kuna tatizo gani? Mnaita watu kwenye interview halafu mnapotea mazima. Kulikoni?

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Huoni kama ni Mungu aliufunga huo mlango ili upate huko kwingine kwenye perdiem?

Malalamiko yetu yasiyo na sababu huwa yanamkwaza sana Mungu.
Unataka kusema mtoa mada analalamika bila sababu? Sababu anayo sana,ni kuhusiana na feedback,ni jambo muhimu kujua nini kinaendelea

Feedback haina umuhimu kwenye mapenzi pekee,uliyemtongoza atakupa feedback kwa namna nyingi ikiwemo kukukalia kimya tu
 
Unataka kusema mtoa mada analalamika bila sababu? Sababu anayo sana,ni kuhusiana na feedback,ni jambo muhimu kujua nini kinaendelea

Feedback haina umuhimu kwenye mapenzi pekee,uliyemtongoza atakupa feedback kwa namna nyingi ikiwemo kukukalia kimya tu
Angeweza kutoa ujumbe wake vizuri tu pasipo na malalamiko.

Wanaotoa feedback za kazi ni wachache sana mkuu.

Hata wenye hizo sheria za kazi ILO wanaweza wasikupe feedback vilevile.

Kuanza kuleta habari za kutumia 300k ilikuwa lazima upate hiyo kazi?
 
Huoni kama ni Mungu aliufunga huo mlango ili upate huko kwingine kwenye perdiem?

Malalamiko yetu yasiyo na sababu huwa yanamkwaza sana Mungu.
It is a matter of principle. Unafikiri mimi ndiyo mwathirika pekee wa hiki kinachoendelea? Na hao wengine ambao hawakupata kwingine? Siyo sawa kumuingiza mtu gharama za kusafiri kutoka Bukoba mpaka Arusha kuja kufanya interview feki huku ukijua kuwa nafasi uliyotangaza tayari ina mtu wako ambaye ulimpata kupitia connection. I may be an exception lakini kwa wengine je? Na kumjulisha huyu aliyeingia gharama kuja kwenye hizi interview fake kwamba hakupata hiyo kazi ili apate closure nayo ni ngumu?

Unapomuingiza Mungu jaribu kupanua wigo wa kufikiri. Wrong is wrong hata ukimsingizia Mungu!

Na hakuna anayelalamika hapa!
 
Angeweza kutoa ujumbe wake vizuri tu pasipo na malalamiko.

Wanaotoa feedback za kazi ni wachache sana mkuu.

Hata wenye hizo sheria za kazi ILO wanaweza wasikupe feedback vilevile.

Kuanza kuleta habari za kutumia 300k ilikuwa lazima upate hiyo kazi?
Hao ambao hawatoi wanafanya makosa sana,lakini busara na hekima ni kutoa feedback hata kwa mstari mmoja tu kama alivyosema mtoa mada

Kuheshimu muda wa mtu,jitihada yake na utu wake ni jambo muhimu sana,binafsi sioni kama mtoa mada kalalamika sana,lkn kama kwa mtazamo amelalmika sana ni sahihi pia,just imagine kaspend almost 300,000, hiyo ni pesa mingi sana
 
Angeweza kutoa ujumbe wake vizuri tu pasipo na malalamiko.

Wanaotoa feedback za kazi ni wachache sana mkuu.

Hata wenye hizo sheria za kazi ILO wanaweza wasikupe feedback vilevile.

Kuanza kuleta habari za kutumia 300k ilikuwa lazima upate hiyo kazi?
Nimelalamika wapi? Hebu nionyeshe jinsi ambavyo nilitakiwa kuandika ili nisionekane kama nalalamika.

Siyo lazima nipate hiyo kazi na hilo nalijua vizuri. Lakini hata kujulishwa kuwa sikupata napo ni tatizo?

"We are sorry to inform you that you were not selected for the job you applied for" ni ngumu kumtumia mtu akapata psychological closure ili aendelee na mambo yake mengine? Tena kwa taasisi ya kidini? Ingekuwa kiwanda cha Mo labda. Lakini taasisi ya kidini? Yenye upendo na compassion? Wewe unamuabudu Mungu gani ambaye ni katili na anayeweza kuingiza watu gharama za kusafiri kutoka Bukoba mpaka Arusha kuja kwenye interview feki? Ni mlokole gani wewe?
 
This is so unprofessional kwani kwa kawaida tumezoea mtu ukishapenya mpaka kuitwa kwenye interview angalau basi unajulishwa kama umepita ama la - hata kama ni kwa mstari mmoja tu (You were not selected!).
Oral haipo hivyo mkuu ila pole sana kwa hilo next time ukifanya oral baada ya hapo wewe vunga tu endelea na shughuli zingine wala usisikilize kwamba labda utaitwa itatokea km bahati tu umepigiwa simu basi ndio inakua hivyo kinyume na hapo potezea, ni mashirika machache sana hufanya hivyo kwa kukujulisha kupitia email ila meengine mengi hukaa kimya na ukiona kimya ni kirefu basi jua kwamba haikua bahati yako ni bahati ya mtu mwingine piga moyo konde songa mbele sahau kuhusu hio nafasi
 
It is a matter of principle. Unafikiri mimi ndiyo mwathirika pekee wa hiki kinachoendelea? Na hao wengine ambao hawakupata kwingine? Siyo sawa kumuingiza mtu gharama za kusafiri kutoka Bukoba mpaka Arusha kuja kufanya interview feki huku ukijua kuwa nafasi uliyotangaza tayari ina mtu wako ambaye ulimpata kupitia connection. I may be an exception lakini kwa wengine je? Na kumjulisha huyu aliyeingia gharama kuja kwenye hizi interview fake kwamba hakupata hiyo kazi ili apate closure nayo ni ngumu?

Unapomuingiza Mungu jaribu kupanua wigo wa kufikiri. Wrong is wrong hata ukimsingizia Mungu!

Na hakuna anayelalamika hapa!
Mkuu ishu ni feedback au interview feki?

Wakati unatoka kwenu ulishajipa asilimia za kukutosha kuwa kazi ni ya kwako?
 
Unataka kusema mtoa mada analalamika bila sababu? Sababu anayo sana,ni kuhusiana na feedback,ni jambo muhimu kujua nini kinaendelea

Feedback haina umuhimu kwenye mapenzi pekee,uliyemtongoza atakupa feedback kwa namna nyingi ikiwemo kukukalia kimya tu
Mtoa mada hakuwa tu na uvumilivu, yeye mwenyewe kasema kuwa alipiga simu akaambiwa awe na subira mchakato haujakamilika! Nimeona malalamiko kama haya kwa watu waliofanya interview serikalini nako kuna tatizo kama hilo.
 
Mkuu ishu ni feedback au interview feki?

Wakati unatoka kwenu ulishajipa asilimia za kukutosha kuwa kazi ni ya kwako?
Kabla hujaanza kuuliza maswali yasiyo na kichwa wala miguu soma bandiko langu - na maoni ya wadau waliotoa ufafanuzi kwa kinachoendelea kwenye hizi taasisi za KKKT. Vinginevyo tutakuwa tunapiga makitaimu bila sababu za msingi.
 
Oral haipo hivyo mkuu ila pole sana kwa hilo next time ukifanya oral baada ya hapo wewe vunga tu endelea na shughuli zingine wala usisikilize kwamba labda utaitwa itatokea km bahati tu umepigiwa simu basi ndio inakua hivyo kinyume na hapo potezea, ni mashirika machache sana hufanya hivyo kwa kukujulisha kupitia email ila meengine mengi hukaa kimya na ukiona kimya ni kirefu basi jua kwamba haikua bahati yako ni bahati ya mtu mwingine piga moyo konde songa mbele sahau kuhusu hio nafasi
Na huwa wanamachaguo kadhaa, sasa yeye anataka feedback ya oral interview, inawezekana hata alikuwa chaguo la tatu au la pili.

Wakutumie we regret, halafu itokee wale wa kwanza hawaja show up, wakikurudia inawezekana?
 
Nimelalamika wapi? Hebu nionyeshe jinsi ambavyo nilitakiwa kuandika ili nisionekane kama nalalamika.

Siyo lazima nipate hiyo kazi na hilo nalijua vizuri. Lakini hata kujulishwa kuwa sikupata napo ni tatizo?

"We are sorry to inform you that you were not selected for the job you applied for" ni ngumu kumtumia mtu akapata psychological closure ili aendelee na mambo yake mengine? Tena kwa taasisi ya kidini? Ingekuwa kiwanda cha Mo labda. Lakini taasisi ya kidini? Yenye upendo na compassion? Wewe unamuabudu Mungu gani ambaye ni katili na anayeweza kuingiza watu gharama za kusafiri kutoka Bukoba mpaka Arusha kuja kwenye interview feki? Ni mlokole gani wewe?
Mkuu hio siku hizi haipo na hua hawatumi kuna mtu mmoja aliwahi kuniambia nilipomuuliza sababu maana na yeye yupo kwenye hio michakato ya kuajiri akaniambia kwamba sasa hivi yaan kwa sasa hivi wanaoajiri wanaringa sana kwa sababu watu ambao hawana ajira ni weeeengi yaan kuna lundo la watu weengi wanaohitaji ajira kwa hio sasa hivi hawabembelezi mtu yaan ukimaliza interview umemaliza na hawana time na wewe sababu kuna lundo la watu wengi wapo hawana ajira kwa hio hujibiwi hata kwa email km ilivyokua zamani unaachwa tu huambiwi chochote sababu watu ni weeengi
 
Na huwa wanamachaguo kadhaa, sasa yeye anataka feedback ya oral interview, inawezekana hata alikuwa chaguo la tatu au la pili.

Wakutumie we regret, halafu itokee wale wa kwanza hawaja show up, wakikurudia inawezekana?
Kazi niliyoomba tuliofanya interview tulikuwa wawili tu maana ni eneo ambalo ni nadra kidogo (halina watu wengi japo sasa hivi watu ndo wanalichangamkia). Na haikuwa na hatua nyingine. Ndiyo maana nilitegemea kama wangekuwa ni professionals basi wangetoa feedback.

Nilipotoka pale niliomba sehemu nyingine (NGO ya nje). Hapa tulikuwa watatu na waliniambia mimi nilikuwa wa pili. Wako very transparent. Na walipomchukua yule aliyekuwa chaguo lao la kwanza wakaniambia kuwa amesha-accept. Nikaomba kwingine na nikapata moja kwa moja.

Sema tu sisi tunafanya mambo kiholela na nepotism kila mahali lakini haya mambo yanapaswa kuwa transparent tu. Na ukijaribu kuyaweka wazi matokeo yake ndiyo kama hivi unapingwa. Ndiyo maana ni ngumu sana kuleta mabadiliko katika jamii zetu hizi.
 
Kazi niliyoomba tuliofanya interview tulikuwa wawili tu maana ni eneo ambalo ni nadra kidogo (halina watu wengi japo sasa hivi watu ndo wanalichangamkia). Na haikuwa na interview nyingine maana ni ngazi ya juu kidogo. Ndiyo maana nilitegemea kama wangekuwa ni professionals basi wangetoa feedback.

Nilipotoka pale niliomba sehemu nyingine (NGO ya nje). Hapa tulikuwa watatu na waliniambia mimi nilikuwa wa pili. Wako very transparent. Na walipomchukua yule aliyekuwa chaguo lao la kwanza wakaniambia kuwa amesha-accept. Nikaomba kwingine na nikapata moja kwa moja.

Sema tu sisi tunafanya mambo kiholela na nepotism kila mahali lakini haya mambo yanapaswa kuwa transparent tu. Na ukijaribu kuyaweka wazi matokeo yake ndiyo kama hivi unapingwa. Ndiyo maana ni ngumu sana kuleta mabadiliko katika jamii zetu hizi. Kabisa kabisa hakuna ulazima wa kumsafirisha mtu kutoka Bukoba mpaka Arusha huku mkijua kuwa kuna mtu wenu wa connection.
Una uhakika mlikua wawili au siku uliyoenda kufanya interview ulikutana na mwenzio mmoja mkawa wawili? Sikia mkuu simple fact ni kwamba ushapata sehemu nyingine km ulivyosema sasa kwanini kuikosa hii nafasi ikuume zaidi sababu ni nini? Sababu ni kutoka Bukoba hadi Arusha tena mara moja? Hivi kuna uzi uliusoma humu wa jamaa alitoka Mwanza mpaka Dodoma na alipofika Dodoma bora angefanya km wewe na asipewe majibu yeye hakufanya kabisa walimkatalia na kumwambia hana vigezo vya kufanya interview hivi maumivu hayo na maumivu haya yapi yanauma zaidi au yanafanana? Nimekwambia mimi niliuliza kwanini siku hizi inakua hivi nikaambiwa kwamba sababu ni wingi la watu wasiokua na ajira kwa hio waajiri wana uwanda mpana wa kuchagua ukiringa wanaita wengine kwa hio ni wewe kuwanyenyekea

Soma hapa uelewe:
IMG-20260606-WA0001.jpg
 
Una uhakika mlikua wawili au siku uliyoenda kufanya interview ulikutana na mwenzio mmoja mkawa wawili? Sikia mkuu simple fact ni kwamba ushapata sehemu nyingine km ulivyosema sasa kwanini kuikosa hii nafasi ikuume zaidi sababu ni nini? Sababu ni kutoka Bukoba hadi Arusha tena mara moja? Hivi kuna uzi uliusoma humu wa jamaa alitoka Mwanza mpaka Dodoma na alipofika Dodoma bora angefanya km wewe na asipewe majibu yeye hakufanya kabisa walimkatalia na kumwambia hana vigezo vya kufanya interview hivi maumivu hayo na maumivu haya yapi yanauma zaidi au yanafanana? Nimekwambia mimi niliuliza kwanini siku hizi inakua hivi nikaambiwa kwamba sababu ni wingi la watu wasiokua na ajira kwa hio waajira wana uwanda mpana wa kuchagua ukiringa wanaita wengine kwa hio ni wewe kuwanyenyekea

Soma hapa uelewe:
View attachment 3603425
Masikini sisi. Sijui tutabadilika lini! Wewe unaona ni sawa kufanyiwa hivyo? Kwa nini wenzetu huwa hawafanyi hivyo? Hata kama kuna waombaji wengi basi mtawekewa disclaimer pale pale kwenye tangazo la kazi kwamba:

1. Tutawasiliana na watu ambao watakuwa shortlisted pekee
2. Ukishafanya interview tutawasiliana na candidates tutakaowachagua pekee. Ukifanya interview na usipotusikia basi jua kuwa hukupita.

Kwisha kazi na mtu unakuwa unajua kinachoendelea. Sasa wewe unaniambia nilinganishe maumivu. Kwani ni lazima kuwa na maumivu? Ili iweje? Kwani sisi hatuwezi kufanya mambo yetu transparent bila makandokando? Hata hawa jamaa zako hapa chini walifanya jambo jema maana angalau ulijua kinachoendelea.


Screenshot_20260608_090520.jpg

Mtu umefanya interview. Wakati huo huna mishe nyingine kabisa na unakuwa na mategemeo kibao. Unasubiri wee kimya. Uzalendo unakushinda unauliza unaambiwa kwamba uamuzi bado haujatolewa. Miezi inapita. Unauliza tena unaambiwa hiring committee haijaa kufinalize mambo. Miezi sita inaisha na unaamua kupotezea. Kwa nini kama walishachukua mtu mwingine wasiseme tu ili nawe ukaendelea na mambo yako? Kama wanaweza kukuandikia kujieleza kuwa process bado, wanashindwaje kukwambia kwamba hukupita? Wewe unaona hii ni sawa?
 
Mtoa maada yupo sahihi kama alikosa inabidi mtu ajulishwe na kingine kama wanataka kuajiri mtu wa dini yao au mchaga mwenzo wangesema umekosa kisa we sio dhehebu letu, mchaga na hata kama hakufaulu

Kama taifa tupende kuwajibika watu wengi wanamshambulia mtoa maada wakati hamna alichokosea
 
Mtoa maada yupo sahihi kama alikosa inabidi mtu ajulishwe na kingine kama wanataka kuajiri mtu wa dini yao au mchaga mwenzo wangesema umekosa kisa we sio dhehebu letu, mchaga na hata kama hakufaulu

Kama taifa tupende kuwajibika watu wengi wanamshambulia mtoa maada wakati hamna alichokosea
Ndugu yangu. Kubadilisha mambo kwenye jamii zetu hizi ni tatizo kubwa. Watu wamezoea shida na mambo kwenda hovyo hovyo. Huwa namwangalia Lissu anavyoteseka gerezani wakati mwingine naishia kumhurumia tu maana watu anaotupigania mh!

Kuna ubaya gani hawa waajiri wetu wanaoita watu kwenye interviews kuwa na tabia ya kutoa feedback kama mtu wamemchukua au wamemuacha. Kama hawawezi basi angalau waweke disclaimer pale kwenye tangazo lao la kazi moja kwa moja ili kuondoa mikanganyiko na stress za kisaikolojia.

Mtu unauliza wanakwambia process bado zinaendelea kumbe walishachukua mtu mwingine alishaanza na kazi. Hii ni sawa? Kwa nini wasiwe tu transparent? Tena taasisi ya DINI?
 
Nimekwambia hio ilikua kipindi cha nyuma miaka ya nyuma huko sio siku hizi siku hizi hawajibu chochote ukituma km ikichelewa interview au kukiwa na mabadiriko yoyote huambiwi kitu chochote wala ukifanya interview km hujapita huambiwi kitu chochote km ilivyokua zamani miaka ya nyuma walikua wanatuma email kwanza ukituma tu maombi unapokea email ya kukushukuru kwa kufanya maombi kisha ukishafanya interview wanakwambia kwa email unajulishwa kwamba umepita au la hujapita na sababu unaambiwa kabisa kwanini haujapita na wanakwambia watakutafuta next time wakihitaji mtu mwenye sifa km zako imeishia hapo hii unafunga email unaendelea na habari zingine, siku hizi haipo hivyo ukituma maombi hata email ya kukushukuru tu kufanya maombi haipo hawajibu kitu na kujibiwa napo mtihani mwingine kwa hio ndio ishakua hivyo tuendane tu na hali jinsi ilivyo hakuna muda wa kulalamika
Unaongelea taasisi gani? Baada ya kuachana na hawa watu wa KKKT niliomba kwenye NGO mbili na zote walikuwa very transparent. Sasa unaposema kuwa siku hizi hawafanyi hivyo unaongelea akina nani? Unaongelea hizi taasisi za kibabaishaji, Ajira Portal au akina nani? Na wewe ni msemaji wa waajiri wote maana naona umekazana kweli kweli!

Hata kama siku hizi hawafanyi hivyo ndiyo tunataka wabadilike sasa na warudi kama zamani. Kama hawataki kujibu kila mwombaji kwa kisingizio eti waombaji ni wengi basi angalau wawe wanaweka disclaimer kwenye tangazo la kazi kabisa ili kuondoa mikanganyiko. Sioni ugumu wo wote wa kuweka maangalizo haya kwenye tangazo la ajira:

1. Tutawasiliana na watu ambao watakuwa shortlisted pekee
2. Ukishafanya interview tutawasiliana na candidates tutakaowachagua pekee. Ukifanya interview na usipotusikia basi jua kuwa hukupita.

Hii nayo bado ni ngumu kutekeleza Mr. HR?
 
Back
Top Bottom